Wednesday, October 17, 2012

KICHWANI...

Kichwa kinajaa mengi kutokana na namna ya mtu unavyokuwa,ukiwa umelala kubali kuota ndoto maana ndiyo sehemu yake,unaweza kuota mchana kuwa usiku,hapa ni pale unapoiamini ndoto ya uwongo kuwa ya kweli,yaani ni sawa na kulazimisha kuvaa nguo ya mtoto ya jinsia tofauti,sijui ikichanika labda italeta maana,maana wengine huwa kazini wakifanya yao,pengine ukiwa kazini ukifanya yako,yakajaa pengine ya kuwa hakuna sehemu ya hifadhi basi yakabaki katika hifadhi ya kuingia na kutoka.
 
 
Hapa mawazo yanaweza kuongezeka zaidi,maana unaweza kuona kile ambacho hujawai kukiona na kukuta kwamba ni kweli ilipasa kukiona,maana ukiwa hujakiona basi utakiona,hapo ni sawa na mtoto kabla ya ukubwa,ni sawa na mzazi kabla ya uzazi,maana vyote vinapotokea hutokea si katika namna ya kuumizana,bali katika namna ambayo kichwa kinaweza kuyafikiria,kichwa hufikiri kutokana na mtu mwenyewe na wala siyo kitu,maana inaweza kutokea hatari ya kukimbia na kila mtu akakimbia kivyake,hapo kila mtu akiwa ameyajaza yake katika kichwa chake.maana ya mbio kujulikana ni tofauti.mtu hufahamu ukweli wa kitu kwa vile anavyofahamu yeye.
 
 
Hakuna maigizo yanayoweza kuja bila kutoka kichwani,haimaanishi kuigiza kwa vile tunavyofikiria kwa kuanza kutafuta vile vya kweli,ukiwa na imani ya kuona utaona maana kuna walioona lakini hawakuweza kuona,hivyo nikiwa na maana ya nafsi na kichwa cha mtu mwenyewe alivyokijaza,ukijaza mchanga kichwani lazima utakuta umesambazwa na machozi,maana unapofika wakati wa mlima na hata pale wakati wa mteremko,kukiwa na mengi sana mengine hayapaswi kufikirika ikiwa siyo chaguzi lako.
 
 

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...