Wednesday, October 17, 2012

UFALME..

 
Hasa pale ukafika wakati maana ni wazi hata ukiwa mfalme inapasa kuunyofoa ufalme wako,ilifika kipindi kuonekana kufungwa njia katika baadhi ya sehemu,ikiashiria hatari ama kirahisi zaidi ikawa si ruksa kupita,lakini ukiwa mfalme unaruhusiwa kwa kuwa wewe ni mkubwa,zama za kizamani sana ambazo zinafanya watu kuendelea kunyonywa bila ya kujua,eti leo ukapange foleni kwa kuwa umekatika mguu na mwengine akaje ya kuwa jana alikuwa akichezea mtoto kwenye vumbi basi mafua yamemshika sana anaomba kupita,kwa maana ana ahadi  na daktari.
 
 
Kali chache kuliko chungu,maana chungu hazina utamu kama ukali wa uchungu,ikiwa inatakiwa kutizamia mbele siyo kwa kuwa ndiyo unapoelekea,kwani hapo yapasa kutazamia namna ya mwelekeo.ufalme umetawala kwa kila asiye mfalme maana kwa kwenda na nyakati imeonekana ni kheri kuhifadhi kuliko kuweka kwani zikijaa mfalme anaweza kuziihitaji kwa kauli inayosemeka kama amri.
 
 
Pengine leo ikakupase uone ufalme wako,leo ukajifanye ni mfalme wa mambo yako kwani ikiwa tangia uwe mtoa huduma hujafikiri kuunyofoa ufalme,kuondoa lile lililo na uhakika wa kukaa milele kwa vile litajirudia tena,kwa nafasi za ufalme zilizotengwa imeonekana wazi unatembea katika reli isiyokuwa kama tazara..maana unawezajishirikisha kwa kujiona Mfalme bila kujua namna gani ya kuweza kuunyofoa,si mbaya kwa usiye jua kujifanya unajua,maana ndiyo nguvu ya mfalme Juha.

KICHWANI...

Kichwa kinajaa mengi kutokana na namna ya mtu unavyokuwa,ukiwa umelala kubali kuota ndoto maana ndiyo sehemu yake,unaweza kuota mchana kuwa usiku,hapa ni pale unapoiamini ndoto ya uwongo kuwa ya kweli,yaani ni sawa na kulazimisha kuvaa nguo ya mtoto ya jinsia tofauti,sijui ikichanika labda italeta maana,maana wengine huwa kazini wakifanya yao,pengine ukiwa kazini ukifanya yako,yakajaa pengine ya kuwa hakuna sehemu ya hifadhi basi yakabaki katika hifadhi ya kuingia na kutoka.
 
 
Hapa mawazo yanaweza kuongezeka zaidi,maana unaweza kuona kile ambacho hujawai kukiona na kukuta kwamba ni kweli ilipasa kukiona,maana ukiwa hujakiona basi utakiona,hapo ni sawa na mtoto kabla ya ukubwa,ni sawa na mzazi kabla ya uzazi,maana vyote vinapotokea hutokea si katika namna ya kuumizana,bali katika namna ambayo kichwa kinaweza kuyafikiria,kichwa hufikiri kutokana na mtu mwenyewe na wala siyo kitu,maana inaweza kutokea hatari ya kukimbia na kila mtu akakimbia kivyake,hapo kila mtu akiwa ameyajaza yake katika kichwa chake.maana ya mbio kujulikana ni tofauti.mtu hufahamu ukweli wa kitu kwa vile anavyofahamu yeye.
 
 
Hakuna maigizo yanayoweza kuja bila kutoka kichwani,haimaanishi kuigiza kwa vile tunavyofikiria kwa kuanza kutafuta vile vya kweli,ukiwa na imani ya kuona utaona maana kuna walioona lakini hawakuweza kuona,hivyo nikiwa na maana ya nafsi na kichwa cha mtu mwenyewe alivyokijaza,ukijaza mchanga kichwani lazima utakuta umesambazwa na machozi,maana unapofika wakati wa mlima na hata pale wakati wa mteremko,kukiwa na mengi sana mengine hayapaswi kufikirika ikiwa siyo chaguzi lako.
 
 

RADHI...

 
Ikiwa kwa yote yaliyopo, yaliyotokea,yalivyo ama kwa vile tu mtu unavyoweza kumfahamu mwenzako,kwa namna ya kusema na kumjua,ntaomba radhi pale ntakapoyakosea maisha yangu,sifa za kidunia ni jambo jema sana ya kuwa pengine umekuja kwa sababu iliyojengeka na hiyo,ntaomba radhi kwa wachache watakao soma na bila kuelewa kwa sababu kuna wale walioelewa,pengine hakuna maana ya kuelewa tofauti kama hujaelewa hapa ntaomba radhi tena kwa kuwa umeelewa tofauti,
 
 
Raha nyinngine jipe mwenyewe,makosa mengine tatua mwenyewe,wanadamu hawana dogo maana hata ikiwa katika usafiri kuna kubanana na kukanyagana wao watataka radhi,hapa pengine ukiwa na majibu yako kwa kuwa haukuomba radhi mapema na si kwamba ulikosea,bali ni katika namna ya utofauti,kwani unaweza kwenda polini kumkamata simba ili kumfuga naye akakudhuru tena bila radhi kwa sababu ameelewa tofauti nini maana ya adui,radhi si kwa ajili ya kujeruhi tu,hata kwa kuona kwamba imetokea,hapo ukihusisha muda pekee.
 
