Monday, January 30, 2012

TUBADILISHANE KILE TUNACHOKIFANYA NA SIKU


Yanayofanyika ni matendo,kwa mtenda ndiyo ikafahamike haswa,ikiwa naye mtendwa akifaahamu zaidi kutoka kwa mtenda,yaani ilikuwaje sio mawazo haya ya kila siku uliyonayo lakini ndio baadhi yanayopelekea kutenda,yote ni matendo tu,ikiwa siku zinaenda wengi wetu ukiendelea kufanya vile unavyovifanya ili mradi siku ikapita,ikawe ili mradi sio tu ndiyo yapite bure,bure isiyo ya pesa,bure ikawe ya kutokufanya jambo kwa siku hiyo,kwani kama unabadilishana vinaenda wapi?yaani hivi vibovu na yale mazuri kwani kuyafikia na yenyewe yanahitaji siku iwe nzuri,itakavyo kuwa ndiyo jinsi ya kuelewa ielewekavyo,

Utasumbuka endapo ukitaka kubadilisha mazuri yawe mabaya,kwani ni uadui utakuwepo hapo,usije kosea na kubadilishana hewa,ili kesho ukapumue na wakati unazo tokea kuzaliwa,kipindi na cha kukifahamu ili ukabadilishane na vile vizuri,maana kipindi hichi kimekuja kinamna nyingine,siku hizi sio kama za zamani,wale wa zamani wanajua hilo yaweza kuwa nao hawaelewi kipindi chao,maana siku zao walibadilishana vyema,ikawe mbuzi kwa ng’ombe,naye mfanyabiashara akalizika kwani alitafuta mbuzi ili abadilishane na ng’ombe.

Ikiwa ni leo sijui kesho kutwa itaitwaje,maana mabadiliko yaliyofanyika ni ya leo tu,kesho ilisemekana watakuja wengine,lakini nao bado hawajaandaliwa ikiwa nao wakija wataanza yao,hata ukawa ni upepo ni lazima ujue unavumia wapi,ikaja hadithi uwahadithie ulikuwa unatokea pande ya kulia na kuelekea kushoto,zote ni pande nzuri labda iwe ujiamini leo na kesho,hapa ukitaka kufahamu ubora mwingine ulio wa zaidi ya leo na kesho.

Siku ni muda,kesho ni siku ya pili,muda huu ukauite wa kwanza ikiwa unategemea wa pili uje ukiwa umejiandaa kwa muda huo au useme muda wowote,usifike mbali wakati mwanzo unaonekana,ikiwa anayeanza hufikiri mwanzo bora iyo ikawe siku,maana hata kesho ikija itakuwa na yake,yale uliyoyapanga na haya mengine yatakayokuja,lazima yaje kwani wengine wanakufikiria kwa yale ya kesho na sio leo,utatafutana huko na usipokuwepo watakutafuta wakufunike,kwani hata walizani wao wamelala wakaandaa na mashuka kumbe yalikuwa ni yetu,unaposhindwa kurudia mema na kusahau mazuri ni kama pale unapofikiria yale maovu yaliyotuumiza siku za nyuma,yule anayefanya kazi bila kuomba mshahara anategemea kulipwa mengi,ikiwapo na mshahara wake mwenyewe.maana hakuupata,na hakuna kazi isiyo na mshahara,labda siku zipite ili ujue nini haja ya mshahara,tena sijui umekujaje baada ya kufanya kazi.

Wanaopaka ina wakiwa na yetu majina ,siku zimepita nyingi mengine yafutike,ikiwa mengine sio ya kuyatendea,utajiuliza kama ni kweli zimepita,bila kukanana pengine huwafahamu wasichana,kwa urembo wazee kuonekana vijana,hata ya jana yasingewezekana,muda mwingine inakuwa ni kujifunza kwa kuchanganyana,siku za zamani watoto ndio walieleweka kutokujua,maana nyingine hata hizo zilizopita zinaweza zisifike kwa wale wenye watoto kujisifu ikiwa ni wana wazazi kama wao,siku zinavyozidi kwenda utafahamu tu,labda uchelewe lakini ni lazima ufahamu ingawaje mpaka sasa umechelewa.

Lengo ni siku kupita,iwe imeeleweka kinamna yeyote.yule anayesema ameelewa vile aiambie siku yake,maana ndicho kitakuwa cha muhimu kwake..

By: Benson G. Makaya,
Tel: +255 714 33 66 57.
email:bensonsmakaya@gmail.com

No comments:

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...