Friday, June 22, 2012

MSINGI..


Katika makubwa yasiyo kuwa na ncha ambayo hayatakiwi maana ili msingi kuwa bora basi lazima ikawe imekuwa,kwa tena tusiseme eti ahh nilijua tu,pengine katika uwingi kila mmoja akasema lake,hapa  ikiwa kuna aliyekataa akasema yeye na mwengine akafikiria yake,hapa misingi inakuwa na uwalakini kutokana na muonekano wa nyumba yenyewe,

Kwa kile kinachojibanza haki hakitaki kuonekana,sasa hapa tusifuatilie sababu,wala haina haja ya kusema pengine yaliyopita ni ya mababu  katika bila kufikiri yalitendeka,hiyo ikiwa hayakuangaliwa mwanzo ama pengine msingi ulikuwa ni mzuri,

Katika ukubwa nyumba imeisha,katika yaliyo makubwa hata ukubwa unaisha maana kwa yale madogo ndiyo yanapotea,hata kwa kuonekana tu,pengine wadogo hao wakabomoe misingi,isiwe tupo huru kwa sababu ya nyufa zinazoonekana,pengine katika kufikiri ikaeleweka kwamba ile nyufa ni kwa sababu ya mwanzo haukua mzuri,maana imefika kwa nyumba kuuzidi msingi,haki labda na nyumba imekuwa kubwa.

Labda kwa kutegemea nyumba kuota  na kukua,maana inapandwa,imekuwa ni mbegu tokea kipindi hicho,na katika mashamba kwa hakuna Yule anayeelewa kama lake ni bora,zaidi ni heli kupanda kama mazao yataonekana baadaye hayo yaliyo bora,huku na pale tutahitaji msaada,maana aliyetengeneza msingi aliacha pengo kubwa kwa anayemalizia nyumba,hivyo yapasa kuoanisha msingi,hapa tukizungumzia hili moja tu.iisije nyumba kudondoka tukiwamo ndanni yake.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...