Tuesday, February 14, 2012
Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.
Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.: Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi yanayomzun...
MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.
Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa
ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi
yanayomzunguka mwanadamu,likiwa leo limetajwa basi litaenda kwa maana yake,hiyo
hiyo ya ukubwa,ukubwa wa kitu sio uzuri,na ubaya sio udogo pia,yote
yanawezekana,ikiwa tu mlengwa amejua kitu,ameujua ukubwa unaozungumziwa.
Makubwa ni mengi ya kutosha,zaidi umilikisha ukubwa
kukua.ikiwa ni katenda basi ni lazima kufikiri,iwe ni kufikiri vizuri ama
vibaya,bila kujali umri maana na udogo upo hapo,yule anayetenda anafikiri kitu
katika yale aliyonayo,ikiwa ni mara nyingine huwa tunasema mtu amefanya makubwa
baada ya kuona mafanikio,lakini katika kipindi cha kuyaona hayo matendo makubwa
kisiwepo,ikawe ni hali tu iliyokuja na kuweza kuitwa ni kubwa.tulingel bahatisha
kuishi kama tungelikuwa tunayaona makubwa ya wazazi wetu,maana tungelikuwa sawa
sasa,kwani ule ukubwa wao usingekuwa kama udogo wetu na tukasema enzi hizi
zimeharibika sana,vijana wanatembea uchi barabarani ikiwa hawana heshima,na
yule mkubwa aliyefikiria kutokea hayo anahisi mafanikio,kwani alifikiri hivyo.
Ndani ya jamii zetu binadamu wengi tupo sawa,labda
niseme kwa sababu hatuna uhakika ya kuwa tuna utofauti zaidi ya ile ya kike na
uume,maana akiwazacho mtu ndio huleta usawa,ikaja kutokea siku labda tutaulizwa
wale wote wanaofikiria chochote watoke mbele,yule atakaye baki atakuwa lazima
hajasikia,maana kama atakuwa amesikia na amezidi kubaki ni lazima
atajiuliza,asipojiuliza huyo aamshwe,maana amelala,na tuangalie tusije ruhusu
akakoloma zaidi kwani watoto wao wataamka zaidi,watakuwa wamezidishiwa kipimo
cha dawa,na madhara yanaweza kutokea,labda yametokea tayari.
Fikra zetu
zimekuwa zikifananisha mengi sana,ikiwa yule mkubwa akafanye ya kitoto,sio
lazima mkubwa kufanya makubwa lakini kila aliye na umri afanye yake yale yanayo
au yaliyo endana na huo umri wake.,kama ni yalikuwa ya akiba basi ayamalizie
kwani ni maisha yake,maisha,mtu inabidi aishi yeye,sio tuishi kwa sababu ya
binadamu mwingine,na endapo inatokea hivyo basi awe ni mungu pekee,muda uliopo
ni ule uliotengwa,labda tufahamu kwa mitihani yetu tulikuwa tunafanyaje,maana
wengine walianza na maswali magumu na wengine ikawa walijibu wao
wanavyojua.,tena isiwe tukachelewa katika kujibu yale tulioyaona tuna uwezo
nayo,maana itafika kipindi muda ukiisha kila mwenye chake atabaki nacho,haina
haja ya kubebeshana mizigo ikiwa dhambi,na tutakapo zeeka labda tuseme hilo
hatukulifahamu..sijui tufahamu vipi kabla ya uzee,au ndio makubwa zaidi ya
fikra.
Wengi tunafikiria mengi,wengi wakubwa tunafikiria
hadhi yetu ya kuwa wakubwa,wengi watoto wakatamani kuwa wakubwa,ikiwezekana
kama sisi,au wale Fulani wanofanya vitu Fulani,yanayotuletea ukubwa ndio
yanayotusumbua ukubwani,ikiwa na tabia za utotoni hazikuachwa au kutiliwa maanani wakati wa ukuaji,kwani
yaeza kuwa mtu katamani kuwa mkubwa na asielewe kama pale ndio anakuwa,wakubwa
tuliitwa hivyo ni kwa sababu inaeleweka tunafanya nini,mambo wayafanyayo ni
kama yale ya msingi wanayofanya watoto nao wakaitwa watoto.tusiwaumize watoto
kwa kuangalia mawazo ya ukubwa wetu,yanayotatuliwa ndio huwa na mwongozo,ni
fikra zinazohitaji kuwa na uwezo tusije pita mahala palipo na uozo tujijali na
kuyaangalia yetu matendo.
IKIWA ATAKUA MDOGO BASI UKUBWA UTAMFATIA,MWANADAMU
YAANI.
By: Benson G. Makaya,
Tel: +255714
33 66 57.
Subscribe to:
Comments (Atom)
Makaya's Forum: ELEWA 2
Makaya's Forum: ELEWA 2 : Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye n...
POPURAL POSTS
-
Kheri huletwa na mwenyezi mungu,mwanadamu ana kheri ya kuwa na pumzi ambayo humfanya akaweza vile awezavyo kwa Kheri yake Muumba,un...
-
Makaya's Forum: ONA KUSIKIA. : Mapema ni kheri kuona bila ya kusikia,maana haya machache tumeyasikia hapa kwa kuwa yalionekana mwanzoni,...
-
Ni wazi macho hutumika kwa kuangalia,kuona,kutazama yote yakiwa kama ni matendo yake,na hii yote inatokana na namna tofauti ambazo zi...
-
Makaya's Forum: UNDERSTANDING. : We do and say a lot, being that it brings an understanding or misunderstandings within the community, ...
-
NIangalie,Nione ni natumika katika utofauti wa namna gani ikiwa pamoja na mashine au mashine zinatumika ikiwa kama ni mifano yangu,zikim...
-
Hapa nikiwa nataka mabadiliko,yaliyo katika mazungumzo ama yakabadilika yenyewe kutokana na mfumo wa kubadilisha badilisha unavyoleta mab...
-
Nafahamu kwamba katika maisha ya kila siku hayakosekani mambo ya kuumiza. Sina shaka kuugua, kufiwa, kukosa chakula, kusalitiwa katika m...
-
Ikiwa kwa yote yaliyopo, yaliyotokea,yalivyo ama kwa vile tu mtu unavyoweza kumfahamu mwenzako,kwa namna ya kusema na kumjua,ntaomba ra...
-
Thinking is a need to fix something, due to ideas, so the concept may be thinking , thinking is an act, modify it to do, Thoughts are...
-
Pongezi kwenu mliowahi kufika mijini,pongezi kwenu wakulima wale wa mjini na vijijini,maana pongezi kubwa kwa watu wa vijijini,hapa...