Wednesday, February 15, 2012

Makaya's Forum: SAUTI KALI...

Makaya's Forum: SAUTI KALI...: Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje kihalisi imet...

SAUTI KALI...



Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje kihalisi imetimia,labda upate mawaidha,yaani utiwe moyo,unaweza kuleta usikivu na ikiwa hivyo ukakaa chini na kufikiria,lakini isiwe hadi kufika kilele,maana hapo nguvu zinapungua,uwezo wa kufikiri unatokana na nguvu pia,na hapa ikaeleweke sio wazee wanawasemea,ni vijana mkaweze kukaa na kuweza tazamia,milango usifunge,makelele yatakuzidia,ingawa ulikuwa hujui ya mwanzo yaliyokufikia,usingeliyafahamu hata kwa nguvu kupayukia,vile sauti  kuwafikia,labda ufikirie  na kwa makini kusikilizia,tunavutiana kwa namna isiyowezekana,na hii itatupelekea kukaa kimya sana,hata ukaweka utamu wa lugha kwa jinsi zinavyojulikana,haita leta msingi zaidi ya watu kupigana,ikiwa wengi wanasoma shule yale ya mtaani yamekuwa hayana maana,ingawa ni yetu ya leo na wala siyo ya jana,tumekuwa wazembe wenyewe haina haja wa zamani kuwatukana,hata ukatembea mbali kutafuta nyama,majani yatakuotea karibu na kuchafua bila hiyana,unahangaika kwa pesa na zimekuwa hazina dhamana.ikawekwe barabara iliyo jaa rami kama mkeka,faida ya nani kama siyo ya malaika?maana imekuwa ikipita siku chache na kubomoka,sijui ni raslimali au ujuzi wa kutokujali,ntaongelea machache yasiyo kuwa na hali,siyo yale ya wanaume wasio lijali,ni wazi kwa mwenye vichache apaswe kuongezewa,maana ni anavyo vichache kweli,ile ya mwenye nacho kuongezewa ni ya watu hai,wafu lao kaburi,na maombezi ndiyo nyongeza yao,nao wafike salama mahala pema mbinguni.

Mambo yanapozidi kuwa magumu ndiyo mwanzo hasa wa yale maraisi,ni kile alichonacho mwanaadamu,ingelikuwa kila mtu anazaliwa anaambiwa nenda kaendeshe baiskeli sidhani kama angetoka mtu na kusema ni rahisi,tena bila kufundishwa..kwani hata hiyo baiskeli yenyewe ingelikuwa ngumu kuitaja bila ya kuiendesha,mbadala wa matembezi yanayotoa sugu miguuni ni mapumziko ya viungo hivyo,hawakuchoka hawa wanaotengeneza baiskeli tangia mwanzo,wakarahisisha mpaka wakaweza kusafiri nazo,sio uwezo ni namna ya kuweza na kigezo,inapochakaa baiskeli makelele huanza,ukapita mikoa mbalimbali kama mbeya na mwanza,baiskeli zinapokuwa kitu cha kwanza,ni maendeleo haya kwani hakuna aliyeyakataza,barabara zikaonekane hazina maana kwani hata mijini ukawawekea bado ni mtafaruku kwa wao kupita yapitapo magari,na ikiwa ni mmoja wapo watakupigia kelele ya kuwa unaleta foleni.mambo ya mjini ni mengi,lakini mji huo huo ndiyo kijiji,sasa uchague moja kati ya kijiji au mji,maana unaona watu wanatoka morogoro wanakuja kutibiwa hospitali ya mkoa dare s salaam,wale wa dar na wenyewe wanafanya hivyo,mshangao kwa wale wanaosafiria nje magonjwa yao,kenda rudi ni maralia na baada ya hapo ni mapumziko..kule hakuna kelele tatizo hapa ni pale unapopumzikia kodi za watu huku wenyewe wakiwa hawazijui hata haki za kwenda hospitali,sauti kali huleta ugomvi kwa kutokuelewana,na baadaye ni vita.

Macho yasitoboke,masikio yameziba sasa wanaopiga kelele waendelee,maana hata ukikataa sauti zenu hazipayuki na haipiti siku,pigeni kelele wanafunzi na mwalimu akija mwambieni ni kwa sababu hakuwepo,maana hujifanya kuelewa yao mara nyingine,hata hivyo ikiwa ni namna ya kutaka kujua ni nini kifanyike mda huo.

By:Benson G.Makaya
Tel:+255714336657
Email:bensonsmakaya@gmail.com


ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...