Tuesday, September 11, 2012

AGIZO LA NAFSI

Sitaki kuchekwa ya kuwa imekuwa nileo nkakosa usingizi,sitataka kuwa mwingine maana wa leo ameondoka akidai kurudi,sitaki ya jana maana yanakuwa na maksudi yake,hata ikiwa ivyo vilivyo ntaipigania na nikijua maana ya kutokujua  na maana ya kupatia ama kutokukosea,leo njoo hata na kesho nitakuita,hata akiwa mgeni basi nimwite mwenyeji ili mgeni asitetemeke,karibu sana mgeni na upumzike ya kuwa kesho ni leo yangu hata usingizi ukaupate.

Usipoangalia utakesha kwa kuwa maongezi ni mengi,usipotazama ukasinzia na kutouona  utofauti maana  na manguli ni wengi,ukasikia yaliyo ya ziada,ukaonyeshwa visivyofutika  haifai kuuliza kwanini,basi kile kilichofuta ni lazima kilikuwa na hitaji la lipizi,pengine ni agizo,umetazama kwa kuona yale yanayokaribiana,karibu sana mweusi maana wengine walishatangulia,walioitwa weupe wamejazwa na rangi ili kuchanganya ikaeleweke imerandana.

Karibu mgeni leo nimepika chakula kitamu kwa wale wasio kula pilau,na kesho ikija karibu tena niliyoyasikia jana sipendi kuyasikia na leo.usijezama kuwa tishio na kutikishika visivyo tishika,uzinguzi uje kwa mwanga maana leo imekuwa ni giza sana sijaona kama ya jana ama vilenipo pazuri likiwa fikra ya mmoja wapo pengine.

CHEMA..

Bado  naizungumzia nafsi yakuwa ni mahitaji kimsingi ikawa kama mtaji,yale ya leo nayarudia kuwa ya jana,maana ikiwa unachanganya lazima ujue ni dawa gani pengine ikawa ni ya maana,mimi nafanya leo iliyo  njema  yakuwa imetegemeka kuwa njema sana,kwa kweli tulipatia sana kwa kuwa na uwezo wa kufanya kile kilicho chema,hatuna haja ya sauti ya kuwa hata mtindo wa mlio umekuwa ni  tofauti,maana mashine  zitarudia mara mbili ikiwa zinataka kuhakiki namna ya vile biashara inavyofanyika.

Kweli tumevuta na yale yaliyo na utakiwa wa kuwa nyumbani maana haitakiwi kuogopa.leo tumetoa ipi ile iliyo ya kwanza ama ile ilyo ya kwanza,kinaweza hichi ni kicheko kwani ile lugha haijaeleweka imekuwa nini,ni kwa akili na uwezo ndivyo utanionavyo,katika rafiki na uwezo ikiwa hata mambo ya kale yakaja kuwa mapya yakuwa tumesikia kwamba imezama na imekuja na majanga ambayo  yataendelea kutokea,leo jichunge maana wangine hawana namna ya kushika yaani mshiko.

Ndotoni ukija basi jaribu kujiondoa akilini maana  uwoga unakuja na itikadi ambazo hazizoeleki,leo basi iwe yetu maana tumekusanyika katika mengi,kwani katika kuogopa pia ikawamo na kujali kwani mengi anapewa Yule anayeanza kwani tukitaka kutamani itakuwa ni kama vile ilvyo ile katika moja wapo,ya leo siyo hii kwani nimeona kwa waliopatia kwa kusahau yaliyotukia,Kilimanjaro ni kama maskini asiye na sababu kwa kuchoka maana ni ukubwa tu,ama ni faida kwa kuwa kuna kuzungumziwa

FIKIRI

Fikiri Leo umetumwa wakibaki peke yao,maana wakitaka kupata faida wazijuazo wenyewe,ikiwa unasikia ni lazima kutaka kuacha maana ukweli  umeonekana,ikiwa chini ni utata basi tujaribu kutafuta vya kupunguza maumivu maana kwa starehe tutapona ikiwa hata kama tutachelewa isionekane kwani mazuri mengi hutokea pindi pale mtu anapojidai yeye ni yale anayotaka na kusema yeye,maana kutokutaka ni namna ya kukosea,haina haja ya kumfunua aliyelala maana adhabu iliyo tamu ni maumivu yanayoifurahisha nafsi.

Usitukane kwa kupiga maana mwanzo  ukiwa mwisho ni furaha inayoleta karaha,iliyokuwepo tangia jana tusiifuate kesho maana hata tukatukana tutahitaji maana ili kuleta namna za kuelewa,usiseme wewe kwani kesho ndiyo zamu yangu,kile kilicho chako ni changu katika upendo usio kuwa na maana ya hitaji,nawapenda sana wageni maana wao niwahitaji wa mambo mengi sana.

Katika ukweli tumenyamaza maana pengine itajulikana ni uvumilivu uliopo katika kukubariana ili mradi ikaeleweka kama ndivyo vile ilivyo katika kuelewa ama ilivyo pangika kimfano maana hata matusi katika kutaja majina itaeleweka kuwa ndiyo naamna ya kuitika ili leo wakaja pembeni wakisema na wao walisikia wakiitwa kumbe majina yanafanana bila kujua.fikiri uliitwa wewe na majibu hukutoa eti ya kuwa hukusikia au pengine mwitaji alijibanza pindi akifikiria ndiyo.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...