Friday, August 31, 2012

NATUMAINI


Ningetaka kulia ningejifungia maana ingekuwa haina maana kuonyesha machozi hadharani,kwa kila mtu akiuliza unalia nini maana wataniona tena wao wakiwa na matumaini katika yale yanayowaumiza juu yangu,ikiwa katika kuanza kutumaini ni kutaka kupumzika katika sehemu na mahala salama nimeshafahamu majibu ya maswali mtakayouliza na hakuna jibu zaidi ya mtu akakuuliza ikiwa ndiyo nlitakiwa kujibu hivyo nikiwa namaana ya ninachotumainia ndicho,pengine katika matokeo ikawa sio matumaini yako,kwa upande wa kulia ama kushoto zote ni njia maana upande wa kuingilia si mmoja pia

Leo nikisema mimi ntakusemea pia wacha ninene pengine yataenea,ni tumaini langu kuwa baba bora kwa mwanangu,natumaini kilio changu umeniskia,hakuna lazima isiyo kuwa na kutaka,pengine ikiwa umetumainia jambo fulani,na kwa jinsi muda unavyozidi kwenda tumaini hutumika kwa namna tofauti na mwisho wa siku kubaki na hakuna kitu au ukakata tumai kabisa,yenyewe huja na namna yavile ulivyoyatumainia,pengine yalikuwa ni matumaini ya kijinga basi na utajaa ujinga zaidi yake.

Pole leo unalia,pole sana kwa ujinga na matokeo yaliyokukutia,maana katika hali ya kutazama unaweza usieleweke kama pengine ni kilevi cha mwili ama nafsi,maana kupoteza kwa kujua mwanzo na kutokujua kama ulichokuwa unajua ni sahihi hapo utalamba galasha,maana wengi huwa wanakuwa na akili zenye ufahamu wa wao,kila mmoja akiwa na wake lakini wako katika kufikiri ndiyo matumaini yako katika kile unachokiwaza,lolote linalotokea linapimwa na nguvu ya matumini yako hivyo kuwa Kamili.

Thursday, August 30, 2012

MAZINGIRA..


Hili halitahusisha uoto wala namna ya kustiri kupumua ya maana hali kuwa shwari,pengine ikiwa hakuna vita ama ipo ila wanaopigana ni panzi maana wao kufurahi,kuna namna za kutokuruhusu zinazofanya mazingira kuwa mabovu,hii ikiwa wachache wamekalia mazingira ambayo japo watoto wangeweza kucheza,kwa nini tuseme watoto?hapo ndiyo tutagundua na michezo mipya ya kikubwa,maana watoto hucheza na wakubwa kufanya kulingana na mazingira.

Tunapotupa takataka jararani tunayaweka mazingira yapate kueleweka,maana  mahala pataeleweka palivyo,hiyo ikiwa haina wa kusingiziwa kwani aliyetupa ataoneka,pengine wengine wasiwe na uwezo wa kuona,lakini ya kibadamu hapaswi kuachiwa Mungu maana yeye ameyaweza yake.muda unavyosogea wale walio wahi wataonekana kuchelewa kutokana na mazingira yenyewe kuwa machafu,tena hii imezoeleka wote yapaswa kuitwa vichaa kwani hata wanaojifanya kuelewa wameelewa mazingira tofauti.kila mtu ana mazingira yake.

Namna ya kufanikiwa katika maisha haijawa katika kufanikiwa vile ilivyo,maana katika mazingira mengine haipaswi hata kuongozwa,na endapo kutakuwa na kiongozi ni lazima wachaguliwe wale wachafu wanaolipenda jalala kwanza,maana katika mazingira ya uongozi huo kutokufahamika vyema,yaani ikiwa hayaeleweki,kipindi hichi tunatakiwa vijana kujitoa ili kusafisha jalala hilo,maana bila ya harufu ya mauti kutoka wachache wataendelea kutupa taka humo ikiwa wamekalia mazingira kwa kusema ni yao..tukichunguza jalala hili vizuri atajulikana ni yupi anayeongoza kwa utupaji taka bora…huyo anaweza kuwa mchafu zaidi.zaidi ni kumtafutia mahala pa kumtupia alimradi asizidi kuzoeana na uchafu uliopo katika mazingira yake.

Monday, August 27, 2012

KAMA KAWA..


Ni kawaida kwa wanaosema bila ya kusikia maana wao wanajua,pengine ikiwa hata jambo bado kuisha ikasikika na kusemekana kuwezekana.maisha yamekuwa dawa maaana watu wanaumwa bila kujua wanaumwa nini,haiwezekani kwa mwanadamu wa kawaida kujipa ugonjwa na kushindwa kujitibu,maana kama ni mawazo unawaza nini kisichowazuka?wachache waliwaza wakatengeneza magari,ikaja kwa wagunduzi kukatazwa ya kuwa watajawa na ‘stress’,hapo ikiwa inakupasa kuogopa stress,tegemea stress zaidi maana ili iwe kama kawa kuna namna yake ya kujua,hapo huwa imetendeka kwa mara ya kwanza.yaani mapema.

