Saturday, July 14, 2012

HESABU...


Ni kama pale tunapowapa watoto wetu usaidizi wa kuweza kupata hesabu ali mradi wasikosee,hesabu hizi ni namna inayomfanya mwanafunzi kuona kama anaweza,hiyo ikiwa kama mtihani maana haina haja ya kuhesabu kitu bila lengo maalumu,tutaeleweka wehu kwa kuhesabu tu tena tutakuwa tunahesabu ili iweje?maana katika hesabu kuna kutaka kugawanya,kutoa,kujumlisha,na kuzidisha,na hii yote ikiwa inafanywa kwa hatua kwa hatua kwani kinachomaanisha katika yote ni idadi baada ya kutoa hesabu hizo,labda leo tujiulize sijui tupo wangapi katika nchi yetu,au haina maana ya kuwapo...?

Yaweza isiwe na maana ya kuwapo kwani tutahesabu nini wakati pesa ya matumizi imeshatoka..?la msingi ni kuingia sokoni kwa namna iliyopo na tutakavyo rudi navyo isije kuwa lawama,maana baadaye itaonekana kama watu hawakuhesabu vizuri, ni kwa sababu mwalimu alishatoa majibu yake mapema kumbe naye alikosea,kwani hakupiga mahesabu kwa yaliyopo,maana kama tutakosea kwa yaliyopo haina haja ya kufanya hesabu za mbele.

Wageni karibuni tu nyumbani chakula kipo,tumepewa pesa ya matumizi nyingi na bila ya kujua nani atazitumia,hii ni hatari kwani imeonekana hatukujua mtihani kama utakuwa na mahesabu ya kuzidisha,tutachanganyana sana hapo mbeleni,maana yaweza mzawa kukosa kula ikiwa hata mgeni naye amejiandaa na pesa zake huko alikotoka,tutalala njaa sana  na haina haja ya kulalama kwani tumeipokea vyema .

Hizi ni propaganda,tusiseme watu wamekuwa wazembe kwa kukosa kula na maendeleo finyu, baada ya hesabu washindi wakionekana wengi hapo tutajua nini cha kuwapa.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...