Sunday, November 18, 2012

MUDA WAKO…

Hakuna anayeelewa kwani wengine wanasubiri waelewe wengine ndiyo wanafanya, bila kujali muda yapasa kufikiri pengine kuwa na wazo, Tumetofautina namna ya kupanga muda wetu,  muda haungoji mtu, ukiwa na subira utapata,pengine hata ukiwa na subira na usielewe unasubiri nini, utakuwa umechezea muda wako , unapopanda ngazi usidhani ni mlima maana kwa kupanda na kushuka, korofi nyingine hazina maana ya kuleta kuongeleka, muda wako ukifika kitaeleweka.

Leo jambo na mambo yameongeleka, kwa yale uliyoyasikia machache ndiyo ya kuweza kuukamilisha muda uliobakia, pengine ikiwa hakuna muda uliobaki basi itapaswa kuongezwa, ikiwa kuna mgonjwa  hilo ni la pili maana wa kwanza hakujiweza, ukisema upo njiani lazima ujue unapoelekea, na uliyefika ulitumia njia gani ili ikiwezekana ukawe wa tofauti. Unapofikiri fikiri na utofauti uliopo, maana kwa kujifananisha unaweza kujiona Kenge wakati wewe ni Mamba.

Ikiwa umekubari kuwa mamba ni lazima ujue kuogelea nchi kavu, mwanadamu anayeishi katika maji huyo kazaliwa huko, na akija nchi kavu lazima aogelee mavumbi. kwa Yule anayeelewa mda wake ni lazima kuufanya si ya kuhofia mavumbi, maana kama kuchafuka unaweza  usitakatishe roho wakati wa kusuuza ila ukaja muda wa kuvaa na kusema mashine hazikufua  vyema, muda ndiyo unaotufanya kuzeeka, haipaswi kuustarehesha muda wako.

JITHAMINI.

Haina thamani kuuzungumzia ujuzi na wakati uwezo unao, Haitawezekana kuzungumzia ya zamani na wakati mapya yapo, uwezo unaoendana na wakati ndiyo unaohitajika, moja sitajidanganya kuwa nimechelewa kufanya ya pili hoja, watakataa sasa yakuwa haijulikani lakini thamini unachokifanya pengine yakupasa kuuliza  maana unaweza ng’ang’ana kujenga barabara na hujui mwelekeo, maisha yametofautiana yanaenda na wakati wake .

Hakuna aliyeumbwa hawezi labda yule asiyejua thamani  katika maisha yake Mabadiliko yanatokana na mtu mwenyewe, wakati mwingine inakupasa kuongea peke yako ikiwa yakupasa kujua yako kabla wengine hawajayajua, maana unaweza kujulikana ndiyo kumbe si hivyo, wapo wanaoteseka kwa kufanya yaliyo sahihi na kuonekana si sahihi kwa sababu ya kutokujiamini ama vile mwingine anavyokutathmini.

Usikate tamaa katika maisha  maana kesho  inakuja kukuletea thamani yako. Ngoja,jithamini jiamini itakuwa tu. Hakuna linalowezekana bila imani usipoijua imani utahukumiwa kutokana na uelewa wako, mabadiliko siyo mafanikio au yakafanye kuthaminiwa vile utakavyo, mtu anaweza kujibadilisha kwa  lengo la kupata jambo, ukikubari kubadilika rangi kama kinyonga haitashangazwa kuitwa kinyonga ila kubadilika tu ni ishara tosha ya kuwa kuna utofauti.



ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...