Wednesday, January 24, 2024

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO: Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahal...

Makaya's Forum: HASIRA YAKO

Makaya's Forum: HASIRA YAKO: Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinak...

Tuesday, January 16, 2024

HASIRA YAKO

Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinakupeleka,binadamu tupo tofuti,mmoja hali nyama ya mbuzi kwa kuwa inamtoa vipele mwengine hali nyama ya nguruwe kwa sababu ya dini sasa nikikasirika usiniulize nimekasikia nini,nina mengi.

Kasirika,usikarike pasipo na sababu.upumbavu wa mtu mmoja usikufanye uvunje simu na mwengine kufikia kumkata mtu panga.angalia unapokasirika sauti yako ya ndani inakwambia nini na kabla haujatenda kwa kutumia kiungo chochote cha mwili yakupasa kutafakari,maana kuna wale wenye hasira za ndani(chuki) hawafanyi mambo yao hadharani.

kama ilivyo katika michezo mmoja akamchezea rafu mwenzake basi wanamichezo waliiga kwenye maisha,na ndiyo maana unasikia michezo haiitaji hasira,ukisusa wenzako wanakula na wenzako huwa wanakula mpaka baadaye ukakitamani tena hicho chakula,kasirika vizuri.

Dunia hadaa utakasirishwa wakitaka kujua maamuzi yako,ukishajua umekasirikia nini maamuzi yako yawe tofauti na hasira zako kwani kweli maisha yana mengi lakini kuna mengine sio ya kukasirikia fikiri mtu anakasirikia mafanikio yako na atayekumbatia maamuzi ya hasira zako yampasa kuwa yeye.

ISHI NA YAKO

Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahala fulani,tambua maisha yana stepu,uliyopo sasa mwengine alipita juzi ukicheka leo mwenzako kulia ni sawa na kulia wakati mwenzako anacheka.

Usibabaike na waliowahi kufikia ukitakacho,tambua muda wako ikiwa unajiandaa jiandae vyema ili ukikosa isiwe lawama kwa wengine,maana imekuwa mmoja akishindwa akatoa sababu za mwengine kumuangusha.

Usifikiri ni raisi kukaza jambo,kuna mengine yanakaza mpaka kufungua inakuwa kama ni kukaza,ujiandae vyema maana kuna vilio,maumivu yasiyo na machozi na hata usumbufu usiohitajika.yatambue magumu yako na jipe muda kuyatatua ikiwa humu duniani wote mpaka muda huu tunatafuta maisha.

Kheri udongo unarudi utokapo maana ingekuwa foleni kubwa barabarani kwa kuwapa heshima wajionao miungu,usifikiri wakati wa magumu peke yake mwishowe ukawapa lawama watu wasio husika na maisha yako,tambua nafasi yako si ile aisemeayo mwengine,watu huwa wanaongezea kwa kile ulichonacho.

Monday, October 9, 2023

Makaya's Forum: NAONA

Makaya's Forum: NAONA: Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni ...

NAONA

Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni moto na unaunguza,Naona vingi ukipata uelewa ntakuelewesha.

Naona wamefunga milango wakijua upo nje,wamefunga njia ikiwa bado haujapita,wanakusema unakonda kwa kukataa kunywa uji,naona ukisoma herufi bila ya kuelewa,umeanza kuita mma ukijua ni uhai,naona chuki juu ya moyo mkunjufu,Subiri ukipata uelewa ntakuelewesha.

Naona hujajua kama sufuria sio kikombe,hujajua mtu anayesubiria hakupata hajapata sifuri,usikimbilie kuendesha vitakavyo kuendesha,subiria kupandishwa basi likisimama utashushwa,Unapokula usijichafue sana meza wapo wabaya watu wanaotafuna vya kumeza.

Naona unaanza kuelewa ya msingi,ukitaka kujisaidia waogope watu na isiwe kwa chuki ,kama umekuwa jua safari unaiweza na unapoelekea naona safari ndo inaanza,Naona unashindwa kufanikiwa kwa fitina nyingi,vita zipo nyingi kaa mbali na maadaui,binadamu yoyote anaweza kuwa adui bila hata wewe kutaka,naona unakuwa msuruhishi mbele ya ndugu zako na sio kuwagandamiza.

Kesho naiona tena,naliyaona ya jana yakanipa majibu ya kuwa mtihani ni ule ule.naona yake akae nayo yako baki nayo mwenyewe ili kutokuchanyikikika,Naona unakanyaga maji na hakuna sehemu yenye moto ,Naona nisikuchoshe Sali sana kaa mbali sana na ndugu msumali.

Thursday, October 5, 2023

NEEMA YA MUNGU

 Neema ya Mungu haipangwi na mwanadamu ,maana siwezi kuomba na kutaka nijibiwe kesho ama muda ule nitakaotaka ikiwa naamini Mungu anapenda maisha yangu na yupo bize kuhakikisha shetani hanichukui moja kwa moja,

Ufahari na mafanikio  unaweza kuwa hitaji la kila mmoja lakini vitu hivyo vinagharama na unaweza kulazimisha kugharamia ukawa navyo lakini ukakosa namna ya kuendesha na kufurahia uliyochonacho,ikawe muomba jiwe akapewa mkate.

Namshukuru Mungu hata nisingekuwa hapa,naishi vile Mungu ametaka na ifike kipindi nisisahau wala kudharau kusali na kumwomba kwa kuwa yeye ananipenda,anabadili kile kitu kinachosumbua nafsi yangu ,anajua ninachohitaji na muda wa kunipa.

Najua maisha yangu hayajabadilika hivi hivi bila neema ya Mungu,pale ninapo muomba ananipa,anabadilisha mazingira.Hata kesho sitasimama peke yangu maana ndiyo umenifikisha hapa nilipo,

Maombi mengine ukatizwa na hofu na kuzuia neema zisikudondokee,namuomba Mungu nifanye tofauti na hofu ilivyo iwe kutaka,kuendea na kukipata kukiwa na maono juu ya kile ninachokihitaji,

Ndoto hata ikifeli moja ntaota tena maana neema yako Mungu haina muda kamili,muda wa kupata kitu zaidi kile mtu usichokidhania.

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO

Makaya's Forum: ISHI NA YAKO : Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha...