Saturday, March 30, 2024

ELEWA 2

 

Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa kuelekezwa,kimfumo kumtafuta mtu kwenye kundi ni ngumu,ili kutofautisha kama kuna mwizi,malaya au mlevi ni kuangalia alipoiba aliekea wapi maana vyote vinaweza kuwa vya mtu mmoja.

Sifa mbovu inayotembea ni sawa na rungu la kichwa ukiwa usingizini, katika miliki matendo mabovu yamekuwa yakitendeka bila woga kuliko mawazo ya mazuri,anayekusifia mazuri hadharani anakusubiri utoke,yule asiyekusifia ana ubaya wake mwingine wa kuelezea.ukigeuka watakwambia hawajakuita na hata wakikuita hawana cha kukwambia.

Kuna namna ipo umefanana na wazazi wako,hata isipokuwa sura basi hasira,tabia wengi wametokea utotoni usimlaumu mtu kwa  kuwa malaya vile unavyojisikia kunywa pepsi mwingine coca,vingine vipo ndani ya damu hivyo tembo akinya sogea mbali pengine uchafu utakumwagikia alafu iabidi uelewe kufuata yako.

Kuna muda huelewi,yaani hata nilichokiandika hauelewi,tatizo lisije kwangu maana ulivyovijaza kichwani mwako vyaweza kuwa kinzani na hivi,nikawa naandika kwa kutumia wino mweupe.kuna mmoja alisema yanatoka popote bila kujua yametokea wapi,ukitaka kupaa kuwa na mahusiano ya karibu na ndege.Usipojua yanatoka wapi jaribu kuwaelewa ndege kwanza.

Watu ni zaidi ya chochote,yoyote yule umwonaye.hata sifa zangu hakuna nzuri imekuwa kwa mwengine,maana kila mtu ananjia yake mafanikio sio utu,ukitaka pesa watakutesa.unapotaka kunielewa isiwe kwa mlengo wako,mtu akitaka kukuelewa asikuelewe anavyokuelewa Ukiishi usimwambie na mwenzio baadaye atajiita kuwa mshauri.

ELEWA 1

Usidharau upendo unaoupata,sio kila kinalengwa kinalengeka,ukiona mchele umeota kwenye maji kuna ardhi chini ,haihitaji nguvu kupanda mbegu,itakuchosha mapema na utapoteza furaha yako vivo hivyo,asikwambie mtu kucheka wakati mrefu wa kununa ni nguvu tosha na ikakupa amani muda wote.

kama hakuna jibu kwanini uliingia kwenye mdomo wa mamba basi utakuwa unaishi nao,kujua kuogelea sio kuitii kiu ya maji ya kunywa,sehemu nyingine za kuogelea kuna mamba,wazee hupendelea sana swimming pool,sehemu za kuogelea ndogo ,vijana hujitupa maziwani na mabaharini na wakifika katikati hushituka na kujilaumu,na huo huwa msingi wa kubomoka.

Kuna maziwa na bahari nyingine zina ghasia sana,utaratibu mtu mmoja lakini wao huwapanga hata ishirini,mawimbi yanatoka popote kwenye mwelekeo,bora swiming pool mawimbi utayaleta wewe.wanasema saidia uendelee na safari,ni vile unatoa dhaka na mchungaji anaenda kununua shamba ili alime apate chakula cha kuuza na familia.

Elewa kwamba sio yote unayoyaona lazima uyaelewe,hata kama umeyasoma sio lazima uyaelewe,elewa wengine wa kuwaacha,kataza moyo wako kushikamana na matendo,Elewa duniani kuna watu watataka kwa lazima kufikiria tofauti ya wewe unavyofikiri ili wao kuonekana tofauti.

Wednesday, January 24, 2024

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO: Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahal...

Makaya's Forum: HASIRA YAKO

Makaya's Forum: HASIRA YAKO: Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinak...

Tuesday, January 16, 2024

HASIRA YAKO

Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinakupeleka,binadamu tupo tofuti,mmoja hali nyama ya mbuzi kwa kuwa inamtoa vipele mwengine hali nyama ya nguruwe kwa sababu ya dini sasa nikikasirika usiniulize nimekasikia nini,nina mengi.

Kasirika,usikarike pasipo na sababu.upumbavu wa mtu mmoja usikufanye uvunje simu na mwengine kufikia kumkata mtu panga.angalia unapokasirika sauti yako ya ndani inakwambia nini na kabla haujatenda kwa kutumia kiungo chochote cha mwili yakupasa kutafakari,maana kuna wale wenye hasira za ndani(chuki) hawafanyi mambo yao hadharani.

kama ilivyo katika michezo mmoja akamchezea rafu mwenzake basi wanamichezo waliiga kwenye maisha,na ndiyo maana unasikia michezo haiitaji hasira,ukisusa wenzako wanakula na wenzako huwa wanakula mpaka baadaye ukakitamani tena hicho chakula,kasirika vizuri.

Dunia hadaa utakasirishwa wakitaka kujua maamuzi yako,ukishajua umekasirikia nini maamuzi yako yawe tofauti na hasira zako kwani kweli maisha yana mengi lakini kuna mengine sio ya kukasirikia fikiri mtu anakasirikia mafanikio yako na atayekumbatia maamuzi ya hasira zako yampasa kuwa yeye.

ISHI NA YAKO

Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahala fulani,tambua maisha yana stepu,uliyopo sasa mwengine alipita juzi ukicheka leo mwenzako kulia ni sawa na kulia wakati mwenzako anacheka.

Usibabaike na waliowahi kufikia ukitakacho,tambua muda wako ikiwa unajiandaa jiandae vyema ili ukikosa isiwe lawama kwa wengine,maana imekuwa mmoja akishindwa akatoa sababu za mwengine kumuangusha.

Usifikiri ni raisi kukaza jambo,kuna mengine yanakaza mpaka kufungua inakuwa kama ni kukaza,ujiandae vyema maana kuna vilio,maumivu yasiyo na machozi na hata usumbufu usiohitajika.yatambue magumu yako na jipe muda kuyatatua ikiwa humu duniani wote mpaka muda huu tunatafuta maisha.

Kheri udongo unarudi utokapo maana ingekuwa foleni kubwa barabarani kwa kuwapa heshima wajionao miungu,usifikiri wakati wa magumu peke yake mwishowe ukawapa lawama watu wasio husika na maisha yako,tambua nafasi yako si ile aisemeayo mwengine,watu huwa wanaongezea kwa kile ulichonacho.

Monday, October 9, 2023

Makaya's Forum: NAONA

Makaya's Forum: NAONA: Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni ...

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...