Monday, July 30, 2012

MVUTO.


Navutiwa na kuona watu wanafuraha maana ni furaha kwangu pia,inanivutia kuona watanzania wameamka na kuacha kulalama,inavutia kweli kwa kuona yale magumu angalau watu wameanza kuyafanya,hapo hata kama hayawezekani lakini kuna imani na tumai ya kuliweza japo moja,hii ni kwakuwa tumeweza kukua katika upande fulani wa maendeleo,ikiwa pamoja na vizazi kuongezeka.

Pengine inavutia sana kwa kuona watu wakijishugulisha kwa vile maisha ni magumu,maana ingalikuwa ni kula tu isingelikuwa na maana ya kuvutiwa na majengo na mambo ya mjini,ingawaje tunasema mjini kuna upatikanaji wa mahitaji kiujumla na zaidi ni haki tumevutiwa na vitu hivyo,pengine tunataka tuwe nani lazima tufanye vile vinavyotuvutia,labda ikija badaye vitarudisha fadhila ikiwa na sisi tutavutia.

Unapofanya yale ya kwako ni kufanya ngazi nyingine katika kupanda maisha yako,tunaposema maisha ni yako ya maana ukifa leo wengine watabaki ikiwa walivutiwa tofauti,ingawa ni vigumu sana kwa mwanadamu kusema kile kinachomvutia kabla ya kufanya,pengine wengine wataogopa,wakisema mbona ya kwako hukusema,haihitaji nguvu katika kuonyesha kile mtu unachopendezwa nacho ni akili na msimamo ya kuwa ni wazi kufanyika.

ONA.

Zungumza katika uwezekano wako,kama vile maumbo yanapokuwa na pembe na kona zake,vile ikafuatwe ikiwa pembe kali,tena nyingine zinazungumzika kama ni zawadi kwa sababu tumekuwa tegemezi katika yale yanayokuwa yetu,inaweza kufika kipindi ukatafuta namna na njia mpya ya kuishi hii ikiwa mtu ameona siri iliyo moyoni ya mafanikio yake..ikiwa katika heshima,uelewa,kujiamini,kujua na hata kufanya ili mradi kufikia malengo fulani.

Ikiwa katika miaka hata maelfu kupita ni uchache wa watu kuonekana wakiwa na moyo mwema yaani wengine tumebaki kuwa washabiki,ikiwa kama ni vita basi tutapigwa tutakufa,kama ni njaa zitatuuma mpaka vidonda,kama ni umbali basi ni kama kuzunguka poli ikiwa kilometa hazijulikani,tutaenda na kurudi tulipo bila ya kujielewa,ya kuwa mazoezi yetu yamekuwa machache kulinganisha na uwezo wa miili yetu.

Ni jambo la ajabu, kwa  tumaini hili. Sina uhakika jinsi utamu ukawa ni sumu, na mara nyingi zaidi kuliko pale haionekani sababu nyingi kwa ajili yake, lakini kwa mchakato wa baadhi ya asili au isiyo ya kawaida kitatengeneza zisiozimika. Inachukua mda kwetu masikini  kwa njia ya  giza miaka kenda  na uchungu huu  ndiyo unatufanya kuishi, na si tu kuishi, lakini kufurahisha, kwa sababu inatupa furaha inayoonekana tulipo.


ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...