Tuesday, July 10, 2012

ULIMI..


Maneno hayana pa kutokea kama sio mdomoni,ilivyo maandishi kwa kuandikwa,pengine ukiwa unataka haraka kuelewa nini maana ya ulimi kabla ya kuufahamu mdomo,kile kinachotoka katika ulimi kinapita mdomoni pia,maana mdomo umejawa na yaliyo katika ndimi ni yanapita tu,

Ni  maneno ya wasanii,wasanii wachache wanaofundisha wakitaka kueleza,mimi ni mlinzi ya kuwa nalinda. na Yule anayemuongoza mlinzi yeye sijui anafanyaje..naogopa kugeuza ulimi wangu,kwani sijasema nimeshindwa kulinda.Haya hayajalambwa labda uyaone ya pembeni,

Vyovyote iwe ikataje kwa namna iliyozoea,naupenda ulimi wangu kwa uvumilivu
 wake,nikikumbuka mara ya kwanza nikipata pilipili,maana nao ulipokea ukisema haya ni mafunzo,tena elewa..asikudandanye mtu hili limeshindikana,maana ulimi unaweza kuwa umegeuka,hata usijaribu kugeuza ikiwa hautaki kusema tofauti,maana hata mpaka  sasa umedanganywa sana na kuambiwa samahani ni ulimi tu..

Unapofanya meno yako yafurahi ni pale uunapoulaza ulimi wetu,kweli hata mkafurahi wengine na wakapewe shida nyingine,maana ulimi kazi yake kuleta maneno.wacha waseme ,watasema mchana usiku watalala,akianza kumung'unya tu ujue ulimi unaelekea maala pake.
ukikaa kimya inaeleweka umekubali,asikukubalishe mtu asijue ni kwa shida ama ni kwa raha tu.

Maana meno yamefanya kazi sana,hata wakasema wasisikike,tena ukifikiri ni nini kama sio ni wewe mwenyewe umeamua,hapo unataka kusema kama unataka kusema utakatwa ulimi,sijui ili meno yasichoke na vingine tunadanganyana sana,vingine havina maana.


ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...