Wednesday, November 7, 2012

MAZURI YANGALI KUJA.

Hapa nazungumzia nafsi ya kila mmoja,ikiwa hata wewe leo ukaelewa iwe katika ndoa namna ya vile maisha yanavyokuwa iwe katika hali ya kutokuwa katika ndoa na kukuta maisha yako vile vile jinsi yalivyo,maisha bado kwa wengine yakiwa ya uadui tu,ikiwa unawaza kuanguka kamwe huwezi kuiona siku yako ya mafanikio.maana mazuri huja baada ya kipimo chako cha kufanikiwa,pale ukaishi maisha mengi na yaliyo jaa vingi,pale umetegemea mengi lakini hakuna katika yale uliyoyafikiria  kutenda na kutokea,maana waweza fanya mia leo na kesho kuja moja na kudhani yale mia yalikuwa ni kanuni,mazuri yangali njiani,mazuri yangali kuja maana kama umefikiri sahihi lazima kuielewa ile maana ya kwanza yaani sababu.

Kama yalikuja basi hongera maana pengine sijui mtu unaishi ukifikiria nini,waweza kuota ndoto na kulazimisha kutokea,ikiwa umezani wewe ni mkuu sana kwa nafasi uliyopo,ukijisahau kwa kuwa  fikra zako ni zimekujaa wewe pekee,kumbuka hakuna mtu anayemfikiria mwenziye katika namna mwenziye anavyomfikiria,ukiambiwa  kuongea peke yako yapasa kuelewa hasa unaposikia ukidhani rahisi ama magumu yote.mazuri yangali kuja,hayo magumu ndiyo njia ya kwenda kuzuri,ukiwa na furaha sasa jua ni yale marahisi yamewezakana,ikiwa mazuri yangali  kuja.

Furaha ya mchizi ni kufurahi,pengine furaha ya mchizi ni anaifahamu mwenyewe,ikiwa umeona mazuri siyo ya kwamba yamekuja ,angalia kesho usijenuna na kupewa lawama,maana si furaha yako unaijua mwenyewe,anayeamini anapata maana anakuwa ametaka akifikiri yatakayotokea,ikiwa mwanzo wa jambo basi una mwisho,wanaposema Mungu hamtupi mja wake siyo kila mtu ni mja wa Mungu,maana Mungu wa mmoja si mmoja yule wa amwaminie mwengine na pengine kesho ifikirike ili ya jana yakaonekana ni tofauti.

Mazuri yangali kuja...!!

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...