Friday, April 27, 2012

USIULIZE


Hatupunguzi machache kwa mengi uliyoyaona kimya ukiamini kile kinachokuongezea,
maana kwa mengi wengi wetu na vichache vyetu tumekosa imani na hata kama ni ya shetani ijulikane basi,ukifikiri ni chaguo maana na wengine wanakataa hili sio lile,au vile ya kuwa mtenda ni mmoja,mengi yapo kutokana yanaendelea kuja yaliyokuwepo yanatakiwa pengine ndiyo maana hautaki kuyaona,ni vitu vingi kweli vitakuchanganya haujichanganyi mwenyewe haujachanganyikiwa kwa kuwa mambo yanajichanganya yenyewe na kuwa yanakuhusu basi inakulazimu japo kuchanganyikana nayo maana pengine imekuwa hadimu ikiwa kwa kusikika kwani inahitaji kusikiliza mara mbili ili kuelewa maisha yako yanataka jibu gani,kama hauna subira kwa kuvumilia basi utaishi hivyo kama umechanganyikana vile

Wachache wako utawakumbuka ndiyo wale wa kipindi kile ulipojibu swali wakasema umepata,haji mgeni usiyemfahamu ukamkalipia maana itahitaji kutoa akiba iliyopo kama siyo upendo basi si haja kuzungumzia,maswali mengine utaacha kusikilizana maana yanakela sana,usifikiriane kwa kuyaweza mambo inapofika mtoto anaitwa baba basi huyo nimaana nyingine baba naye alikuwa mtoto.Imefika kipindi cha biashara kudharaulika kabisa kama zilishindwa korosho na misonge kuuzika sasa watu watakula nini sawa isiwe hawavai kwa uoto wa asili kama ilivyokuwa inawezekana kujistili kwa mvua za ukame na mwingi utitiri ni kama kuuza mwili kuliko kufikiri.

Utafikiria vikubwa kile cha chini ni katika fikra za kwanza pengine unatoka nje ya sehemu uliyopo na sio nje yako,,lakini endapo unaendelea kufahamu maisha basi hilo hautalihusisha tena,maana penye kuchanganyikiwa kuna msamaha,chizi akiua huchukulika yeye ni chizi,na tena hapa usimfikirie chizi na kujisahau mwenyewe pengine ukidhani ukipata itakuwa hivi kwani ilivyokosekana ilikuwa vipi,usijejali itakuwa vipi bila kufikiri na ilikuwa vipi  vizuri anapewa mtu,hapa tusipeane uchizi kwa  kudhania ni kizuri sio vile mmoja aliye na  mawazo akawaza mtu anawaza vile.anayewaza kwa kujua wakati ndiye wakati wake maana amewaza hivyo,usibishe bila kujiuliza usiogope mawazo bila kubisha utajua kwa yale mabaya yakataze kabisa,na pengine mabaya yakaja kama mazuri.

By;Benson G.Makaya
tel:+255714336657
email:bensonsmakaya@gmail.com

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...