Wednesday, October 17, 2012

UNAPOZUNGUMZA…

 
Wakati na muda unavyokwenda…kwa kuongea mazuri ama  vile ukaja muda ikatulazimu kufanya,ikiwa mwengine akilalama kwa kuzungumza sana akiwa na maana ya kuchoka ya kuwa amezidisha,ukiwa hauhitaji kuongea sana zaidi ya jambo kutendeka,hapa wachache wakikuangalia kama umeweza ama ulikuwa umezungumza tu,hapa wachache watakushangilia ya kuwa umetenda kweli,licha ya kuweza kutokana na baadhi ya nafsi kushindwa kutimiza malengo waliyonayo,na hiyo siyo kwamba wamekuwa wakisema sema bila kufanya,pengine yapasa kufahamu cha kufanya kabla ya kuzungumza.
 
Mara nyingine itakuja kipindi hata yale yasiyo kuwa na maana kwa mtu mmoja kutendeka kwa kuwa mtu  aliyezungumzia ni wa maana,bila kufikiri unaweza kulamba kalata dume,pengine hata ukiwa na mapenzi na hilo dume kwa kuwa na uzalishaji lakini kuna nyingine hufanyika kwa kuwa wachache walishafikiria mwanzo,tena tofauti si kama ilivyozoeleka,hakatazwi mtu kusema bata ni kuku,maana hapo inahitajika sababu,ikiwa kuna wale watakao pata kuwa bata ni kuku na wapo watakao kosa ya kuwa kweli bata si kuku.tunahitaji mazungumzo mazuri.
 
 
Hii imekuwa kama chaguzi maana kuna wengine hutumia kuzungumza wakiwa hawana ya kutenda,kama vifaa hakuna yapasa kuomba kwa jirani akiwa hana kazi navyo,maana baadaye anaweza kusema kwanini hukusema mwanzo,bila kudhani kama mwisho wake ndiyo umefika au ni mwanzo wenyewe maana kuna kuchelewa,,leo unahitaji kusema maana pengine hata ya moyoni yatatoka ikiwa yana milango yake,unapozungumza jaribu kuuweka kuwa ni moyo umezungumza .maana japo tutasubiri kwa kauli ya upendo utakaposema kusubiri.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...