Wednesday, July 18, 2012

POLENI WATANZANIA..


 
Poleni watanzania,wabishi na mimi nimo..!!maana kwa misiba mingi kufikia,pengine wengine wanasema mungu ametoa na mungu ametwaa vile tukafarijiane majumbani kwetu,muda huu huu wengine tumechelewa kufika eneo la tukio japo tukarusha kamba kuwaokoa wachache pengine ilitakiwa kutokuruhusu leo na kuwa kesho lakini ndiyo imetokea,haya ni majonzi yetu,hapa tunastahiki kushtuka,maana si kwa kutokuwa kawaida bali kuwa tumeuweka uongozi pembeni na kuweka ubinadamu,maana fikiri unaambiwa mtoto wako yupo humo,pengine je wewe ungekuwemo humo?haya ni kiimani zaidi,haya ni ya mungu.


Tusife moyo kwani japo tunarekebishana kidogo,tukumbuke hiace zote zimeacha kutembea mijini na sijui ni kwa sababu ya udogo,ajali ama foleni,pengine bahari imekuwa na mabonde,na madeleva wameshindwa kuendesha kwani walizoea tambarale,pengine ni wazi inahitaji kuvichunguza vyombo vyetu,maana ndiyo tulivyonavyo na kama watu ni wengi inapaswa kuwabeba ikiwa watu hao wanashughuri za kimaendeleo pande ya pili

Zanzibar ni kwetu ndiyo maana tuliungana,kama ingekuwepo sasa ni mimi na wewe,katika muungano kuna mengi humo,mwisho tunapata undugu,kutoka dare s salaam mpaka Zanzibar sio mbali kwa ndege lakini tumezoea meli,na boti huu ni usafiri unaotukidhi na maisha yetu,hivyo tunahaki ya kuwa makini na vyombo tulivyonavyo,ikiwa kama vinataka kuzeeka basi tunavifanya virudi katika ujana kwa maana kikizeeka sana hatuna budi kununua vipya,poleni sana ndugu zangu,poleni sana watanzania wenzangu..
Mungu alaze roho za marehemu pema..!!

HALI BADO NGUMU..


Maana bado inaendelea,hali kuwa ngumu.ikiwa kwa mara ya kwanza tulipoambiwa tukajifanya tumeelewa tena sasa tunaambiwa turudie tunashindwa kuelewa.tumekuwa bidhaa sasa mpaka tukashindwa kuzuia upepo,tunapelekwapelekwa tu,hatuna misimamo zaidi ya kugombania vyama,tunapumbazwa na sifa badala ya maisha yanayotuhusu,maana tunataka haki pasipokujua haki tunapata wapi zaidi na badaye ije tumlaumu mtu,eti aahh Yule hakuwa kiongozi bora,sasa tunataka nini,maisha bora,kiongozi bora,chama bora au wewe bora?hata nisifahamu maana kila mtu ana kujifahamu mwenyewe.

Kesho tuangalie tusije gombana,maana hivi tunavyoenda bila ya kuelewa hiyo inaashiria jambo bovu,maana tutaenda kinyume na maana ya mwongozo,hata kama ni mbovu.nzima ipi?hata hivyo hakutunga yeye..hamkujua ya kaisari anapaswa apewe nani?,sijui hata tutajengaje maana kila mtu atataka kuujenga mnara wake,ili uwe wake ndiyo ndiyo hapo tutatofautisha ujuzi na pesa,mwenye nguvu atajenga tu,kwani we hujui namna ya kufyatua tofali?haina maana ya kuitwa mtanzania kama ni mchina.

Haina maana kumkataza mgeni asiingie na wakati ni kwake,maana ameshanunua sasa tunataka kuwalipa mara mia au?mkubwa akielewa amekosa sio kumchapa mkubwa mwenzake,leo tunaondoka bila taarifa,samahani hivi bunge la nyumbani litaongozwa na nani?kama mama na baba wote wamechukia,na familia zenyewe zilivyo za kihindi kila mtu anataka aonyeshe hasira zake,rudini bungeni jamani..swala la kukaa chini na kuangalia ni nini kifanyike,maana tutagombea viti huku watu wanaendelea kuteseka,maana sijui mtueleze mnang’ang’ania nini na wakati mnashindwa kusaidia watu walio katika msaada,hapa mahala hapata kuwa sawa, hali bado inaashiria  vigumu.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...