Tuesday, May 29, 2012

A BUTYFULL SLAVE..

 A slave is a slave to him or her self. 
To work out...
is you to move,
 and the word ‘move’ fills an action, that’s moving…
as when we will be together
   ’we will be moving’,
  it also  consider a heart when I talk about it. a heart that knows, 
does not mean to know wrong,
 but to know what you suppose to know.
 I came to realize this time we start to look for our self as maybe as we are moving while not watching our back, 
it’s not what you leave behind..
It’s nothing out there,
 when you look in this two eyes, 
it needs to start moving for a third one; either you see...
 you cannot try to remember. 
I SAY we
 TOGETHER.
He says......
For God ways I accept, 
I praise,
 He WHO raised me up with thy soul faith!!

UZOEFU HAUULIZWI.


Wale wazuri wamefanya yao,tena ni mengi na mpaka yakawa mazuri bora,pengine walitumia ujuzi wao na katika maisha kitu ujuzi sio kitu kusikia,sio kitu kusema wala kufanya katika wakati wowote wa muhitaji yaani ni mtu kuelewa kujua na kuthamini kinachoendelea kutokana na muda,haina haja ya kutafuta ujuzi ikiwa kazi unayo,kuishi ni kufanya kazi ama shughuri ambapo unatoka ujuzi,sasa ukifikiri unaishije ndiyo utajua ujuzi ni nini maana unatakiwa kutoka mahala Fulani unapopaona,kuishi vigumu sio taabu ni kupenda ni kama huwezi kuoa ikiwa unaishi vigumu,na kama una uthibitisho wa ugumu ulionao hapo itakuwa haukupata mafundisho yangeyokuzoesha kufanya hata usichokipenda.

Kusudi halina sababu ya kwanini ilete maana yenyewe,ingawa hatuwezi kufanya kitu bila kusudi,kusudi sio sababu ama mazoea kusudi ikiwa ni dhumuni,na hata tusifanye mambo ya sababu maana tumejawa na sababu nyingi sana katika kila tukifanyacho,lakini kusudi huwa linatimiza nia,ni kueleweka kwa kutimiza dhumuni lililotokana na uzoefu,kujua tena ni  kuijua sababu iliyokosewa mwanzo,sasa ikiwa ni kwa sababu ipi ndiyo pale tutauliza dhumuni la kila mmoja ili tuonyweshe uzoefu.

Kuna uzoefu mwingine haufai kuuzoea,hasa ule ambao hauupendi wewe mwenywe kwani ndiyo utakuwa ni uzoefu wako baadaye unapoendelea,utakuwa umezoea hivyo kama ni kupenda au kutokupenda,pengine unataka uzoeane,uwe na umoja uijenge nchi pamoja maana hata ukibisha wazoefu watazitafuta sababu na kufanya yao bila ya kuuliza,umezoea kufanya nini hata ujiulize basi na kama umezoea hivyo na haujaambiwa ni vizuri basi usubiri majibu,ulimwengu hutoa ushindi,Ushindi wako upo mikononi Mwako uko mahala pale Umezoa.

NIA NA THABITI YAKO MWENYEWE


Pengine usije ukaenda mahala bila kujua hii ikiwa kuna kuagizwa ama kwenda,na ikiwa umeenda ni lazima ujielewe kwa namna ya kusema unaenda,maana hata ukaendelea na safari yako itaonekana si maana kwa wale wengine,na ijulikane kuna ulazima wa kuwazungumzia na wengine ya kuwa kuna uhitaji wa kuwa pamoja,nia ya umoja hujenga thabiti yake,hujenga yale yaliyo yake,hujenga lile lililo na thubutu

unapothubutu kufanya jambo  si kuwa na akili Fulani,si kupima uwezo Fulani,na ingali kuwa hivyo hata usishindane,na iwapo dawa ya Yule mbishi ni kutaka kuona kama imejulikana vipi,hapa akiwamo au hata asipokuwapo ueleweka wake unamfanya awe hivyo kwani muda tukiungalia huwaisha yale yaliyokuwa na thubutu la kweli,mateso na pilika za maisha zinafanya kutokusikia kwamba pengine fulani alisema nini,pale tunaposema pombe ni mbaya tunathubutu na tunaona,tunaposema simba ni mkali hata kwa picha anajionyesha na thubutu yake ni endapo anakutana na mwanadamu,hapa katika simba ni sawa na katika maisha,maisha yanaralua kisiri ya kutokusema kwamba nimeralua pale,hii ikiwa imerudiwa,nia na thabiti ya mtu haitakiwi kurudiwa zaidi ya kufanya,kufanya na kueleweka kama ilivyo,Ikitokea basi ifanyike katika uthabiti wake.

