Friday, June 22, 2012

MSINGI..


Katika makubwa yasiyo kuwa na ncha ambayo hayatakiwi maana ili msingi kuwa bora basi lazima ikawe imekuwa,kwa tena tusiseme eti ahh nilijua tu,pengine katika uwingi kila mmoja akasema lake,hapa  ikiwa kuna aliyekataa akasema yeye na mwengine akafikiria yake,hapa misingi inakuwa na uwalakini kutokana na muonekano wa nyumba yenyewe,

Kwa kile kinachojibanza haki hakitaki kuonekana,sasa hapa tusifuatilie sababu,wala haina haja ya kusema pengine yaliyopita ni ya mababu  katika bila kufikiri yalitendeka,hiyo ikiwa hayakuangaliwa mwanzo ama pengine msingi ulikuwa ni mzuri,

Katika ukubwa nyumba imeisha,katika yaliyo makubwa hata ukubwa unaisha maana kwa yale madogo ndiyo yanapotea,hata kwa kuonekana tu,pengine wadogo hao wakabomoe misingi,isiwe tupo huru kwa sababu ya nyufa zinazoonekana,pengine katika kufikiri ikaeleweka kwamba ile nyufa ni kwa sababu ya mwanzo haukua mzuri,maana imefika kwa nyumba kuuzidi msingi,haki labda na nyumba imekuwa kubwa.

Labda kwa kutegemea nyumba kuota  na kukua,maana inapandwa,imekuwa ni mbegu tokea kipindi hicho,na katika mashamba kwa hakuna Yule anayeelewa kama lake ni bora,zaidi ni heli kupanda kama mazao yataonekana baadaye hayo yaliyo bora,huku na pale tutahitaji msaada,maana aliyetengeneza msingi aliacha pengo kubwa kwa anayemalizia nyumba,hivyo yapasa kuoanisha msingi,hapa tukizungumzia hili moja tu.iisije nyumba kudondoka tukiwamo ndanni yake.

ISHI UTAKAVYO


Wengi wameonekana wakiishi maisha ya samahani hiyo ikiwa hawajafikiria ni namna gani waweze kuishi,kwa bila ya kujua nini wanachokifanya yaweza kuwa umefanya mengi lakini yakaonekana machache,umegandamizwa na maumivu mengi maumivu ya maisha na bado upo na pengine unapomaliza jambo uwe unafikiria kabla labda baada ya hili nini kitafanyika ili kugeuza kuwa na kufanya kile mtu unachokihitaji ukiwa unahitaji kuishi maisha yaliyo sababu yako.

Muda mwingine ushangae yale unayoyafanya pale yakaleta mshtuko,ukiwa umeelewa cha kufanya na ukachagua hapo unaweza kujua ukweli wako wa maisha na maisha ni kuishi tena vile unavyoweza ikiwezekana vile unavyopenda ,mafanikio yaweza kuwa hakufika ndiyo maana akaondoka ama kughairi hilo hutajua lakini Kile kinachokuja baaada ya muda unahaki kukijua na kukifauru maana kimekuja muda wako,hapa usipofikiria hofu ya  kuachwa na muda angalia usichague hivyo pengine wengine watakula kichwani na wewe uanze mkiani ama mwingine atataka paja na mwenzake kidali,pengine ni kutokana na ilivyo ama vile waipendavyo baadhi ya kila mmoja wapo.

Ishi ukiamini unajituma  na sio kutumwa,ishi ukiamini wewe ni bora Zaidi ya mwengine akuchukuliavyo,ulizaliwa peke yako sina hakika kama kua mtu mnagawana shida na raha,wengi wanaopenda na kuishi wanavyotaka hula raha zao na shida zao wenyewe na wewe ukifanya hivyo utakuwa umeishi vile unavyotaka na sio lazima iwe hivyo ila kuishi kutakuwa pale pale.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...