Tuesday, September 27, 2016

YAFANYE MAPITO KUWA ELIMU.

Yafanye mapito yako kuwa nguvu inayokusukuma kwenda mbele ukitegemea kuishi ndoto zako na sio kile unachokiogopa na kuhofia,wengi hawafanyiyale wanayoyategemea zaidi ya kile kilichopo pasipo kufikiri ni kwanini mtu anajawa na msongo wa mawazo yanayokataza kuishi ndoto zako.

Labda  kwa sababu ya watu na matendo yaliyopita yanaisumbua roho yako, watu wengi wanaishi wakikimbilia wasichokijua kwa kuogopa nafsi zao kubaki nyuma na baada ya kuangalia wanajikuta walichokifanya kilipaswa kufikirika kabla ya maamuzi ya kutenda, hivyo kukuletea shida katika kufanikisha mambo  pasipo kujua wapi walianza.

Wengine wanaishi maisha yao kwa kujiona, kujiona kwamba ndiye yeye,ukijiona kwamba u tajiri na wakati bado ukihitaji msaada na kuuacha uhalisia, kwamba kila kitu kipo sawa katika malengo na yale unayoyahitaji huku unasahau maisha yanakutegemea wewe, kwa lolote unalolitafuta na lenyewe linakutafuta, ni kama nguvu ya mvutano.

Hivyo ni lazima kuwa nalo jambo, acha kufanya lile lisilo na tamanio kwako na fanya kile unachoweza maana na chenyewe kitafanana nawe, ukitembea sana katika maisha utakutana na kauli ambazo nyingine zinasimamisha na kurudisha nyuma nafsi yako, ikiwa lakini yako utaitumia vizuri ukiangalia ni wapi utawekeza akili yako  na baadaye uyaache maamuzi yako yakikufata sambamba nawe.

Angalia katika njia ambayo unaweza kuyatengeza maisha yako yakawa vile utakavyo kama vile ukaamini kwamba ipo siku maisha yako yatakaa na kubadilika ukiamini unaweza kuyafanya maisha yako katika yale utakayo yakakurudia ama kukupata upya, kama hauna kitu nyanyuka na ukafuate kile unachokitaka.

Hutapoteza kile unachokitaka kipo na kinakusubiri wewe kama bado ulikuwa haujakipata,achana na mawazo ya kilichopotea maana unapoelekea ni mbele kupata maana amua sasa ili watu wengine waje wasome kupitia wewe.wengine wanasema hapana huku wakiwa hawajui kama wanakataa juu ya nini.

Nguvu iliyopo ndani yako ni kubwa,jiamini na safiri na nyota yako.

 

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...