Friday, June 29, 2012

MKUTANONI..


Mara kwingi ninapotoka ninakutana na watu wazuri,wakiwa wao ndiyo wao hasa ndiyo ikawe hata maana ya kukutana,pengine tukimaliza mkutano upate japo neno jema kwamba karibu kwenye mkutano,sijui ikiwa imetendeka nini ndani humo,maana kabla tulisema bila kujuana,pale ikaenda kimeisha kikao tupeane karibu,hizi zikiwa na maana ya sijapenda ulichokifanya na vile karibu sana,maana utasisitizwa hata siku nyingine,hapa sio kujua kwa kuwapo,ni kujua kwa kuelewa,tumejuana kwa kukutana.

Pengine sio bahati mbaya ila ni nzuri iliyokuwa na ubaya,kama vile jamaa alisema kuhusu mwongo ya kwamba ” Kuna mtu anauongea uongo si kwasababu amedhamiria ila ni kwasababu anajua huo ndio ukweli huyu hawezi kuwa mwongo, bali huyu haujui ukweli”.kwa kweli sio kosa la kukutana,bali ni vyema tumekutana ili kuelezana,pengine kila mtu awe na lake ili kuweza  maana,pengine ili kucheka zaidi ama kununa,maana ya kununa siijui zaidi yake,pengine ni kufa tu..

Sasa si italeta ugomvi,tena itakuwa ni bahati mbaya,maana kuna watu wanajua kununa kweli kweli,hapo bila ya kujua wanapoteza namna ya kucheka,kutabasamu..maana maisha ya mwanadamu aliyefanikiwa kiroho na namna awezavyo ni kucheka,hata kutabasamu maana ni mwanzo wa kucheka.

Hakuna maana ya kusema wewe ni nani wakati wewe ni nani,maana inahitaji uje kwa adabu tena ukitaka kusema wewe sio nani,maana hakuna aliyekutilia maanani,’hapo mwanzo alikuwepo sungura na fisi’,hadithi hizi hatuzitaki siku hizi.asante sana kwa kukutana maana imefika kipindi nimekueleza hata yale ya jana,ngoja kesho ije tutafayaje kama sio kusikiliza ya jana?kama umeyaacha mawili kayachukue,ikiwa haiwezekani ingia hivyo hivyo mkutanoni.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...