Sunday, July 1, 2012

CHAPA NG’OMBE.


Ni kauli vile mchungaji akimwambia mwanafunzi wake,maana sio kila mchungwaji anachungwa na mchungaji mwema,wengine si katika maovu bali ikiwa bado kutokujua kuelekeza,yaani wewe ng’ombe usipite hapo ni lazima na viboko?maana bora hata Ukamsukuma pengine mnaweza kusikia yaliyo karibu naye akalalamika tu,mnachapa sana ngombe hawa hii ikiwa ni historia ya kwamba ni bora akawa anachapwa chapwa hapo ukiwa unataka ngozi ,yeye yule sasa akiwa ameumbwa kama mwanadamu,ya kuwa na kizazi,yaani wote ni binadamu..sishangai pale unawaita watoto mbwa,ni mbwa pekee anayeweza kumzaa mbwa.

Labda utafute madawa ya kukaushia ngozi,maana ng’ombe wameskika wakilalama sana,ingali na viboko hivyo imekuja hata wanyonyaji,hata muda wa malishoni kwa ngombe imekuwa taabu,fikiri mchungaji anapolala hulala na usingizi upi na Yule ngombe alotoka machungoni kwa viboko?maana hilo la mchungaji sijui ndiyo kuendeleza nchi ama ni kutengenezana baadaye wakapata maziwa ndani yake,hutajua maana ya kiboko cha mgongo ni uelekeo wa wapi zaidi ya kutia maumivu.

Katika lile linalomuumiza mwanadamu ndiyo lile au yale yaliyotukia na furaha,maana hata mwisho wa sukari ni uchungu,pengine mchungaji utuulize kuhusu utamu wa viboko hivi,maana si kulalama,ila isemekanavyo maumivu yakizidi umwone daktari,sasa kama daktari amegoma  haya maumivu yanatokea wapi ikiwa yule daktari ni mwanafunzi,angelikuwa mwalimu asingekubali kuikosa heshima yake uelekezani,maana ni wito huo na mchungaji punguza namna ya nguvu zitumikazo kuchapia ng’ombe wako,maana kuna wale wenye vichaa,wakiruka kile cha kukanyaga  ni kesi yako mwenyewe,maana utaelezea imekuwaje hata viboko ukashindwa kuchapa,au vilichapwa kwa namna ya utofauti yaani yakaanza maumivu na kichapo kikaja baaadaye.

UCHUNGU


Uchungu wa uzazi aujuae mzazi,tena ikiwa Yule anayeujua uchungu katika kuzaa,hapa isiwe nazungumzia uzazi,pengine tukafikiri ni namna  gani pale ikaeleweka Fulani ana machungu..si ya kuwa kwa kwengine ikajulikane namna hiyo,bali Yule aujuae uchungu,akauelewe kwa vile uumavyo,kumbe ni maumivu,kumbe uchungu unauma,haya si mambo ya Kiswahili,pengine tusitake ya kizungu ila yakawe yanaeleweka basi..nakubali katika lile mtu asemalo,kwani kweli yake ipo humo,humo anakuwa ameamua yeye maana ni mahala,kama ilivyo pale,yaani ndani humo,pengine ni duniani,yakuwa machungu yameonekana kuwa mengi,duniani kuna maumivu..!!

Sikatai hakuna kulalama,pengine tukawaruhusu wezi kutuibia,maana kama hatutasikia machungu basi wezi endeleeni kuiba….maana ifike wakati hatujaelewa kwa nini wanaiba,maana hayo si ndiyo maovu..mengine machache lakini si yote hata hili moja linatosha sana,katika kifo cha mwizi kinatia uchungu sana,sijui Yule anayaekufa huwa anasikia maumivu gani?ikiwa hatujaelewana nitafanya kurudia,lakini tukubari na machungu yatakayo tujia,maana tunyoshe mikono haya tumeyashindwa,na tusiposema hivyo lazima tuulizwe yaliyopitwa…hapo ndiyo tutaona machungu,maana yalipitwa na imepasa kuyarudia,’ni kazi kubwa kuirudia adhabu’

Kila ya jana yanaisha ninapoamka asubuhi,hii ikiwa nimeamka,nafsi yangu ikiwa inaniambia kufanya kile kizuri cha jana kilichobaki,maana ndiyo kitaleta kesho,hapo nikiwa naogopa machungu,sasa huyo sio mimi na mimi nitasema machungu yangu yapi?ama iwe mimi wa sasa ndiyo kama mimi..hapa nimezunguka sana,baadaye itaitwa mizunguko,maana ikinyooka wanaita minyooko labda iwe na majungu,yakifikirika kinamna yoyote tofauti na msemaji hayo ni majungu,,maana si vile kila mtu ana machungu yake naye afanye yake,ikiwa kila mwanadamu hapendi kulia uvunguni.

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...