Tuesday, January 16, 2024

HASIRA YAKO

Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinakupeleka,binadamu tupo tofuti,mmoja hali nyama ya mbuzi kwa kuwa inamtoa vipele mwengine hali nyama ya nguruwe kwa sababu ya dini sasa nikikasirika usiniulize nimekasikia nini,nina mengi.

Kasirika,usikarike pasipo na sababu.upumbavu wa mtu mmoja usikufanye uvunje simu na mwengine kufikia kumkata mtu panga.angalia unapokasirika sauti yako ya ndani inakwambia nini na kabla haujatenda kwa kutumia kiungo chochote cha mwili yakupasa kutafakari,maana kuna wale wenye hasira za ndani(chuki) hawafanyi mambo yao hadharani.

kama ilivyo katika michezo mmoja akamchezea rafu mwenzake basi wanamichezo waliiga kwenye maisha,na ndiyo maana unasikia michezo haiitaji hasira,ukisusa wenzako wanakula na wenzako huwa wanakula mpaka baadaye ukakitamani tena hicho chakula,kasirika vizuri.

Dunia hadaa utakasirishwa wakitaka kujua maamuzi yako,ukishajua umekasirikia nini maamuzi yako yawe tofauti na hasira zako kwani kweli maisha yana mengi lakini kuna mengine sio ya kukasirikia fikiri mtu anakasirikia mafanikio yako na atayekumbatia maamuzi ya hasira zako yampasa kuwa yeye.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...