Pengine unataka kueleweka tofauti,pengine unataka kujulikana tofauti,nia na thabiti yako ikatuthibitishie,ule uthabiti unapothibitika ndiyo huonyesha asili ya tendo,maana itakuwa imetendeka kwa nia isiyojalikana kama ni njema ama la,hiyo tukaiacha kwa mtendaji kutokana na akili zake,unapokuwa majumbani na kukuta unatukanwa na mkubwa wako sio jambo la kusema nani kamfundisha mwenzake,maana hata matendo mengine yanaingia bila kueleweka ndani ya eneo husika na yakitaka kuonyesha ni matatizo.

Hasara ya utambuzi si kama ile apatayo mfanya biashara maana hapa hata nia ziko tofauti,wala kutambua inakuwa ni vigumu,hata kama akili ya mwanzo ni kufika katika mlengo Fulani,lakini nia ya mtu itaonekana na thabiti yake,tena usichelewe ukaseme ni bahati mbaya,kwani utakuwa umenuia huko,na baadaye kuja kusema kwani hakuona!!mengine yasipase kumwachia mungu,mengine ni yako hata haina haja kuyaweka chini ya uvungu,utaficha yaliyo na maana,utaficha visivyo na uelewa,hapa hutaelewa na hutamaanika,ukifanya leo nia yako iwe mbele,ufanye leo kwa kutokuogopa yanayotokea,kwa kuthibitisha unayafikia  na utafika.


NGUVU ZAKO..



Endapo tulizaliwa wanadamu kunakuwa na urahisi Fulani wa kuweza kuelewana,hapa hata ule uwezo wa kuelewa zikajulikana kama ni nguvu,tusijali zilizopotea kwani zinazokuja ndiyo tunazoziombea,maisha ya mwanadamu sio ya kulalamika zaidi ya furaha,pale tulipoambiwa tajiri kwa tundu la sindano na ngamia sio pale tulipotupia nguvu zetu,yaweza kuwa ni hapo lakini utambuzi usio kuwa na uwezo unaweza kufanya yale mengine kuwa mengine,hapo watu wakiwa wamechoka,hawataki yale magumu na kutaka mepesi,wakiamini kuweza kwa hali ya kawaida wakiamini kuweza kwa kusema ilikuwa rahisi bila ya kutumia nguvu zako,kile kinachoisha kimetumika,yanapokuwapo maneno ni lazima tuseme,

Yanapokuwapo maumbo ni lazima tuyaunganishe,maaana kutimilika kuwa moja si sawa na nusu inayoelea,hapa tukiunganisha nguvu zetu ingawa sio lazima zangu na zako ama za Yule bali zako,zangu na mwengine yeyote,haujafika wakati wa kulalama wakati bado hakuna wa kumlalamikia,maana kama ni kwa mungu huku ndiko tunapoelekea,tunapompa lawama Yule aliyezoea tutaweza kuonekana wajinga wenyewe maana hapo tunahaki ya kuulizana kwani nguvu nyingine ziko wapi?ama hatuna na kama ni hiyo ieleweke hata kwa kusema,isemeke ikiwa inahitaji msaada maana inaupungufu wa nguvu

Pumziko la mtu anayetafuta ni nguvu kwa mmoja aliyelala,hapa tusilale,hapa hakuna kulala maana wakati ndiyo huu,muda wakuupoteza ulipita na kubaki wa kutumia nguvu,tumelishwa sana na wakubwa zetu wakiwa wazazi pamoja na ndugu baki hiyo yote ikiwa ni kutaka kuonyesha nguvu,,hakika misemo ipo lakini si kwa mwanadamu ikaonekana kwamba hapa au pale alishindwa nguvu,kwani maana ya hakifai ni kile kilichoachwa jana,hakikufahamika kama kipo ama kilifahamika na nguvu hazikuwepo,

