Monday, October 8, 2012

PESA..


Nikisema iilkuwa wakati wa matumizi nitadanganya umma,ila kama sikuweza kusikia basi kushuhudia baadhi ya matukio ya kipindi icho,vijana wa kisasa wanasema wanakumbuka enzi zao,enzi ni nyuma na ujenzi,maana inawezekana enzi zikawa ni nzuri kuliko ujenzi,unaweza kujenga kile usichikitegemea na bila kujua utachanganyikiwa kwa kuporomoka hadi kujikuta huna maana kabisa..kile kinachopoteza hata thamani ya kukopeshwa hicho kitabaki na maana pekee,pengine ikiwa wanaotumia hawana maana pia,bora kuwa hauna maana kuliko kufanyishwa hauna maana.

Wengine watasema naleta vita kwani wao wameshazoea kama miaka ile ya 75,unajua ili kubadilisha namna ya kukaa ni kumweka adui pembeni,dawa ya adui hakuna asiyeijua kama siyo aibu za kuoneana rangi,ikiwa moja imependeza na nyingine imeiva,zote nzuri tuangalie wasije badilisha mpaka zikawa sita maana kila kijiji itabidi kitumie pesa zake,tena  karatasi za kuingilia na kutoka’ zikae sawa maana mda si mrefu adui anaiporomosha thamani.

Nimebaki na maswali mawili matatu yanayonishusha thamani,pengine kujumlisha ni kutoa,maana ikiwa kukuwa kwa mgomba ni kukomaa lazima tuangalie na virutubisho,unaweza kukua mwili tu..leo ukajibadilisha rangi hii,kesho ukaona upendeze na nani na fulani…yote yako hayo,kama unazo zaidi ya moja zenye thamani moja mpe hata wa jirani ya mbali ya nchi nyingine pengine zinaweza kupanda thamani zikiwa huko maana nabii hasifiki kwao.

USWAHILINI KUNA VITUKO


Nashangaa sana kuona watu wakiangaika na katiba ikifika muda wa kenda miaka sasa,nashindwa kuelewa nilichosomea ni nini maana ni wazi siwezi kuandika katiba,hapa lazima nikuulize kijana mwenzangu ikiwa ni utani kwa mzee akimwambia kijana mwenzangu..sikuweza kufikiri wala kujua endapo piki piki hizi za wachina zinavyotenegenezwa kwa wingi na kuingia kama karanga,ushuru bure kama unapeleka kule,leo ije waseme hakuna spea,hizo zikiaribika ndiyo mwisho wa safari yake ya maisha,wakisahau jamani hizi pikipiki ndiyo zinazotuendesha,wakisahau yaliyo katika katiba ndiyo yanayotuendesha,tena siyo kibinafsi.
.
Tumezoea kuendesha bila kujua kama tunaendeshwa,kama swala ni kukubariana basi liwekeni kwa wananchi watamtafuta aliyeitunga ya kwanza,maana nashangaa kila siku kubishana,yaani kama ulikuwa unaishia vizuri,sasa unang’ang’ania kuishi vibaya,wewe kijana angalia usije kufa umri si wako,wazee mnayafahamu haya ila hampaswi kuitwa wapumbavu.usitegemee kufa kwani ni bahati mbaya,kama unauwezo amka kesho nenda kajikwae  barabarani,na wala siyo lazima iwe kwa  wote,

Nina imani ya kuwa na wengi walio soma na wasijue wamesoma nini,hili ni kosa la kutokuambiwa kama ubongo hautanuliwi na ulimi,ni namna ya kuuweka makini,ili kesho-kesho kutwa isije ikaja usiamini.unawezashindwa kuelewa ni kwanini yale maneno yamekutazamia wewe,maana hata kama ni mimi lakini ni namna unavyoichukulia wewe,huu ni uswahili na haina kustaajabu yaliyo na vituko uswahilini.

UANADAMU UTATA..

Naomba samahani kwanza kwani kwa hili tendo nilijua kwanza,kama hujui kwanini unaishi,ulipo  na ulivyo utakuwa ni mpumbavu anayepaswa kuishi na wapumbavu,maana inaweza kuwa ni wa milele,kama hujui upo duniani kwa ajili ya nini? embu jiulize sasa,kaa chini fikiria na muulize hata mwenzako,ndiyo inawezekana kufanya kile ambacho hakipo katika mategemeo yako lakini ikawa kipo katika njia ya kuendea kwako,fikiri mara ya tatu na kujilaumu kwa kufanya na kuona umekosea,

Namna ya matendo na jinsi ulivyo ndiyo yanafanya maisha yako,kumbuka kipindi unapewa mitihani kama ulikuwa unafanyiwa na mwenzako,maana sasa shida ndiyo mitihani yako,jirani yako ndiyo Yule aliyekuwa akikusaidia hata kwa chumvi inapokata mida ya giza’.pengine wengine hawaelewi kwa kuwa na kuishi kivingine,kama sijakosea mwanadamu lazima aishi maisha yake halisia,hasa pale anapokuwa mtu mzima,watoto huwa wanachukulika hawana makosa kwa kuwa kwao wao ni vigeni,hata hawapaswi kukaa sebureni.

