Tuesday, January 31, 2012

MENGI YAMEDONDOKA.


Ikiwa ni kutoka juu hadi chini,chini hadi chini kabisa au juu kwa juu huko huko,pale pasipo kuwa na uangalifu mzuri na mara nyingine ukaseme ni bahati mbaya,Yaliyokuwa yameshikiliwa ndio sasa yanahitaji msaada,maana hata wale walio kuwa na nguvu wameamua kuachia,yanayodondoka huwa hayasemi zaidi ya yale yanayoshindikana.Kwa nini kama kudondoka tusingedondokea juu huko huko,maana yule anayedondoka akiwa chini yeye hubaki pale,na kwa yule aliye juu ikawe ni mshangao mkubwa tena.

Ikiwezekana umesahau maneno yetu ulipokuwa mtoto tukiyasema na ndiyo maana imefika muda shikamoo zimezidi,sio kwa utani lakini muda umesogea,angalia tusije kuwa sisi ndiyo wazee,kwani watoto wanazo zao,na kamwe mtoto hawezi kulingana na mtu mkubwa ikiwa hata anaumwa,ukumbuke ile ngoma ya watoto inakesha kwa namna yake,yale ya zamani yamekuwa ya kisasa zaidi,hawakua na mambo ya ujana ambayo yapo katika kipindi hichi na yanamaliza nguvu ya taifa,ingawa ilikuwa ni kipindi cha ujana wao.

kwa sasa wazazi wanashindwa kufanya lolote na watoto kukua katika namna wawezavyo wao,hatukatai mtu kuwa mzungu,kuwa mwarabu,lakini ni lazima mtu anaye taka kuwa katika jamii tofauti na yake ajielewe yeye,ajitambue ya kuwa hakuna muda wa kufananisha zaidi ya kufanya,yakuwa mwanzo unaonyesha mwisho upo katika namna zipi,njia hufanya mwanzo kuwa mwisho mara nyingine,kwani inapaswa kuurudia kwa makosa machache yanayotusibu katikati ya safari yetu ya maisha kabla hatujayamaliza.

Wale wanaotembeza sio wale waliopendeza,ikiwa haikusemeka hivyo,uzuri kila mtu anao wake,tukiambiana watu ni wabaya basi itakuwa ni vita ya kuutaka uzuri kwa lazima,tukiwa tunatoka safari tuangalie mizigo yetu tusije kuisahau nje,maana na wachache tukaonekana tumependeza wanajua tunapesa,tumefanikiwa kumbe ni tumefanya ili kuweza kutembea vyema,maana wachache hawachelewi kukwambia umepungukiwa akili,ila wakifanya wazee si mbaya kwani ndiyo walivyokuwa navyo na walitembea hivyo.

hata ikiwa akaja mgeni na kubisha hodi,mshikishe jembe huyo,mwambie ndani wasafiri walipaki vyao na wamelipia pesa nyingi ikiwa hawataki usumbufu,tukalime na hao wageni maana si wamekuja na majembe wenyewe?angalia unapofundishwa na mwalimu mgeni,kwani lazima ujiulize wa kwanza yupo wapi?kama kashindwa uangalie Yule aliyeweza,muda unapita na utakao fuata ndiyo wetu maana sisi ndiyo wazee,na usikubali kuacha mafao maana utasumbuliwa tu,taarifa za mbali zinaweza kuja zikiwa zinatuhitaji na lazima ujiandae kwani ni sisi wa kuongoza,umwangalie sana Yule mzazi wa mtu mwingine anapomwambia mwana wa mwingine kuwa hana adabu,ikiwezekana ijulikane kama adabu yake ni nzuri ili tuache za wazazi wetu.
‘sio kila kitu wazee’.


By:Benson G.Makaya,
Tel:+255714336657
Email:bensonsmakaya@gmail.com

NAMI NIWEMO.




