Wednesday, July 11, 2012

ELIMU MTAANI..

Elimu ni kuweza kukua katika uelewa,hapo nikitaka wengi ama waliokusudika kufika mahala wanapopapenda,kwa namna iliyo moja hadi nyingine ikiwa ni yoyote,kwa chochote kinachoweza kutokea  kulingana na mazingira yaliyopo ama vile nikayaita hayo yenyewe mazingira ni elimu,elimu mtaani ni ‘experience’ tosha,inatosha kwa kusoma haya yaliyopo mtaani maana ndiyo mwongozo ,kwani Yule anayekosa hukosa wapi?umetaka kufundishwa shuleni ukasahau makosa,umejifunza usiyoyajua na kuacha usiyotakiwa kuyajua,hatutakiwi kutenda makosa

Mtaa kwani wa nani?hivi wengine hatupiti mitaa ile maana kuna wakabaji sana,imeitenga halisi kwa kutaka vya rahisi,leo kabeni na mkiongezeka japo siku ifike arobaini na tano,maana arobaini zinapita sana,siku zinabadilika,yale yaliyomtaani kufahamika kama si ya kihalali,ikiwa watu hawana kwa kula wala kulala mahali,siwezi kuuliza ni lini itakuwa ‘graduation’ ya elimu yetu ya mtaani,kwani kumekuwa na mafanikio,yasiyohitaji cheti.

Leo mitaa imejaa sana.tena hapa haijatofautishwa kwa vile wale ni wazee ama ni vijana,au watoto imetutaka kusoma pamoja maana kinachofanyika ni kile kimoja na haina haja ya kukosea kwa kufanya vile ilivyo tofauti na mkubwa wako,maana tofauti hiyo ni ‘experience’jaribu uone ili kufikisha taarifa katika mitaa,maana sio kuonekana tu hadi kufikirika,utakuwa ni mtu wa hivyo maana ikawa unatofautisha mtu aliye na 'certificate' na Yule asiyenacho,elimu mtaani haina mwisho,elimu mtaa haijali muda wala umri hata mzee wa miaka mia anaweza kuwa darasa la kwanza,ni kwa sababu madarasa hupanda na kushuka,leo kwako na kesho kwangu.


No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...