Kama kawa Baraka za kwangu mchache nimezipata,yatafanyika yale yaliyokusudika ikiwa ni mema mbele ya macho ya Yule aliyetuumba,na tena Baraka zenyewe zinapokuja hapo utaskia kama kawa ‘alikuja’,ikiwa mtu amekuwa zaidi ya vile vyema ilivyo,muda mwingine lazima tukubari mateso ili kuja kula raha baadaye,na Yule atakayekuja kudai hizo raha baadaye ni lazima aulizwe tabu amekula kipindi gani,maana kwa wengine taabu ni kama kawa,ikiwa kwa mgeni ana haki ya kushangaa.

Mjini joto limewaka kama kawa,na hii ikiendelea lazima kutafuta zaidi dawa,magonjwa mengine si kwamba yameshindikana bali wagunduzi bado hawajaumwa ugonjwa huo,na pengine ikiwa wameumwa basi waligundua vingine hao..maana siku hizi vikombe watu wanakunywa kama kawa si wakijiamini kwa namna wanavyotembea,ukisahau kujikwaa utaanguka kabisa.maisha ni dawa yahitaji kunywa kujiponya.

Saturday, August 25, 2012

TENDA WEMA NENDA ZAKO..


Hulazimishwi kulia na wakati wewe unataka kufurahi na kucheka,swala la msingi ni kujua unapokatazwa kulia,hapa nikiwa sina maana ya kuhudhunika kwa lile linalokwaza,hakuna baya alitendalo mwanadamu zaidi ya Mungu mwenyewe kujua,maana imekuwa hata nafsi yenyewe ikajitendea mabaya ikiwa wema umezidi sana,maana binadamu umekua unayashika mabaya kuliko yale yaliyo mema ikiwa mabaya hayo yanahesabika ujiulizie mazuri ili ukayatende na uende zako,hapa mtu ukiwa na lengo la kutaka kujua,na sio kushabikia kwani unaweza kushabikia timu alafu ikawa inafungwa kila siku ni sawa na kumsaidia mtu kila siku alafu mwishoni anakufukuza kama mbwa,yakupasa kuacha kushabikia usivyovijua.

Adhabu zote yakupasa kuzitumikia kwani maumivu hujenga,lakini si katika namna ya kutaka kuishi na adhabu hiyo hata kama mema yanahitajika,mwanadamu kila siku anakuwa kwa kusikia na kuona pia unaambiwa maneno mengine siyo ya kuwaambia watoto wako wakiwa hawatakiwi kujua menigne yale,ingawaje ni vyema kumjuza mtoto ili naye akikuwa akatende yale tu yaliyo mema kwake na yakuwa wanadamu hatuna dogo yakupasa kutazama pande ya kule na huku alimradi ikufae.

Shukuru mungu yakuwa unapumua mengine ni ya dunia,songa mbele usikate tamaa kwa kwenda na bila kutenda,kwenda zako isichukulike hasira kwani kesho na kesho kutwa mjinga atafahamu kuandika na kusema shukrani,Mbinguni unaenda kwa ajili ya mazuri na mabaya yako,kama mtu unaamini kule atapata adhabu kwa mabaya yako basi ujue hayo ni ya Mungu asiyoyaruhusu wakati huu uliyasikia lakini hukuyafanyia kazi ama uliyafanyia kazi lakini si sahihi na vile ilivyotakiwa,ya binadamu yanaisha hapa hapa duniani,unapaswa kuwa mwema ili kufanikiwa vyema katika maisha yako na kuleta amani ya moyo na fikra iliyo na  mafanikio makubwa.

MAAJABU...



Kwa Mungu kila goti litapigwa,kila anayetenda atende akijua kwa maana ya kutokupiga magoti tofauti,unaweza kuwa mitamboni na kushindwa kufanya yale yanayotakiwa,pengine ukiwaza mengine ni magumu bila ya kuyapigia goti maana yamekuja yenyewe na kuonekana maajabu,kumbe maajabu ni yale yasiyo na muonekano mzuri pengine ukayashindwa au kufanya wachache kwao ndiyo ikaeleweke kama yalitendeka,imekuwa maajabu ni kitu cha kawaida na hiyo sio kwa upande wangu tu,pengine ikawa haifahamiki,haina haja ya kuumia na wakati inaonekana jambo fulani ni la ajabu,ili labda wengine wasithubutu,maana ukaambiwe ujaribu kwanza.

Katika yale yaliyo marahisi hata yale maajabu huwamo,maana mengine yanahitaji mazoea kwanza,pengine bila kudhani kudharirishwa zaidi ya kuwa shujaa,pengine ukajidharirisha mwenyewe,kwa kuangalia yaliyo ya ajabu unaweza kuona vyema,na hiyo vyema kuja na kuwa uwongo,hapo ukiwa umedanganywa na macho,maana yenyewe yanaona kila kitu,pengine yangekuwa yanachagua basi maajabu yasingeonekana ya nini sasa?

Moyo hufurahi kwa lile linalotendeka,hata likiwa chafu kwa mwengine lakini safi kwako,hii ikiwa unaye ishi ni wewe,pengine hujui kuwa na wengine wanaishi,tena siyo kama wewe wao ni kiajabu ajabu,maana ungelielewa hilo mwanzo.machache yaliyotangulia ndiyo katika yale machache ya maajabu,maana kuna maajabu mengi sana duniani hapa,ikiwa na yenyewe yaliumbwa,hayakuumbwa nasi bali yanakuwa kutokana na sisi.pengine ungalikuwa mtoto bado ungetueleza maajabu uliyotumia kuyaangalia mpaka ulipofikia umri wako,

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...