Saturday, September 1, 2012

CHEKECHO...

Mafanikio ni kwa kila mwanadamu anayehitaji kuishi,ikiwa katika mipangilio iliyo na mlango maana katika kutoka kuuliza waliingia wangapi isiwe shaka,maana wasije kutoka wengi kuliko walioingia,au pengine ikawe ni namna ya mtoko ya kuwa patapewa na jina kabisa,aliyeona mbali hasumbuliwi na wa mbali zaidi maana karibu ni ya Yule aliyeikaribia mbali yake,tukitangaza sifa kwa mbadala wa kujisifia maana tumedanganyika na  sifa zetu,leo tutasemsemea twiga na huku kuku akitotolewa na mwanadamu,pengine tuangalie hii namna ya uzungu,na hata vile vilivyo visafi kwa kuvaa nguo nyeupe ijulikane ndani yake,mwishowe ikiogopeka kuitwa rangi tuu ya kuwa imepauka.

Fikiri kubwa na dogo pia maana hata wateja wanataka nyongeza ya kupunguziwa bei,wakijisahau ni wauzaji wa bei kubwa,katika pambano la vita kifo ni rafiki wa siraha,kifo hakina huruma ya kuwa hakisemi,yaweza kuweka mipango lakini bado ikagonga mlango,maana ya mlango kugonga ni uwepo mzuri wa kizuizi,tukizuia dondora waliotoka kwenye mti wenyewe,maana hata harufu tu wanaijua,pengine njaa ikizidi sana hata harufu ya kinyesi haisikiki,hii ikiwa pua imechoka kunusa hata hewa,mazingira yote yakiwa  ni machafu,kwa waliotaka maji wakasingizia mifereji.

Linalomalizia katika mengi huwa ni la mwisho hivyo haina kusema namaliza,maana wakati unaanza 
haikutegemeka tena kuanza,labda kupitia mwisho wake,maana kama halikuisha vizuri basi ndiyo itakuwa limeendelea kuanzia hapo,maana huo nao huitwa mwanzo,wakati huo  ni mwisho pia,pengine ni katika kuchagua maana swala utuonyeshe na yale magumu umeyafanyaje,maana yaliyokuwa marahisi yalitamkwa kwa kusema asante ili mradi hata waliopata japo kuona kusema kashukuru,sio kwamba hatujui maana kuna wale wenzangu bali ni katika namna ya kutafuta uzoefu.

MUINGILIANO


Muingiliano wa kuongea imeletwa kupitia maneno yaliyoongelewa ikiwa  kwa uchache wa kuelewa ama kutokufikiri ikaleta namna iliyo tofauti ati kusema kwamba wachache walifikiria,na hapo ikiwa walishajipa maksi mapema ya kuwa wamekuwa haina haja hata ya kusema nani atakuuliza,maana kipofu asiyeiona si sawa na Yule anayeona asiyeona.pengine wasioona wakiwa wameona vyao na ili kuepusha muingiliano ni lazima kutambua katika nafasi uliyopo,ikiwa umepewa ya kuchangamkia,inamaana ya kumaliza mpaka mwisho ikiwa damu bado inachemka,na haki ikitakikana.

Katika nafasi ndogo iliyopo hakuna namna ya kusema ‘adjust’ hii ikiwa na samahani ndani yake,kwa maana ilivyo kwa kunenwa ,wengine wakija huja bila ruksa ati ni shemeji,shemeji mkeo maana ndugu zake ndiye wanakuita hivyo,kumbe shemeji ni heshima ilivyo kama baba,tena mkwe,maana wengine hawashangaliki zaidi kama wakitenda yao peke yao na wakitenda yao wakiwa na wakwe zao,hii inaashiria umungu katika kuhofia maana na nafsi ya mtu inabebwa na kile alichonacho,kama yangu katika maandishi yangu,pengine nakua nimesema japo nimeingilia kunena.

muda mwingine unaweza kuingia bila hodi kwani kuchangakiwa ni kama kuchanganya,yaani kuleta fulani ikaingiliana na fulani na matokeo yakajulikana yasipojulikana basi umechanganya zaidi.maana kama ili itokee juisi ni lazima kuweka sukari basi tulambe sukari yenyewe,ukaingiza hata visivyo tumika ali mradi ikaeleweka kwamba ni imepemdeza,ingawa sio yako lakini watu wanafanya hivyo,pengine ujaribu hivyo..ili kutokuingiliana.na kama inatokea basi inajulikana mapema.maana kama umeingia sasa hivi haukuwekewa nafasi,labda tuelezane kwa namna uliyokaa hapo.

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...