Wednesday, June 13, 2012

INABIDI TU..!!

Umekuawa wakati mzuri maana kilichotakiwa kimepatikana,katika kuona yale yasiyooonekana ikabaki muda na watu kudanganya,maana kwa kuzunguka hapa na pale bila ya kusema,ikiwa haikutakiwa kusemeka,hapa zitakuwa lawama,hapa tutaonana wabaya,ikiwa kitakuwapo ya nini  ishindwe kuwepo?hapa napenda kusema kugundua hapa napenda kuhema bila kuumbua.

Unaweza kulenga mahara na kuona hapaonekani,hiyo ikiwa si ya kwamba hakuna mwanga,ama vile ilivyo kwa wale wanga,maana imekuwa kutembea katika namna yao wakati wa jua ikiwa ni mwanga upo hapo huleta kutokuamua,katika kujifunza kukataa ni vyema kuanza na kuogopa,maana kama utajifunza kukataa kuogopa basi hatimaye utapata furaha,hapo ikiwa ni kufanya mazoezi kufurahi.si ni utofauti?

Labda kwa hili la sasa tuelewane,ikiwa limetokea sio  muda wa sasa na lakini halikuweza kushangaza,maana katika kujua imani ni lazima kujua kukataa,tena sio kwa sababu ndiyo ni kawaida lakini kuna uwezekano wa hapana,maana napo jibu lipo,hapo nikiwa namaana ya mtu au watu kuelewa,kama vile tulivyoelewa mwanzo,pengine ningelikuwa peke yangu hata nisingeshinda,hapa tufikiri wote maana yanatakiwa mazuri na mabaya ili kujifunza.

Tusifuate historia japo na nafasi kidogo na ya kwako!!

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...