Saturday, March 30, 2024

ELEWA 2

 

Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa kuelekezwa,kimfumo kumtafuta mtu kwenye kundi ni ngumu,ili kutofautisha kama kuna mwizi,malaya au mlevi ni kuangalia alipoiba aliekea wapi maana vyote vinaweza kuwa vya mtu mmoja.

Sifa mbovu inayotembea ni sawa na rungu la kichwa ukiwa usingizini, katika miliki matendo mabovu yamekuwa yakitendeka bila woga kuliko mawazo ya mazuri,anayekusifia mazuri hadharani anakusubiri utoke,yule asiyekusifia ana ubaya wake mwingine wa kuelezea.ukigeuka watakwambia hawajakuita na hata wakikuita hawana cha kukwambia.

Kuna namna ipo umefanana na wazazi wako,hata isipokuwa sura basi hasira,tabia wengi wametokea utotoni usimlaumu mtu kwa  kuwa malaya vile unavyojisikia kunywa pepsi mwingine coca,vingine vipo ndani ya damu hivyo tembo akinya sogea mbali pengine uchafu utakumwagikia alafu iabidi uelewe kufuata yako.

Kuna muda huelewi,yaani hata nilichokiandika hauelewi,tatizo lisije kwangu maana ulivyovijaza kichwani mwako vyaweza kuwa kinzani na hivi,nikawa naandika kwa kutumia wino mweupe.kuna mmoja alisema yanatoka popote bila kujua yametokea wapi,ukitaka kupaa kuwa na mahusiano ya karibu na ndege.Usipojua yanatoka wapi jaribu kuwaelewa ndege kwanza.

Watu ni zaidi ya chochote,yoyote yule umwonaye.hata sifa zangu hakuna nzuri imekuwa kwa mwengine,maana kila mtu ananjia yake mafanikio sio utu,ukitaka pesa watakutesa.unapotaka kunielewa isiwe kwa mlengo wako,mtu akitaka kukuelewa asikuelewe anavyokuelewa Ukiishi usimwambie na mwenzio baadaye atajiita kuwa mshauri.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...