 
Muda mwingine ni wazi machache hayastahiri kutokea,dunia imeumbika kwa kusema yote ni mazuri na ilikuwa hakuna haja ya kuomba radhi kwa kuwa mti mzuri hutoa matunda mazuri pengine uwe tasa.na kama kuna utasa basi itapasa kuomba radhi kwa kutokufahamika,zaidi maisha yaendelee kwa kuwa kuna mengi ya baadhi ambayo yanaweza kukuletea hadhi.

MBADALA....

Hapa nikiwa nataka mabadiliko,yaliyo katika mazungumzo ama yakabadilika yenyewe kutokana na mfumo wa kubadilisha badilisha unavyoleta mabadiliko,pengine nikiwa sitaki kutoka kwa kuwa kuna mbadala basi ikaje zamu yangu nikaamua kutoka kwa kuwa ilitakiwa kubadilika,kubadilishana maana kukiwa kuna kitu kilishikiliwa,unaweza  unayoyafanya yakawa siyo yale yanayofanyika,hapo mambo yatabadilika kwa matokea halisia.
 
 
Wengi wao wengine hao hufikiri kile cha mtu ndiyo chao,hapo wakifanya mbadala,maana kuna kuwa na mbadala wa kufikiri katika kile kizuri ama kibaya ikiwa vyote ni vitu lakini kukawa na mbadala wa mawazo katika kujua kile ni kizuri ama ni kibaya,pengine ikawa ni kizuri kile kilichosememwa ni kibaya,hapo  ni baada ya kizuri kufanya mbadala na kibaya,pengine endapo  mazingira yamesema.na hapo kunakuwa na mbadala zaidi kwa pale utakapotaka kusema mwenyewe ikiwa tayari mazingira yalishasema..
 
 
Kesho isingeweza kuja bila kubadilishana na siku njema ya leo,hapa ukisema bora kesho maana ya kutokuielewa leo,ama ukaielewa kwa kubadilishana na fikra za kutokuelewa,hapa ukiwa umefanya mbadala wa fikra na zaidi ikatokea katika matendo,kwani mwanzo ilisemwa kwa kuwapo na jambo Fulani,na ukiona mwisho umekuja jua lazima kuna mabadiliko,hayo yakiwa kama siyo kimatendo basi ni namna ya muda ulivyotumika.

UNAPOZUNGUMZA…

 
Wakati na muda unavyokwenda…kwa kuongea mazuri ama  vile ukaja muda ikatulazimu kufanya,ikiwa mwengine akilalama kwa kuzungumza sana akiwa na maana ya kuchoka ya kuwa amezidisha,ukiwa hauhitaji kuongea sana zaidi ya jambo kutendeka,hapa wachache wakikuangalia kama umeweza ama ulikuwa umezungumza tu,hapa wachache watakushangilia ya kuwa umetenda kweli,licha ya kuweza kutokana na baadhi ya nafsi kushindwa kutimiza malengo waliyonayo,na hiyo siyo kwamba wamekuwa wakisema sema bila kufanya,pengine yapasa kufahamu cha kufanya kabla ya kuzungumza.
 
Mara nyingine itakuja kipindi hata yale yasiyo kuwa na maana kwa mtu mmoja kutendeka kwa kuwa mtu  aliyezungumzia ni wa maana,bila kufikiri unaweza kulamba kalata dume,pengine hata ukiwa na mapenzi na hilo dume kwa kuwa na uzalishaji lakini kuna nyingine hufanyika kwa kuwa wachache walishafikiria mwanzo,tena tofauti si kama ilivyozoeleka,hakatazwi mtu kusema bata ni kuku,maana hapo inahitajika sababu,ikiwa kuna wale watakao pata kuwa bata ni kuku na wapo watakao kosa ya kuwa kweli bata si kuku.tunahitaji mazungumzo mazuri.
 
 
Hii imekuwa kama chaguzi maana kuna wengine hutumia kuzungumza wakiwa hawana ya kutenda,kama vifaa hakuna yapasa kuomba kwa jirani akiwa hana kazi navyo,maana baadaye anaweza kusema kwanini hukusema mwanzo,bila kudhani kama mwisho wake ndiyo umefika au ni mwanzo wenyewe maana kuna kuchelewa,,leo unahitaji kusema maana pengine hata ya moyoni yatatoka ikiwa yana milango yake,unapozungumza jaribu kuuweka kuwa ni moyo umezungumza .maana japo tutasubiri kwa kauli ya upendo utakaposema kusubiri.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...