Saturday, August 25, 2012

MAAJABU...



Kwa Mungu kila goti litapigwa,kila anayetenda atende akijua kwa maana ya kutokupiga magoti tofauti,unaweza kuwa mitamboni na kushindwa kufanya yale yanayotakiwa,pengine ukiwaza mengine ni magumu bila ya kuyapigia goti maana yamekuja yenyewe na kuonekana maajabu,kumbe maajabu ni yale yasiyo na muonekano mzuri pengine ukayashindwa au kufanya wachache kwao ndiyo ikaeleweke kama yalitendeka,imekuwa maajabu ni kitu cha kawaida na hiyo sio kwa upande wangu tu,pengine ikawa haifahamiki,haina haja ya kuumia na wakati inaonekana jambo fulani ni la ajabu,ili labda wengine wasithubutu,maana ukaambiwe ujaribu kwanza.

Katika yale yaliyo marahisi hata yale maajabu huwamo,maana mengine yanahitaji mazoea kwanza,pengine bila kudhani kudharirishwa zaidi ya kuwa shujaa,pengine ukajidharirisha mwenyewe,kwa kuangalia yaliyo ya ajabu unaweza kuona vyema,na hiyo vyema kuja na kuwa uwongo,hapo ukiwa umedanganywa na macho,maana yenyewe yanaona kila kitu,pengine yangekuwa yanachagua basi maajabu yasingeonekana ya nini sasa?

Moyo hufurahi kwa lile linalotendeka,hata likiwa chafu kwa mwengine lakini safi kwako,hii ikiwa unaye ishi ni wewe,pengine hujui kuwa na wengine wanaishi,tena siyo kama wewe wao ni kiajabu ajabu,maana ungelielewa hilo mwanzo.machache yaliyotangulia ndiyo katika yale machache ya maajabu,maana kuna maajabu mengi sana duniani hapa,ikiwa na yenyewe yaliumbwa,hayakuumbwa nasi bali yanakuwa kutokana na sisi.pengine ungalikuwa mtoto bado ungetueleza maajabu uliyotumia kuyaangalia mpaka ulipofikia umri wako,

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...