Wednesday, February 15, 2012
Makaya's Forum: SAUTI KALI...
Makaya's Forum: SAUTI KALI...: Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje kihalisi imet...
SAUTI KALI...
Sauti zimezidi kuwa kubwa,zimejaa na chumba ni
kidogo,ikabaki ikawa na sasa imekuwa ni mtafaruku,sio mda wake huu,ingawaje
kihalisi imetimia,labda upate mawaidha,yaani utiwe moyo,unaweza kuleta
usikivu na ikiwa hivyo ukakaa chini na kufikiria,lakini isiwe hadi kufika
kilele,maana hapo nguvu zinapungua,uwezo wa kufikiri unatokana na nguvu pia,na
hapa ikaeleweke sio wazee wanawasemea,ni vijana mkaweze kukaa na kuweza
tazamia,milango usifunge,makelele yatakuzidia,ingawa ulikuwa hujui ya
mwanzo yaliyokufikia,usingeliyafahamu hata kwa nguvu kupayukia,vile sauti kuwafikia,labda ufikirie na kwa makini kusikilizia,tunavutiana kwa
namna isiyowezekana,na hii itatupelekea kukaa kimya sana,hata ukaweka utamu wa
lugha kwa jinsi zinavyojulikana,haita leta msingi zaidi ya watu kupigana,ikiwa
wengi wanasoma shule yale ya mtaani yamekuwa hayana maana,ingawa ni yetu ya leo
na wala siyo ya jana,tumekuwa wazembe wenyewe haina haja wa zamani
kuwatukana,hata ukatembea mbali kutafuta nyama,majani yatakuotea karibu na
kuchafua bila hiyana,unahangaika kwa pesa na zimekuwa hazina dhamana.ikawekwe
barabara iliyo jaa rami kama mkeka,faida ya nani kama siyo ya malaika?maana
imekuwa ikipita siku chache na kubomoka,sijui ni raslimali au ujuzi wa
kutokujali,ntaongelea machache yasiyo kuwa na hali,siyo yale ya wanaume wasio
lijali,ni wazi kwa mwenye vichache apaswe kuongezewa,maana ni anavyo vichache
kweli,ile ya mwenye nacho kuongezewa ni ya watu hai,wafu lao kaburi,na maombezi
ndiyo nyongeza yao,nao wafike salama mahala pema mbinguni.
Mambo yanapozidi
kuwa magumu ndiyo mwanzo hasa wa yale maraisi,ni kile alichonacho mwanaadamu,ingelikuwa kila
mtu anazaliwa anaambiwa nenda kaendeshe baiskeli sidhani kama angetoka mtu na
kusema ni rahisi,tena bila kufundishwa..kwani hata hiyo baiskeli yenyewe
ingelikuwa ngumu kuitaja bila ya kuiendesha,mbadala wa matembezi
yanayotoa sugu miguuni ni mapumziko ya viungo hivyo,hawakuchoka hawa
wanaotengeneza baiskeli tangia mwanzo,wakarahisisha mpaka wakaweza kusafiri nazo,sio
uwezo ni namna ya kuweza na kigezo,inapochakaa baiskeli makelele
huanza,ukapita mikoa mbalimbali kama mbeya na mwanza,baiskeli zinapokuwa kitu
cha kwanza,ni maendeleo haya kwani hakuna aliyeyakataza,barabara zikaonekane
hazina maana kwani hata mijini ukawawekea bado ni mtafaruku kwa wao kupita
yapitapo magari,na ikiwa ni mmoja wapo watakupigia kelele ya kuwa unaleta
foleni.mambo ya mjini ni mengi,lakini mji huo huo ndiyo kijiji,sasa uchague
moja kati ya kijiji au mji,maana unaona watu wanatoka morogoro wanakuja
kutibiwa hospitali ya mkoa dare s salaam,wale wa dar na wenyewe wanafanya hivyo,mshangao
kwa wale wanaosafiria nje magonjwa yao,kenda rudi ni maralia na baada ya hapo
ni mapumziko..kule hakuna kelele tatizo
hapa ni pale unapopumzikia kodi za watu huku wenyewe wakiwa hawazijui hata
haki za kwenda hospitali,sauti kali huleta ugomvi kwa kutokuelewana,na baadaye
ni vita.
Macho yasitoboke,masikio yameziba sasa wanaopiga kelele
waendelee,maana hata ukikataa sauti zenu hazipayuki na haipiti siku,pigeni
kelele wanafunzi na mwalimu akija mwambieni ni kwa sababu hakuwepo,maana
hujifanya kuelewa yao mara nyingine,hata hivyo ikiwa ni namna ya kutaka kujua
ni nini kifanyike mda huo.
By:Benson G.Makaya
Tel:+255714336657
Email:bensonsmakaya@gmail.com
Subscribe to:
Comments (Atom)
Makaya's Forum: ELEWA 2
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
POPURAL POSTS
-
Makaya's Forum: KATAA : unaweza ukawa unakataa mazingira uliyonayo,ukajikataa,ukakataliwa ama ukakatalika hiyo yote ikaonekaa kwa kuwa ...
-
Eti kuwaza sana ni vibaya,nawaza sana nakuwa na mawazo nawaza sana yaliyo mema nawaza sana kuongeza kupata maisha sio kama ya fulani bali y...
-
Na kama ni ndani ya familia iwe ni mzazi ama mtoto ndiye anayemwambia mmoja wapo hapo ujue kuna namna,ile iliyokuwa kama vile katika n...
-
Kizazi kinachokuja ni kizazi kinachosoma kupitia yale tuliyoyafanya!pengine isitoke lawama kama kuna upotevu wa namna yeyote ikiwa wal...
-
Matatizo yanayochangia watu kuachana yako mengi, ambayo mtu unaweza kujaza vitabu kuyaelezea, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi ...
-
Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...
-
Maana bado inaendelea,hali kuwa ngumu.ikiwa kwa mara ya kwanza tulipoambiwa tukajifanya tumeelewa tena sasa tunaambiwa turudie tunashin...
-
Muda ukiwasili palipo inatakiwa kuelekea, maana ikiwa ni kufanya hata kwa ilivyo kwa namna ya kuweza kuutenganisha muda ili uje kule...
-
When I was a child, I saw how a magnifying glass could burn a piece of paper, when the rays of the sun were focused through it. The fir...
-
With the goal of reaching the understanding must arrive in an environment where you say its your time and to each of us to hear there, ...