Thursday, July 5, 2012

ITAKAVYOKUWA.

Na kama ni ndani ya familia iwe ni mzazi ama mtoto ndiye anayemwambia mmoja wapo hapo ujue kuna namna,ile iliyokuwa kama vile katika namna,mtanisamehe sana ndugu zangu kwa kuwarudisha nyuma,maana huko mbele vyovyote itakavyokuwavyo sawa tu,sio kwa wazazi ama kwa watoto,vyovyote vile..

Mara nyingine usisema ni kauli gani wakati hautajua ni kwa sababu gani,maana hata ya kusema ni ile ya namna gani tu,uliporudi nyuma uliwakuta mababu zako wakikuambia,maana ulisikia,kwa yale yote yaliyo mabaya ni yale waliyoyasemea,walisema mengi ndiyo maana haina haja ya kuwaambia nyinyi,wale walio watoto maana muda si wake,unaposema itakavyokuwa si ni ile ile ni  iliyopo inayoendelea kufika mahala Fulani,hapo useme umepita muda mrefu sana sijalisikia swala lile.ndiyo itakavyokuwa hivyo

Ngoja ngoja itakavyokuwa ikaumiza matumbo,kama samaki mkunje angali mbichi akitaka kunyooka mwache kwani atainama kukiokota kilicho sharti,maana kipo chini,lazima kurudi mwanzo,maana kama utaendelea kunyooka utakiuka waliyosema,sio ya kijinga yale,yalikuwa ni kwa ajili yako,uchambue yaliyopo maana mengine yanaelekea kuoza,yasije kufanya na yale mabichi mengine kushindwa kukunjika.

ukisema kwani imekuwaje ndiyo ilivyokuwa,na mara nyingine haiwezi kuwa bila nyingine kuwako,kwa hiyo vile ilivyo ndiyo vile itakavyokuwa,uangalie muda tu,muda unaenda sana,siku hazijirudii ndiyo maana haiwi tena ,nyingine namna tu,na hata sijui kwanini zimekuwa haba kwa namna ilivyo,maana ingepasa kila mtu kuwa na siku yake,na kama ipo basi neno itakavyo kuwa lisingekuwepo,ungetamani siku yako ije tu,na utatamanije kila siku?itakavyokuwa ndiyo hivyo hivyo..maana wengine wameshaelewa ilivyokuwa.

MDUNDIKO..!!


Mpira unapodunda sana,maana hata control zikakushinda,umekuwa kitenesi hata katika namna ya kukidaka ikawa mzozo,pengine kwa ajili ya hawa unaowaona,hata ikawe hujui umeona nini namna gani ipi yaani mpaka ikaeleweka ile ni kwa nguvu na nyenzake kwa akili,ikiwa hatujui imedunda ama imepaa maana nguvu ya juu hutegemea na ya chini vile ilivyo kwa kipimo cha akili yakiwa yanashirikiana katika kuyasogeza marefu na mapana.

Vingi vinapaa lakini hatuelewi vinapaaje pengine ndiyo vinavyotembea hivyo,vinadunda yaani,ilivyo muda usemekao zamani watu walikuwa wakitembea miondoko Fulani ya mdundiko walionekana wahuni,muda huu imezoeleka kwani unajidundia mwenyewe,wee dundaa na badaye utaeleweka maana ndiyo itajulikana nguvu zako ulikuwa unazitumia katika upande gani,hakatazwi mtu mara mbili asipoelewa ni aendelee na yanayompa nguvu kuyafanya kwa wakati huo

Hata kumbe mipira mengine siyo yakuitumia hiyo wanasema inachezeka hata mchangani,sijui kwa nini isingekuwa haiwezekani,kurudi ni kufuta maana iliyopo ikiwa  nguvu iliyotumika katika kudunda kwa mara ya kwanza na kushindwa kufikia mara ya pili kujaribu tena hapo unakuwa umefuta,sio adhabu ni mazoezi ya kuweza kumbe hata mpira unapojaribu kudunda hutafuta mahala panapoleta maana,hapo utasikia ule umetoboka,basi hapo ujue kuna mtu kakosa lengo.

Dunda ndugu usiogope uwanja wako,maana makelele tumeyasikia na pengine yangekuwa kiburudisho hivyo vingine uviite kukua kwa lugha maana ukafikiri yametokea kwenye nguvu ama pasipo tumia akili ,kwa sababu ya kudunda huanza chini ikiwa na lengo la kuelekea juu au huanza juu ikiwa na lengo la kuelekea chini.Chagua namna unaweza,fanya vile unaweza.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...