Friday, August 3, 2012

MALENGO NA MAONO.


Katika maisha unapaswa kuwa na malengo na maono,
malengo ni kujua namna gani mwanadamu unaweza kuishi,ikiwa tofauti na maono ni namna gani unaweza kuyakamilisha yale yaliyo katika namna gani unavyoweza kuishi,pengine ikiwa ni kwa nafsi moja tu ama ikawe katika ukuaji wa pamoja na ikiwa kiimani,akili na nguvu kiujumla,hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kumfanyia mwingine,labda sio maisha,pengine itakuja wakati na kusema hapa sikufanya na pale ilifanyika maana malengo yakiwa ni mengi kuliko maono.

Una muda na nafasi ya kuweza kutambua mahali ulipo zaidi ya duniani,
maana kama ni lengo basi lilifikirika,na likaonekana tena kwa mbali ndiyo huwa nzuri zaidi maana ya kufanyika kiuhakika,unaiona vyema,unajiandaa,pengine ikifahamika kabisa kwamba maisha mengine hapaswi kuishi mwanadamu umdhaniaye,pengine ukawa unaishi maisha ya watu wengine na hiyo ikiwa ni tofauti na malengo,na utofauti uaja zaidi baada ya kuonekana,ikiwa maono ni mazuri.

Unaweza kuona sana na usifanye lolote,na hivyo inapaswa kuwa na namna nyingine za kuyasukuma malengo na maono hayo kwani ukaongeza namna ya unavyofikiria ama ukafikiria hivi na sio vile ilivyofikirika,hapo binafsi kila mtu akafikiria lake maana haina ulazima sana wa upamoja endapo mmoja ametaka kufikiria lake pekee.pengine utaungana kwa mapenzi na mazingira yaliyopo,
hapo kila mtu akielezea kwa maono yake.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...