Saturday, April 20, 2019

BINADAMU UNAPOJIULIZA(usimwachie Ulimwengu)


Najiuliza umeniuliza kwanini Sitoi salamu nami huwa najiuliza pia kama huwa unaipata salamu yangu,ikiwa ubongo wa mwanadamu wa kila aliyeumbwa una swali la kujiuliza jiulize unaelekea wapi maana kila siku zinavyokwenda ulimwengu unaelekea na kuzidi kutoa maswali yanayoendana na technolojia ambayo haikukupa misingi yenye mizizi ya kina katika kujua mambo yaliyo duniani yanayoendana na maswali hayo katika kukabiliana na maisha ulimwenguni. 

Jiulize kama umeshawahi kujiuliza kwa nini unafanya kile unachoweza kukifanya ama kwa nini unahitaji kufanya kile ambacho unahitaji kukifanya?je pengine ukifikiri  kuna kuwa na uhakika wa kupata majibu ya maswali hayo au njia na majibu ya maswali hayo?maana aina nyingi za majibu yanayotokana na  kuangalizia yanakuwa hayana maana iliyokiundani pale inapokuja mtoa majibu anapoangaliwa kwa umakini zaidi, utekelezaji wa waliotoa majibu huelekeza swali hilo lilimlenga nani,ikiwa kila mtu ana mtihani wake hivyo hata majibu ni tofauti pia.

Nimekuja kuishi duniani hivyo nina kila sababu ya kufanya hivyo iliyo vyovyote ili iwe, niishi. kutangulia sio kufika lakini sio katika kifo na hii mara nyingi hunipelekea kujiuliza naishije ama ntaishije ? sasa hili ni chaguzi ukizingatia Moyo nao hutaka kuamua yake pindi majibu yanapotoka hivyo bila kuuhusisha moyo wangu huwa nayavumilia majuto ikiwa pia nazingatia na muda nilioanza kupata wajukuu na kusoma hali zaidi kupitia hapo, 

Kama ndugu yangu pia una jiuliza swali kama hilo pia basi jaribu kuangalia na moyo wako unasemaje ili majibu yako yakahusishwe na wewe binafsi.Na inapofika kipindi humwelewi mwenzio ni bora ukauliza au ikiwa unataka kuelewa jinsi unavyoelewa basi kaa kimya maana mengine yanakuwa siyo yako.

Maisha yana mengi ni mtihani hivyo maswali mengine siyo yako ukiyajibu unakuwa kama unatumia akili yako vibaya,Kama utapenda kuyajibu na kuona umepata zaidi basi Mwalimu(Ulimwengu) ndiye atakayesema kweli kuzingatia na muda na ujue binadamu ameumbwa kupambana kila siku, 

Usijali kama swali la jana limebaki kuwa swali  la nyumbani la leo inawezekana leo kulikuwa hamna swali pia jawabu ni kujipa moyo na kusonga mbele kwa kuangalia yanayofuata.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...