Friday, September 14, 2012

YANAWEZEKANA LEO.

Nilijua ilikuwa ni mara yangu ya mwisho kukuona na japo kukusabahi,maana pengine ilikuwa ni dakika za mwisho kwa lile lilotakikana jana likaja leo,hapo nikawa nimekuchelewa kwa kutokuwahi muda,maana itakuja kila siku na kuona kwamba yaliyopita ndiyo ndwele,hapo chululu tukitaka kujua maana,isisemeke na kujulikana kama imesahaulika kwani katika upendo unaweza kuwapo hata kwa adui yako,leo nikisema na kesho ntaweza kurudia,maana nikiwa na hitaji la kutokusahau.

Leo ikiwa imekuja haijaja kwa ahadi kwamba ndiyo imekuletea vizuri,gari,tunapenda sana magari kwa kutaka kusafiri na kuelekea kusikojulikana,kwa kijana ama kenda umri namna gani leo ikitakiwa kuwa ni siku ya nafasi,kwa vile vinavyopendeza vikashikana ili kuzuia mmomonyoko,si ya kuwa yakidondoka kwa uzembe wa kutokujua uongozi na kusahau kusubiri kesho wakati kuna leo,pengine tukifuatana na ya jana ili kuleta maana.

Unaweza kulaumu siku yako kwa kutokuona kesho inakuja,maana hiyo na hayo ni mafanikio tu,pale unapopenda una chukua muda ikiwa hakuna makosa na haina haja ya kulaumu,ama hapo ndiyo tuamke na kusema samahani,makosa mengine waweza yafahamu mwenyewe kwa kutokujua kulaumu kesho.ikiwa aliye na hitaji na kuishi na kufanya yeyote anayoyaweza bila kungoja kesho.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...