Mwanadamu anastahiri upendo,mwanadamu anastahiri namna ya kujiona mtu katika dunia,maana umekuja kwa ajili hiyo,unapoambiwa mbaya shukuru mungu maana wazuri mungu kawanyima ubaya,kubari kuwa yangu ni kama yako,na kama huja baada ya kuona muda unaobidi kutumika ni ule ule lakini kinachobidi kutendwa kimetofautiana,mwanadamu tafuta ridhki yako ujione mfalme,ukiona mwenzako anamsema mwenzako angalia isije kuwa ni kawaida yako,fanya mambo yako…

JIULIZE...


Unaposhindwa kabisa ama kuweza pia ni kheri ukajiuliza,jiulize kama ni kweli unahitaji mafanikio ambayo yatakukidhi,ukiwa na akili timamu,ukiwa na akili zako unazozifahamu,isieleweke kuzingulika kwani mwisho wa siku utajizingua mwenyewe,usiwe na haraka ya vitu usivyovifahamu,usiwe na  haja ya kutaka pasipo kufahamu,ikiwa kwako jiulize kama ipo kama kwangu,yako ni yako lakini ni katika usawa wa matendo,wacha niseme hivi ilivyo ikiwa katika kuelewa.

Angalia usije ukapotea maana na njia zimekuwa ni nyingi sana,anafatia na maswali ya kujiuliza unaweza kwama na kuoneka ulitungwa hadi  swali sijui jibu atakuwa nalo nani..kwani ingelikuwa ni kiulizo basi ni lazima ungenijibu wewe,mara nyingine gadhabu hutumika kwa kuona maswali magumu yakikusonga,mara nyingine maswali huwa marahisi ikawa unayefanya magumu jiulize mepesi yapi?maana swali la mtihani jepesi si ya kuwa umelipatia maksi..

Nilijiuliza nikasema sina haja ya kuuongelea mtihani labda iwe katika chumba chake,nikajiuliza yajana niliyoyaweza leo kumbe ni  mepesi,ndiyo maana nikawa najiuliza sana kuhusiana na siku ya kesho.utu uzima unamajina zaidi ya pesa ilivyo,maana mwanadamu haendani na fashion ingawa anaitengeneza mwenyewe,jiulize  kama shavu lako la kushoto liko sawa na la kulia,ili utakapopigwa hata la kulia ukageuzia na kushoto.

MAFUNZO

Hakuna matatizo yanayokuja na kusemwa yameshindwa kutatuliwa,matatizo yangu siyo ya kwako hata kama tumefunzwa pamoja hatuwezi kulinganishwa kwa hilo maana ya kujifunza ni kudhalau yaliyopita ya kwanza maana yangu,usimdharau mwenzio kwa kuwa wewe umepata unachojivunia maisha,maisha ni mzunguko leo ukiwa nacho na kesho unaweza usiwenacho ni maana ya kesho kutwa kuja ili kujifunza maisha hayamfundishi mtu mtu anajifunza kutokana na kile asichokuwa na ufahamu nacho,yale yanayotokea ndiyo yanamfundisha mtu tena ikiwa yamefanya hayo kueleweka ni maisha yako.

Mwanadamu hajui lolote ndiyo maana asijue nini kuabudu,wanadamu ni wengi na Mungu ni mmoja Kubali makosa pale ulipokosea,na kama unajua unajitambua kubali makosa yako hapo ulipo,ukikubari na utajua hata kama unajua basi utajua mengine siyo yale unayoyafahamu,mtu kujua ni kama ladha ya utamu,maana kila mtu aujuavyo utamu wake hasa pale unapozidi na kupunguz.

Haki iliyo ya mtu siyo ya kila mtu,pengine ieleweke mtu Yule asiyejua na kuonekana anajua ndiyo ataweza kujua,maana ametaka kujifunza ikiwa kuonekana siyo kujua.mengine mengi hutokea mafunzoni na huwa ni sehemu ya maisha,hapa wachache wakiona kana kwamba waliishi sehemu nyingine na nyingine iliyobaki.mafunzo si lazima ujifunze popote pale,unaweza kwenda kufundisha walimu na ukawa bado ni mwanafunzi.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...