Saturday, February 4, 2012

UZURI.



Katika kila kitu kuna sifa,ili kitu kiweze kujisikia kwamba ni kitu kinahitaji sifa,sio kila sifa ni nzuri,wala sio kila uzuri ni uzuri,inaweza ikawa ni hivyo kimaandishi na maneno yalivyo lakini katika maana ikatoka tofauti na uzuri ulivyo,uzuri  ni kwa uzuri tu.Katika yote mazuri huwa juu ya watu,kwa watu haipendezi kukawa na uzuri bila ya watu kuwa wazuri,ikiwa watu tunatakiwa kuendana na vile tuvifanyavyo au tunavyoweza kuvimiliki,ikiwa mtu ana chake tunaweza kutofautisha uzuri ikiwa na watu pia tuko tofauti,ikiwa katika mavazi na undani wetu zaidi,kwani sio wote wanaovaa vizuri kuonyesha vyao,ieleweke kuvaa vizuri sio kupendeza kwani wengine hufurahisha maumbile na mioyo kwa kuvaa wawezavyo ikiwa ni tofauti na uzuri,mavazi ndiyo yanayomfanya mtu aonekane katika namna inayompendeza yeye,mavazi ndio humtambulisha mwanaadam,tena tusifike mbali kwa kuulizia jinsia maana mavazi tunayaona wenyewe.

Wanaocheka sasa baadae wanaweza kutafuta wao,kama lengo ni kuuelewa uzuri.tukiwa tunajifahamu ni sisi tusitake na wengine watujue tusijifanye tupo juu wakati ni chini tusipopajua,tutaumia tukiwaza mazuri yamepita bila kuonekana wakati ni sisi wenyewe tulikuwa katika mabaya,ingawaje haikupendeza kwa mabaya kuongeleka pengine yangekuwa ni sawa na yale mazuri,labda utofautishaji tu,ni kama pale tunapoimba na kusoma na ifike kipindi tusielewe kama tulikuwa tunaimba ama tunasoma,kwani muda mzuri wa kufikiri yote hayo ungekuwa ule wakati hasa kabla ya kutenda,ingawaje sio kosa,na hakuna wa kumpa mwenzake lawama kwani kila mtu ni mzuri katika upande wake.

Lugha huwa zinachanganya sana,tatizo sio kusikika,tatizo sio njia ya mawasiliano,tatizo ni kusikia,kivingine tumeweza kusikika tofauti na vile maana ya mtu inavyoweza kumjia ikiwa tunasikia kwa lugha nzuri na safi,kama ni mbaya basi inapaswa kubadilishwa,maana hata sasa tumekuwa tukijitahidi kufahamu lugha nyingine,na hapa tuone uzuri,ya kuwa sio ile ya kwanza haifai bali na ya pili imekuwa bora,na ya tatu mwishowe tutakuja kugundua zote ni nzuri ila utofauti ni pale katika matumizi ya lugha hizo,ikiwa wengine wanatumia lugha chafu haimaanishi ni wachafu,labda lugha chafu ilitumika kumwambia mtu aache uchafu wake,lugha ile inaweza kuonekana ni nzuri kwa mchafu,yakuwa ni yake.

Nguvu haibadilishi rangi,kile kinachokuwa kibaya baada ya kupungua basi ni kizuri maana ni kimepungua tu,kumbe itafika kipindi tunaweza kujaza uzuri wetu hadi mioyoni,maana imekuwa kama ni sura tunazibadilisha,maumbile tunayaweka vile tunavyotaka wabaya waone vizuri,yaweza kuwa nasi ni wabaya  na tunatenda ili tuonekane tumefanya vizuri,lakini katika yote ni heli tumefanya,maana tusiogope kujifunza,ikiwa watu wanajenga madaraja sio kwa ajili wapiti peke yao,na kwa kile chochote kilicho kibaya kimetendeka nasisi tukajifunze juu  ya hicho,tusije kunywa sumu na haya maisha yalivyo magumu,maana siku hizi tunapona,tatizo linakuja katika kuendelea kuishi kwani mtu aliyekata tama anastaili falaja,lakini hawa wa kutoa faraja nao wamekuwa wafanyakazi,wanatafuta mshahara ingawaje mwanzo waliweza,na ndiyo maana ya kufika mpaka muda huu

Tuiache imani ibaki kama dhamana,ikiwa ni lazima turudi na kufanya yale mazuri ya maana.

By:      Benson G. Makaya,
Tel:     +255 714 33 66 57.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...