Thursday, February 16, 2012

Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!

Makaya's Forum: BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!: Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia kote,hatuwezi kuan...

BINADAMU ANAPOTEMBEA..!!



Binadamu anapotembea anaangalia wapi..?maswali mengine bwanaa!!tuseme ni kushoto ama kulia,wale wenye uwezo huangalia kote,hatuwezi kuangalia kote bila kuwa makini,yaani utambuzi kiujumla kujielewa.
Hatuwezi kusema wote tunaangalia kote,kwani wote sio wale tunaotembea,na hii haiwezekani,ni kweli tunatembea,na ni kweli sio wote.muda wote tuseme sio haki kutendeka lakini ndio inatendeka,hakuna yule atendaye lisilotendeka na likaitwa tendo bora,matendo ni yale hasa tuyatendayo,ndiyo na yote sio mageni,sio yale ya kushoto wala kulia,ya chini yatabaki huko maana hayana haja ya kuyafikia,wengine watasema hawajawahi na kama kutenda ni kuwahi basi wote tumechelewa.

Sio yale tuliyonayo tukimaanisha tumeyatenda,hata kama tumeyatenda si yale tunayoyasema tumeyaweza,yapo yote na tuliyoyashindwa,tunapotembea sio miguu tu kwani hata akili nayo hufanya kazi kubwa mikono nayo pia ikatembee,muda mwingine tutembeze na mioyo yetu.Wengi watu hatuelewani,tumesahau kuwa hata wale wa zamani waliandika,ndiyo wale waliotembea wamefika hadi hapa,waliacha akili zao zinatembea,sasa wengine wakiangalia wanavyotembea wanapofika ni pale walipo,mahala na muda wanautaja kama ulivyo,ya kuwa wapo hapo.Kama matembezi ya maelfu yameshindikana basi hatutaweza yoyote,wataweza wachache,ni kama ilivyo shule kwani chochote kile sio cha kusoma,cha kusoma huwa wanaambiwa soma hapa,elewa pale unaposoma,jua unachokisoma sio kile unachokiona,macho hayadanganyi lakini kwa dunia jinsi inavyotembea haiangalii mwanadamu amesimama ki namna gani.

Tusherehekee vyote na tujipongeze hasa pale tunapoona tumeweza kukimbia,ikiwa ni wengi wanapenda kuwahi,labda tutembee haraka tu tusikimbie,yakuwa hatujui tunakimbilia wapi,tusije kimbilia bomu,bomu hufyatuka endapo pale kunakuwa hakuna uangalizi na yule anayekimbia uangalizi wa sehemu aliyopo ni mdogo sana,tukubari yote ya kuwa tunauwezo wa kukataa yote,kwani hata tukisema ni kutaka ufikiriavyo wewe lazima wengine watakubari huku wengine watakataa,labda tuseme haina haja ya vyote hivyo,watakao kataa na kukubari vyote kheri kwani yule anayekataa njia hii anayo nyingine,yakuwa anataka kupanua uelewa,ili asaidikike atakua ametembea.

TEMBEA UYAONE..

By: Benson G. Makaya,
Tel:  +255714336657.
Email:bensonsmakaya@gmail.com

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...