Thursday, February 16, 2012
Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!
Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!: Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia kote,hatuwezi kuan...
BINADAMU ANAPOTEMBEA.
Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali
mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia
kote,hatuwezi kuangalia kote bila kuwa
makini,yaani utambuzi kiujumla
kujielewa.Hatuwezi kusema wote tunaangalia kote,kwani wote
sio wale tunaotembea,na hii haiwezekani,ni kweli tunatembea,na ni kweli sio
wote.muda wote tuseme sio haki kutendeka lakini ndio inatendeka,hakuna yule
atendaye lisilotendeka na likaitwa tendo
bora,matendo ni yale hasa tuyatendayo,ndiyo na yote sio mageni,sio yale ya
kushoto wala kulia,ya chini yatabaki huko maana hayana haja ya
kuyafikia,wengine watasema hawajawahi na kama kutenda ni kuwahi basi wote tumechelewa.
Sio yale tuliyonayo tukimaanisha tumeyatenda,hata
kama tumeyatenda si yale tunayoyasema tumeyaweza,yapo yote na
tuliyoyashindwa,tunapotembea sio miguu tu kwani hata akili nayo hufanya kazi
kubwa mikono nayo pia ikatembee,muda mwingine tutembeze na mioyo yetu.Wengi
watu hatuelewani,tumesahau kuwa hata wale wa zamani waliandika,ndiyo wale
waliotembea wamefika hadi hapa,waliacha akili zao zinatembea,sasa wengine wakiangalia
wanavyotembea wanapofika ni pale walipo,mahala na muda wanautaja kama ulivyo,ya
kuwa wapo hapo.Kama matembezi ya maelfu yameshindikana basi hatutaweza
yoyote,wataweza wachache,ni kama ilivyo shule kwani chochote kile sio cha
kusoma,cha kusoma huwa wanaambiwa soma hapa,elewa
pale unaposoma,jua unachokisoma sio kile unachokiona,macho hayadanganyi lakini
kwa dunia jinsi inavyotembea haiangalii mwanadamu amesimama ki namna gani.
Tusherehekee vyote na tujipongeze hasa pale
tunapoona tumeweza kukimbia,ikiwa ni wengi wanapenda kuwahi,labda tutembee
haraka tu tusikimbie,yakuwa hatujui tunakimbilia
wapi,tusije kimbilia bomu,bomu hufyatuka endapo pale kunakuwa hakuna
uangalizi na yule anayekimbia uangalizi wa sehemu aliyopo ni mdogo
sana,tukubari yote ya kuwa tunauwezo wa kukataa yote,kwani hata tukisema ni
kutaka ufikiriavyo wewe lazima wengine watakubari huku wengine watakataa,labda
tuseme haina haja ya vyote hivyo,watakao kataa na kukubari vyote kheri kwani
yule anayekataa njia hii anayo nyingine,yakuwa
anataka kupanua uelewa,ili asaidikike atakua ametembea.
TEMBEA UYAONE..
By: Benson G. Makaya,
Tel:
+255714336657.
Email:bensonsmakaya@gmail.com
Subscribe to:
Posts (Atom)
Makaya's Forum: ELEWA 2
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
POPURAL POSTS
-
Kule kwetu kuna mahala panaitwa makunguru,ali hali ingalikuwa nzuri tungalihamishia ikulu, mambo yamekuwa mengi hata ya kujisti...
-
Yafanye mapito yako kuwa nguvu inayokusukuma kwenda mbele ukitegemea kuishi ndoto zako na sio kile unachokiogopa na kuhofia,wengi hawafanyi...
-
Kufikiri ni kuwa na hitaji la kurekebisha jambo,kunatokana na mawazo,kwa hiyo fikra zinaweza kuwa ni mawazo,kufikiri ni kitendo,kure...
-
Unaweza kufanya jambo bila hali yoyote,maana kutokuifikiria na hata ikikatalika mwanzo mwishoni ukikosea utasema samahani,kwa sababu u...
-
Sometimes you can find strong powers of concentration in yourself. When you really and earnestly want to excel in your studies, pass an...
-
» Most people with personality disorders have what is sometimes referred to as "disorders of the self," because they often do...
-
When there is darkness , we need light... Light is direction , light makes the appearance to be consistent if the view ...
-
Lugha ni chombo cha mawasiliano,watu huwasiliana kupitia lugha tofauti ikiwa nao wako tofauti,bila ya kuzungumzia nadhifu za nje,lugh...
-
Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...
-
More of my love for you, you increase your pocessions and with how they can, You make me, When you give me the courage which is suitab...