Wednesday, September 26, 2012

UNAPOIANZA SAFARI


Kupitia kutumika ama ilivyo kama inasemekana kuishi ikiwa ni katika ngazi tofauti mwanadamu unapokuwa katika kuelekea mafanikio ya safari yako,mengi husemeka na wengi pale mwanzo unapoanza,ikiwa ni maisha yako inakupasa kabla ya kujipa tumaini la kujua kama ipo siku,kama mambo yalikuwa tofauti basi yataenda utakavyo,maana nzuri yangu mimi ndiyo inayoweza kutuletea ugomvi hasa ikaonekana kama nilipo ni mwanzo.

Kila mtu ana lake la mwenzako haipaswi kulinyemelea,safari ni yako hasa zaidi kama imetokea umeifanya bila kujua unashuka kituo gani ni bora kuuliza katika Yule unayeona umefanana naye kimaisha,pengine ukiwa unapata vyanzo vya kukufanya uweze lakini ‘kwa kuwa fulani kasema basi ile itakuwa mbaya’,na ubaya wa safari unategemea na kujiandaa kwako pengine ukiwa kama ulikuwa ni wakupanda milima alafu ukavaa suti,lazima kuonekane namna ya kutokufikiri sahihi,isipokuwa mlengwa usipojilaumu juu ya safari yako.

Mengi yanapotokea hutokea ya kuwa ni rafiki ama ndugu hawa wakiwa ni baadhi katika vile vinavyofanya safari ieleweke ipo katika namna gani,haraka hufanya ajari na ikawa hata unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako,hatari ya safari  imekuwa baada ya safari yenyewe kuanza,fikiri uwezo wako maana wanaokatisha tamaa ya maisha wapo karibu yako tena kila mtu akijifanya mjuaji,mtu unapojifanya unajua jua unajua ya kwako ya mwengine mwache aende nayo kwani kujilaumu kwa kukosa hupewa moyo na siyo mtu kaa mbali na kuwa makini na maisha ya mwenzako,kama huwezi jambo hakuna faida ya maneno na wakati muda unataka kusema yake.

No comments:

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...