Wednesday, April 4, 2012

Tutatukuza majina yetu tukasahau ya baba zetu..!!!


Hata majina yanaonyesha unaelekea mbele,bora kusahau kuliko kukumbuka wachache wanayotaka yasahaulike,sina maana ya kuujua muda kabla.tena hata kufuata ushindwe maana hutajua,imefika muda sasa bado unajaribu tu,ujuzi wamebaki nao wanaoweza,jua hivyo kwa kile ambacho unakijua wewe.ikiwa ngumu sana yahitaji kufikiria kwani unaweza kukosa wakujibu,watakimbia wengi sana kwani hata mwalimu ukimuuliza anachokisoma hakika huwa kama mwanafunzi ,pengine labda kama hauelewi.
Hapa maisha yamekuwa matamu,na muda mwigine mkojo  ugeuke maji,hii ikiwa sio tu ya kutaka kupingana na maulana ,kwani mbona hata maji hufanya vile wezekavyo,nikiwa namaana,yanawezekana tu,ni kama pale njaa endapo haitazidi zaidi ya kuja maana iliyopo haijawa vile zaidi yawengine walivyofikiria .Waliowahi kufanya pengine hutamani tena,kama inarudiwa basi ni tamu,
na kama itazoeleka na kuwa tabia kabisa basi hiyo itakuwa kwenye damu,hapo hakatazwi mtu kufanya lake na asidhani ya kuwa amekatazwa basi ni wivu,
vile itakavyo kuwa katika mmoja akaichukulie mfano na kwa mwengine ikiwa tu kuna kuamini au ipo na imeeleweka hivyo mengine yakaja kama kushindwa,ni matokeo pia.

maana kuna wengine hushindwa kweli na kutokujua kama wameshindwa,wa kwanza anaweza kuwa wa mwisho na wa mwisho akafuatia kuwa wa pili,
hii ikiwa ni kuna yale ya kukataa na kukubari,
sasa katika chaguzi kila mtu naye akatakiwe kuwahi katika namna yake,maana hata ukaweka muda haitaleta maana kwa wale wanaowai sana,achana na hapa maana muda nimeuzungumzia kitambo sana

Pengine haina haja ya kusema kuwa Fulani kasema kwani wamesema wengi na hata  Fulani alisikia kwa Fulani,mabaya yenye utambuzi hayapaswi kumkataza mtu zaidi ya kumwelekeza,ikiwa unakata kulia na ukawasha indicator ya kuelekea kushoto hapo lazima tufanye maajabu kutokea..kumbe maajabu yapo hapa hapa,hata haina haja ya kuwashaangaza wale wanoshangaa maana washangazaji hawajielewi kama ni kuchekwa au ni sifa zimelengea wapi.

Kipindi cha kudanganyana sio cha leo,
kesho inakuja na kwa namna tulivyojipanga kwa mazoezi hakika hadanganywi mtu,maana ilivyokuja leo ni wazi ilikuwa haifahamiki kwani kilikuwa kinasomeka kitu kingine,kumbe chazamani kinaweza kuwa kipya,hapa hata bila imani unashinda,
unapoamua kushindwa utahesabika pale ulipotaka kushinda na ukashindwa kweli,maana sio tu umeshindwa kwa kujiandaa kushindwa,
useme utajua mwenyewe maana yakupigania yapo mengi hata usiyape idadi  yakuwa yaliyoanza haukuyahesabu.

Embu acha ya kikubwa yakawa hivyo  maana walifanya mababa zetu hayo

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...