Sunday, February 12, 2012

WATU WANAENDA MAHALA PA KUABUDIA NA HAWAJUI WANAENDA KUFANYA NINI..!


!
Ingalikuwa tumezidiana sana utofauti basi pangekuwa si mahala pale pa heshima kama inavyojulikana,tokea ilipoanza tulijua ni mahala pa kuabudia ikaja hii leo kila mtu akaelewa lake,na hii inatokana na kuwa wote tuna matatizo,tena ndiyo yanayotupelekea kufika mahala pale,ikiwa lengo sio kubishana kama ilivyoeleweka basi na wengine tuelewe tunavyoelewa,ikiwa si lazima kuelewa hivi,vile ambavyo havieleweki.mwanadamu asipokuwa anaeleweka ndiyo mwanzo wa kueleweka,kwani hata tukafikiri kuelewa ni nini tutabaki hatuelewi na wachache wakawa viongozi wa wasio elewa.

Siku ya sita ni ipi ili ya saba nikapumzika?yamebaki mabishano kwa wale wote kuonekana hawana uhakika,mawazo ni yetu ndiyo maana tunayafuata mahala yalipo,kama ni kuyatoa ni pale tulipo,hata tukasema hakuna asiye na mawazo hapo tutakuwa tunayataka,kwani yajapo mengine ya kuyafikiri hatutaelewa hasa zaidi kwa lile lililopo,inakuwa ni rahisi kumwamishia mbwa ujuzi wa binadamu bila ya mwanadamu mwenyewe kujua kama anao huo wa mbwa,kwani ingalikuwa naye mbwa anajua kusema tungaliamuliwa kila mara hata tuwakutapo majalalani,na wao wangechagua cha kula hata kugoma pale kinapokuwa hakiwapendezi,hapa nikiwa na imani kwa Yule mfugaji anao uwezo wa kula zaidi mbwa wake,na kama mbwa huyo kazidi basi jua hayo ni mawazo,tena epuka karibuni waeza kuwa mbwa.


Shetani asemi kwa sauti tukatenda,yupo kimya akisubiri tutende,si anajaribisha?maana anaweza kutumia nguvu zake bure wakati tupo katika upande wake,mahala pengine pana maana zake,maana nyengine zina mahala pake,hata ikawa hatuja maanisha kuwa mahala hapo tutaleta maana zetu,vingi vipo ili kuijaza maana,na maana hukamilika pale inapojazwa,hujazwa pale kitu kinapokuwepo,ni kama pale mahala pa kujisaidia,na hata huwa ni lugha au ni mahala penyewe,maana kama ingalikuwa ni kumfuata na kumwomba mungu kuhusu wokovu inatupasa kufahamu tumeyaacha mengi sana,tunakimbilia matokeo yetu ya yakitutokea tunasema maisha ni magumu,ni sawa na Yule aliyamua kwenda kusomea udaktari hapaswi kugoma kwani hata mhasibu anayempa huo mshahala mdogo akigoma sijui ataupata wapi.na ingalikuwa ni udaktari wake angelibaki huko akijitibu.

Tuheshimu mahala pa kazi,watu wanafanya kazi ili wale,wale wasio fanya na wasile maana hawajatoa taarifa ya kuwepo kwao mahala hapo,tusijichague kwa kwenda na kuongea maneno ya mungu,eti tukajiita tukasema tunajifahamu sisi ni watoto wa mungu,bila kujua kama  ametukubari,eti tukabisha tukisema ni mara ya kwanza,hapa tutakuwa hatuna fikra za nyuma,wale wenye mawazo wanajua nini maana ya mahala walipo.unaweza kuwa mtoto ki umri au rika lakini si vile kwa baba,hapa nazungumzia nyumba hizo..maana wamekuwa wakipiga makelele sana kuwakaribisha watu..bila wageni kujua tuangalie mlangoni wametuandikia kabisa..mgeni njoo mwenyeji apone..sasa anayeponywa sijui ni yupi hapo,lengo hapa sio kukataza,bali ni kujua la kufanya uwapo mahala husika.

By:Benson G.Makaya
Email:bensonsmakaya@gmail.com

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...