Tusiwakaribishe wale wengine wasio na uwezo wa kufikiri,wao nguvu zao hutumia kwa utofauti na wenye akili,wao nguvu zao hutumia ipasavyo ya kuwa ni tofauti na sisi,wa kuchekwa hakuna maana wote hatujafanya,wote bado hatujatumia nguvu zetu,kama tumetumia embu tuambiane ni mahara gani,yaweza kuwa zilitumika bure na umekuja wakati ni ieleweke sasa,kipindi cha kupita hakifai kupita tena,kipindi kinachokuja ndiyo kile tunachokisubiri,Yule anayeandaa nguvu kwa ajili ya jana hataki la leo,ingawaje na lenyewe lilibaki tokea jana hiyo,ni kama mpiga picha hutumia nguvu zake ili apate kula,hutembea pengine asipokuwa na ofisi na hiyo ni kudhihirisha maana ya nguvu,akirudi aseme amechoka na mwingine akaulize kwa nini maana yaweza kuwa alitumia nguvu ndogo katika kufikiri iliyompelekea kutumia nguvu kubwa katika kutembea,labda tuandae mazingira kwanza,tuyainue,tujiinue.

Onyesha nguvu zako tokea moyoni,onyesha kwa kile ukifanyacho tangia usoni..!!










AMANI


Maana pengine tukaelewe kama ni imani,ikiwa ni kwa ufahamu wa mtu,pengine tukahisiane vibaya,hapo tukiwa hatujajuana,matukio mengine ni  mambo,matukio  mengine ni maswala ya kawaida,pengine sisi ni wa kina nani,pengine haina maana  ya kuwa na imani wakti wewe si mtu wa amani,amani huja pale mwenzake asimfikilie Yule mwizi,pengine mlevi hii ikiwa mmoja amejiweka mungu sasa,au hata kuonekana.sasa kama ikaja na mwignine  akawa mungu si itakuwa balaa,maana hapa wasomaji watakoma,lakini ni amani inayofanya tuwe na imani,imani yangu imeniweka ,tutavutana kwingi sana,hii ikiwa ni kutaka kueleweshana,na hapa ikiwa tutafikiria pesa basi vyote anaweza akapewa mwingine,maana kama ulikuwa na amani ikakuletea imani na imani yako ndiyo hiyo uliyonayo sasa hivi basi mshukuru mungu wako,maana amekuweka huru na Baraka mpaka sasa.

Mimi ningekuwepo zamani ningewaambia kitu,lakini kuna hichi cha sasa hichi ambacho wote tunakiona,tusifanye ije baadaye watuhadhithie,ya kwamba kama hatukuwepo vile,yaani tukatafuta bila misingi,hata tusione wala kujua nini maana ya jambo Fulani,pengine watu wengine wanacheka wakiwa hata na hasira,hii sikatai kwani mimi sio wote,ukiwa wa kuwa mmoja haujengi ukimya wa maana ya maisha ya mwanadamu,hapa tunazungumzia ukiwa zaidi,tumepoteza vingi na kila mmoja anakikumbuka chake,cha mwenzako kizuri ni kile cha mwingine kimebaki kidogo,maana hata tusingepishana tusingejua mengine,mengine kuyafahamu yakupasa kuwa na imani yenye kuleta amani,tusifanye vita kwa kujua tunakwenda mbinguni,kwani tunapoenda kwa watu bila taarifa tunajua kama wamepika chakula gani?hapa lazima tuwe na mazoea,lakini mazoea haya kuna yale ya utofauti,pengine ni mazuri tuseme.kama mkubwa anapokuwa na kwake anakuwa na amani sana,hili nimesema mimi,kwa  Yule asiye na amani basi hata akizaa mtoto ataamini ni wa Fulani,maani ile imekuja katika imani,yaani yeye akaamini hivyo

Amani ya moyo ni nzuri,hivyo ni kwa sababu ninayo,chako jipe,kama vile ilivyo katika imani,ninaamini kupitia amani hakuna kitakachonishinda mimi,hapa ukibisha basi utakuwa unahitaji kuelekezwa,mengi tu mazuri lakini lingine sio zaidi ya lenza.itafika kipindi tutaanza kutangaza makanisa katika vyombo vya habari,hapa imani itakuwa zaidi na amani itapotea,pengine lile kanisa fulani  la pale chini ni la jamaa Fulani hatumjui alafu haya mengine yakwetu,si ushindani na tunataka!!lazzima vita ije,pale tukiwa tunaamini huyu ni adui yetu lakini ingawa ni mwanadamu mwenzangu.hapa tutapoteza vingi hata vile tulivyovipenda kuliko binadamu wenzetu,amani ikipotea hakuna kinachoeleweka,maana lengo zuri la kuelewa kitu ni kuishi na hicho kitu,hakuna kuishi katika vita kwa ni tokeo lake kuu ni kifo,tulete amani sasa,kama ni nyeupe na inasema sasa si tukae chini na kuelezana,mambo ya msingi yapo mengi tu,hatuwezi kuyafanya bila amani maishani.