Ikiwezakeana sura yangu iwekwe kwa kaisari,kilichoniweza ni kile nilichokiongeza,cha kwanza nilikuwa nacho mapema,ndiyo maana ya kuja na kusema,ni maongezi nikifikiria,pembeni haina haja ya kukuitia,tuongee pamoja tuelewane tusije jutia,ni mjita wa suguti mara musoma nimetokea,muda wote haina haja ya kuitajia,tumefanya vingine kwa waliotofauti ikaeleweka,wale wachache..tusiotaka hongera kwa makosa yetu,kila mtu anayafahamu ya kwake!! inanikumbusha kulee,kule kwenye sura yangu,angalau basi tufikiriane ndugu zangu,labda nimesema hivyo hata nikiwa nina nia mbaya,wala si uongozi wangu utakuwa mzuri,ubaya wangu hautadhuru lolote ni mimi na uongozi wangu.Labda tufahamishane kwa hili,nikipata nafasi ya kupiga picha ntapiga kama ile katika shilingi mia,moja ile ya upande fulani,muda unavyoenda tutachaguliwa wake ,maana naona nguvu zetu zinaisha,viwili kwake chake,moja kwetu vyetu,hii ni mbaya ikitokea kwetu,labda tusijue nini maana lakini ombi langu ni hilo,moja..hili la sura yangu kuwapo pale,najua ntaweza ikiwa sijafika hapo waje wawaambie,zikiwa kama hadithi kwa wale watakao chelewa sana.

Tusitake maisha ya kurudi utoto bila kujua tutawarudishia wapi watoto wetu,maana tuwape na njia ili wale wenye watoto wengi wengine wajisaidie,hata kama ni njia na zenyewe zimekuwa ni nyembamba zikihitaji nguvu ili kupita,tukisema kukonda ili kupita vyema wao wanasema tumepata ugonjwa wa mawazo na tukinenepa inakuwa vibaya kwa mapitio,itabidi tutafute njia yetu.kilichozidi zaidi lazima kiwe na sifa yake iliyoongezewa zaidi,ni kweli maisha yalikuwa ni magumu lakini hii iliyopo ni zaidi,hakuna asiyejua kuishi labda asikuelezee,yale tunayoyataka yataleta maafa,nikiwa sijui maana yake labda,niseme maswali ya dunia nakumbuka kauli hii nilipoulizwa kwa nini maswali ya dunia jibu likaja ya kuwa hilo nalo ni swali la dunia,hatuwezi kwenda na maswali huku majibu tumemwachia mwengine,maana kama ni shule zimekuja hadi za lugha tofauti,hili si kosa kwani shule ni kujifunza na endapo unataka kujifunza unatakiwa kujifunza kitu ambacho wewe unataka kujifunza,haina mshangao ila ni ya kustaajabisha sana shule watu tumeenda za nini?maana ionekanavyo tu wengi sana tumesoma na maswali yakiwa hayana majibu.

Labda kama sijamaliza lengo lieleweke,maana inaweza kutoka picha tofauti na ndugu zangu wakasema 'tulijua sisi' ,wengine humaanisha vyao daima,bila ya kumjali mlengwa,hakika matangazo tunayaona,tumejitahidi kulemba sura zetu zikiwa na ujumbe mbalimbali tofauti,hiyo yote ikiwa ni kushawishi,hapa napo tunashawishi lakini imekuwa ni namna tofauti,kwani lengo hapa ni uwepo wa sura tu mahara pale,pengine hata nkikumbuka kwa kipindi kile waswahili ndugu zangu walikuwa na usemi juu ya upendo ingawa unawezekana bado ukawepo,nakupenda sana nikinywa maji nakuona kwenye glass,yaani mzungu hapa anakwambia ‘indeep’,huu ni undani..ingali bado tunaendelea kuishi basi ukawe undani wangu mwingine.tumalize na hili...

‘Ikiwezekana sura yangu ikae katika shilingi’

By: Benson G. Makaya,
Tel: +255 714 33 66 57.
Email:bensonsmakaya@gmail.com


ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...