Thursday, October 5, 2023

NEEMA YA MUNGU

 Neema ya Mungu haipangwi na mwanadamu ,maana siwezi kuomba na kutaka nijibiwe kesho ama muda ule nitakaotaka ikiwa naamini Mungu anapenda maisha yangu na yupo bize kuhakikisha shetani hanichukui moja kwa moja,

Ufahari na mafanikio  unaweza kuwa hitaji la kila mmoja lakini vitu hivyo vinagharama na unaweza kulazimisha kugharamia ukawa navyo lakini ukakosa namna ya kuendesha na kufurahia uliyochonacho,ikawe muomba jiwe akapewa mkate.

Namshukuru Mungu hata nisingekuwa hapa,naishi vile Mungu ametaka na ifike kipindi nisisahau wala kudharau kusali na kumwomba kwa kuwa yeye ananipenda,anabadili kile kitu kinachosumbua nafsi yangu ,anajua ninachohitaji na muda wa kunipa.

Najua maisha yangu hayajabadilika hivi hivi bila neema ya Mungu,pale ninapo muomba ananipa,anabadilisha mazingira.Hata kesho sitasimama peke yangu maana ndiyo umenifikisha hapa nilipo,

Maombi mengine ukatizwa na hofu na kuzuia neema zisikudondokee,namuomba Mungu nifanye tofauti na hofu ilivyo iwe kutaka,kuendea na kukipata kukiwa na maono juu ya kile ninachokihitaji,

Ndoto hata ikifeli moja ntaota tena maana neema yako Mungu haina muda kamili,muda wa kupata kitu zaidi kile mtu usichokidhania.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...