AMANI MWONGOZO WA IMANI MAISHANI..

AKILI YAKO


Pengine unatenda tofauti,pengine hautumii akili Yako wenyewe,pengine unatumwa bila kufikiri,akili sio kufikiri tu,akili sio uwezo akili sio namna ya mmoja akaelewa ya mwengine akili ni namna ya wewe ulivyo,kinachojulisha matendo yako,fikra zako na kile hasa kinachoonekana kwako maana unaweza usitende na ikaona ni akili yako,labda wametenda wengine,labda ilibidi ufanye wewe,lakini bado ikaonekana sio wewe yaani hata kama imefanyika basi uwezo ukawa ni mdogo au umekimbilia upande mwingine maana unautafuta sasa na bila kuonekana,yale yaliyoonekana yamekuwa machache,hayajaweza kutimiza maana,ikiwa inayotakiwa si ile tu wanayoitaka wengine,ni ile ukasema wewe sasa,katika kushangilia tunajumuisha akili,hapa nazungumza  na watendaji

Pengine utende wema na kwenda zako,pengine utende mazuri na kwenda zako,hakuna kuomba yasiyo na uzuri kwani mabaya yapo mengi,tutarudi nyuma kuelezana uzuri lakini ile kweli ya akili ipo ndani ya wewe,yaani mtu ndiyo maana ya kupewa uwezo.akili humfanya mtu,akiwa na umbile si vitisho kwa wenye akili maana wao hutenda yao,ni kama pale katika kusoma,ni kama pale katika kuelewa,wachache wakapewa uwezo wa kusoma,wachache wakapewa uwezo wa kufikiri,wachache wakafanye maana wao walikuwa hawajui namna,tena kwa hapa sio ya kwamba ilitokea,bali ni kwa akili zinazokuwa thabiti zinazoweza kufikirika,ni akili zako zinakutambulisha

Yaliyopo yote umeyakuta,yanayokuja yote ni akili,ni ya ufafanuzi hata wazazi wetu wakatutegemee kwa baadaye,maana kwa wengine wasio kuwa na kujua si kwamba hawana akili,hawafikirii zaidi ya kufikiri vile ilivyofikirika,hapa nikiiwa na lengo la mwanzo lakini sio kurudisha akili mwanzo,usikae chini kupoteza muda maana na akili zinakuwa,unashindwa kwa akili kupitiliza uwezo wake,ama uwezo wenyewe kupita mahala pale akili ilipofikiria,hapa huwa nachanganyikiwa,hapa huwa nakuwa na mambo mengi,pale akili inapolindwa na kuendeleza hufanya hivyo,maana imekuja kuwa kubwa kutokana na kujazwa,kama vile ilivyo kwa ujazo usio kuwa na chombo labda na kwa wenye akili za kiupande Fulani kuona katika namna Fulani hiyo hiyo,

Akili haimbadilishi mtu,akili haimwendeshi mtu,labda mtu anaendesha akili yake,tukisema matairi yanaendeshwa na gari hapo utautafuta mwanzo kwa vyema,maana isije kuwa yalipaswa kutembea pekeyake japo ukaongezeka,wamekufa ndugu wengi sana kwa ajali zisizokuwa na uendeshwa na akili,unaweza kupata ajali za kimaisha kiujumla,ukiumia kwa mateso ya viungo na mwili,ukiumizwa na maisha na dunia kiujumla,akili zako ndiyo mwongozo na kipimo kikuu cha imani,pale inapofika imani imekuwa si lazima akili kukua,yaweza kuwa akili imekuwa tofauti ilivyo na imani ya mtu mwenyewe,nikiwa sizungumzii imani basi husisha hata akili,maana hata akafika mwislamu asimwelewe mkristo ,ni akili yako tu


Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...