Wednesday, September 26, 2012

UKAMILIFU..


Kuna ulazima wa kuchagua wewe ni nani ikiwa unataka kukamilika,pengine ukiwa na malengo,mipango yako iliyokamilika na ikitakikana kufanyika ama imeshafanyika na wanadamu kuona namna ya vile ilivyotendeka ikiwa wao ndiyo huleta makamilifu ya sifa,chako ni chako,kichafu na kisafi ni vyote vilivyo kamilika ikiwa ni katika namna inayotakiwa,kwani pale anapopenda mmoja mwengine anaweza penda hapo ilipo ya kuwa ni katika kukamilisha matokeo.

Mabaya huwa ni mazuri kwa kuwa yameweza kuwa na uwezo wa kuwa mabaya .kukamilika ni namna ya kitu kilivyo,na endapo hakijakamilika ni lazima kupeana namna ili inapokuwa inataka kukamilika iweze kukamilika katika namna na maana ya vile ilivyo.pengine ni utofauti unaofanya mtu asiwe na ukamilifu,akiamini yeye ndiyo yeye,kwa kuweza jambo na wengine kushindwa.hayajawa mashindano maana hata muda wa mchezo wenyewe unapangwa na  wewe mwenyewe.

Maisha yanajengengeka na namna ya ukamilifu wako,ikiwa haujatimiza jambo na unahisi ya kwamba si mkamilifu basi jaribu kukamilika kwa kuweka kile unachokihitaji kukifanya kuwa kama ni baba au mama maana hakuna pengine pa kuwapata,si ndiyo ikawe fulani ni mtoto wa fulani na fulani,si vile ikawa haieleweki  kwa kutokukamilisha uzazi,na ki ubainadamu wengi hupenda kujikamilisha na kutokukamilisha ya wengine.wakijua yao yamekamilika.

UNAPOIANZA SAFARI


Kupitia kutumika ama ilivyo kama inasemekana kuishi ikiwa ni katika ngazi tofauti mwanadamu unapokuwa katika kuelekea mafanikio ya safari yako,mengi husemeka na wengi pale mwanzo unapoanza,ikiwa ni maisha yako inakupasa kabla ya kujipa tumaini la kujua kama ipo siku,kama mambo yalikuwa tofauti basi yataenda utakavyo,maana nzuri yangu mimi ndiyo inayoweza kutuletea ugomvi hasa ikaonekana kama nilipo ni mwanzo.

Kila mtu ana lake la mwenzako haipaswi kulinyemelea,safari ni yako hasa zaidi kama imetokea umeifanya bila kujua unashuka kituo gani ni bora kuuliza katika Yule unayeona umefanana naye kimaisha,pengine ukiwa unapata vyanzo vya kukufanya uweze lakini ‘kwa kuwa fulani kasema basi ile itakuwa mbaya’,na ubaya wa safari unategemea na kujiandaa kwako pengine ukiwa kama ulikuwa ni wakupanda milima alafu ukavaa suti,lazima kuonekane namna ya kutokufikiri sahihi,isipokuwa mlengwa usipojilaumu juu ya safari yako.

Mengi yanapotokea hutokea ya kuwa ni rafiki ama ndugu hawa wakiwa ni baadhi katika vile vinavyofanya safari ieleweke ipo katika namna gani,haraka hufanya ajari na ikawa hata unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako,hatari ya safari  imekuwa baada ya safari yenyewe kuanza,fikiri uwezo wako maana wanaokatisha tamaa ya maisha wapo karibu yako tena kila mtu akijifanya mjuaji,mtu unapojifanya unajua jua unajua ya kwako ya mwengine mwache aende nayo kwani kujilaumu kwa kukosa hupewa moyo na siyo mtu kaa mbali na kuwa makini na maisha ya mwenzako,kama huwezi jambo hakuna faida ya maneno na wakati muda unataka kusema yake.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...