Tuesday, February 14, 2012
Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.
Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.: Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi yanayomzun...
MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.
Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa
ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi
yanayomzunguka mwanadamu,likiwa leo limetajwa basi litaenda kwa maana yake,hiyo
hiyo ya ukubwa,ukubwa wa kitu sio uzuri,na ubaya sio udogo pia,yote
yanawezekana,ikiwa tu mlengwa amejua kitu,ameujua ukubwa unaozungumziwa.
Makubwa ni mengi ya kutosha,zaidi umilikisha ukubwa
kukua.ikiwa ni katenda basi ni lazima kufikiri,iwe ni kufikiri vizuri ama
vibaya,bila kujali umri maana na udogo upo hapo,yule anayetenda anafikiri kitu
katika yale aliyonayo,ikiwa ni mara nyingine huwa tunasema mtu amefanya makubwa
baada ya kuona mafanikio,lakini katika kipindi cha kuyaona hayo matendo makubwa
kisiwepo,ikawe ni hali tu iliyokuja na kuweza kuitwa ni kubwa.tulingel bahatisha
kuishi kama tungelikuwa tunayaona makubwa ya wazazi wetu,maana tungelikuwa sawa
sasa,kwani ule ukubwa wao usingekuwa kama udogo wetu na tukasema enzi hizi
zimeharibika sana,vijana wanatembea uchi barabarani ikiwa hawana heshima,na
yule mkubwa aliyefikiria kutokea hayo anahisi mafanikio,kwani alifikiri hivyo.
Ndani ya jamii zetu binadamu wengi tupo sawa,labda
niseme kwa sababu hatuna uhakika ya kuwa tuna utofauti zaidi ya ile ya kike na
uume,maana akiwazacho mtu ndio huleta usawa,ikaja kutokea siku labda tutaulizwa
wale wote wanaofikiria chochote watoke mbele,yule atakaye baki atakuwa lazima
hajasikia,maana kama atakuwa amesikia na amezidi kubaki ni lazima
atajiuliza,asipojiuliza huyo aamshwe,maana amelala,na tuangalie tusije ruhusu
akakoloma zaidi kwani watoto wao wataamka zaidi,watakuwa wamezidishiwa kipimo
cha dawa,na madhara yanaweza kutokea,labda yametokea tayari.
Fikra zetu
zimekuwa zikifananisha mengi sana,ikiwa yule mkubwa akafanye ya kitoto,sio
lazima mkubwa kufanya makubwa lakini kila aliye na umri afanye yake yale yanayo
au yaliyo endana na huo umri wake.,kama ni yalikuwa ya akiba basi ayamalizie
kwani ni maisha yake,maisha,mtu inabidi aishi yeye,sio tuishi kwa sababu ya
binadamu mwingine,na endapo inatokea hivyo basi awe ni mungu pekee,muda uliopo
ni ule uliotengwa,labda tufahamu kwa mitihani yetu tulikuwa tunafanyaje,maana
wengine walianza na maswali magumu na wengine ikawa walijibu wao
wanavyojua.,tena isiwe tukachelewa katika kujibu yale tulioyaona tuna uwezo
nayo,maana itafika kipindi muda ukiisha kila mwenye chake atabaki nacho,haina
haja ya kubebeshana mizigo ikiwa dhambi,na tutakapo zeeka labda tuseme hilo
hatukulifahamu..sijui tufahamu vipi kabla ya uzee,au ndio makubwa zaidi ya
fikra.
Wengi tunafikiria mengi,wengi wakubwa tunafikiria
hadhi yetu ya kuwa wakubwa,wengi watoto wakatamani kuwa wakubwa,ikiwezekana
kama sisi,au wale Fulani wanofanya vitu Fulani,yanayotuletea ukubwa ndio
yanayotusumbua ukubwani,ikiwa na tabia za utotoni hazikuachwa au kutiliwa maanani wakati wa ukuaji,kwani
yaeza kuwa mtu katamani kuwa mkubwa na asielewe kama pale ndio anakuwa,wakubwa
tuliitwa hivyo ni kwa sababu inaeleweka tunafanya nini,mambo wayafanyayo ni
kama yale ya msingi wanayofanya watoto nao wakaitwa watoto.tusiwaumize watoto
kwa kuangalia mawazo ya ukubwa wetu,yanayotatuliwa ndio huwa na mwongozo,ni
fikra zinazohitaji kuwa na uwezo tusije pita mahala palipo na uozo tujijali na
kuyaangalia yetu matendo.
IKIWA ATAKUA MDOGO BASI UKUBWA UTAMFATIA,MWANADAMU
YAANI.
By: Benson G. Makaya,
Tel: +255714
33 66 57.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Makaya's Forum: ELEWA 2
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
POPURAL POSTS
-
Unapokwenda ni sawa,kwa kuwa kila siku kadri ya zinavyokwenda mwanadamu anaishi katika ile hali ya kutokusema kwamba!! na sio haielewe...
-
Hata usipozungumzia utaifa lakini kiwango cha maisha ya mtanzania ni kidogo sana,hapa nikiwa nazungumza na watanzania wale walio na nd...
-
Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahal...
-
WALTER CHILAMBO SPEECHWISE.. NI mshiriki wa EPIC BONGO STAR SEARCH ANAYETOKEA MBEYA,HIVI SASA AKIWA KATIKA FAINALI HIYO ITAKAYO FANYIKA DI...
-
Kuna muda yapasa kujifanya kutokujua kwa kusahau pengine ikiwa ni makusudi ama vile ikawe ni mpango wako mwenyewe,kama ungejulishwa lile...
-
Kufika sio kuwahi yaweza kuwa kuwapo ama kutangulia,na yale yanayotokea sio lazima kupanga kwani mara nyingi tunasema hatupangi sisi za...
-
Yafanye mapito yako kuwa nguvu inayokusukuma kwenda mbele ukitegemea kuishi ndoto zako na sio kile unachokiogopa na kuhofia,wengi hawafanyi...
-
Kufikiri ni kuwa na hitaji la kurekebisha jambo,kunatokana na mawazo,kwa hiyo fikra zinaweza kuwa ni mawazo,kufikiri ni kitendo,kure...
-
Ni namna ya maisha yanavyokwenda,maana leo ikaja lakini siyo kesho,ukawa na hofu ya leo maana ile ya jana nusu imeishia leo.. kama i...
-
Unakasirikia maisha yako wengine wakiwa na furaha,ikiwa lengo si kutaka kuijua furaha ya mwengine bali kujua ni namna gani hasira zako zinak...