Tuesday, February 14, 2012

Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.

Makaya's Forum: MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.: Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi yanayomzun...

MAKUBWA ZAIDI YA FIKRA.


Makubwa ni neno linalosifia kitu,kitu yaweza kuwa ni kitendo,kifaa,mawazo,nafsi ya mwanadamu mwenyewe na mengineyo mengi yanayomzunguka mwanadamu,likiwa leo limetajwa basi litaenda kwa maana yake,hiyo hiyo ya ukubwa,ukubwa wa kitu sio uzuri,na ubaya sio udogo pia,yote yanawezekana,ikiwa tu mlengwa amejua kitu,ameujua ukubwa unaozungumziwa.

Makubwa ni mengi ya kutosha,zaidi umilikisha ukubwa kukua.ikiwa ni katenda basi ni lazima kufikiri,iwe ni kufikiri vizuri ama vibaya,bila kujali umri maana na udogo upo hapo,yule anayetenda anafikiri kitu katika yale aliyonayo,ikiwa ni mara nyingine huwa tunasema mtu amefanya makubwa baada ya kuona mafanikio,lakini katika kipindi cha kuyaona hayo matendo makubwa kisiwepo,ikawe ni hali tu iliyokuja na kuweza kuitwa ni kubwa.tulingel bahatisha kuishi kama tungelikuwa tunayaona makubwa ya wazazi wetu,maana tungelikuwa sawa sasa,kwani ule ukubwa wao usingekuwa kama udogo wetu na tukasema enzi hizi zimeharibika sana,vijana wanatembea uchi barabarani ikiwa hawana heshima,na yule mkubwa aliyefikiria kutokea hayo anahisi mafanikio,kwani alifikiri hivyo.

Ndani ya jamii zetu binadamu wengi tupo sawa,labda niseme kwa sababu hatuna uhakika ya kuwa tuna utofauti zaidi ya ile ya kike na uume,maana akiwazacho mtu ndio huleta usawa,ikaja kutokea siku labda tutaulizwa wale wote wanaofikiria chochote watoke mbele,yule atakaye baki atakuwa lazima hajasikia,maana kama atakuwa amesikia na amezidi kubaki ni lazima atajiuliza,asipojiuliza huyo aamshwe,maana amelala,na tuangalie tusije ruhusu akakoloma zaidi kwani watoto wao wataamka zaidi,watakuwa wamezidishiwa kipimo cha dawa,na madhara yanaweza kutokea,labda yametokea tayari.

Fikra  zetu zimekuwa zikifananisha mengi sana,ikiwa yule mkubwa akafanye ya kitoto,sio lazima mkubwa kufanya makubwa lakini kila aliye na umri afanye yake yale yanayo au yaliyo endana na huo umri wake.,kama ni yalikuwa ya akiba basi ayamalizie kwani ni maisha yake,maisha,mtu inabidi aishi yeye,sio tuishi kwa sababu ya binadamu mwingine,na endapo inatokea hivyo basi awe ni mungu pekee,muda uliopo ni ule uliotengwa,labda tufahamu kwa mitihani yetu tulikuwa tunafanyaje,maana wengine walianza na maswali magumu na wengine ikawa walijibu wao wanavyojua.,tena isiwe tukachelewa katika kujibu yale tulioyaona tuna uwezo nayo,maana itafika kipindi muda ukiisha kila mwenye chake atabaki nacho,haina haja ya kubebeshana mizigo ikiwa dhambi,na tutakapo zeeka labda tuseme hilo hatukulifahamu..sijui tufahamu vipi kabla ya uzee,au ndio makubwa zaidi ya fikra.

Wengi tunafikiria mengi,wengi wakubwa tunafikiria hadhi yetu ya kuwa wakubwa,wengi watoto wakatamani kuwa wakubwa,ikiwezekana kama sisi,au wale Fulani wanofanya vitu Fulani,yanayotuletea ukubwa ndio yanayotusumbua ukubwani,ikiwa na tabia za utotoni hazikuachwa  au kutiliwa maanani wakati wa ukuaji,kwani yaeza kuwa mtu katamani kuwa mkubwa na asielewe kama pale ndio anakuwa,wakubwa tuliitwa hivyo ni kwa sababu inaeleweka tunafanya nini,mambo wayafanyayo ni kama yale ya msingi wanayofanya watoto nao wakaitwa watoto.tusiwaumize watoto kwa kuangalia mawazo ya ukubwa wetu,yanayotatuliwa ndio huwa na mwongozo,ni fikra zinazohitaji kuwa na uwezo tusije pita mahala palipo na uozo tujijali na kuyaangalia yetu matendo.

IKIWA ATAKUA MDOGO BASI UKUBWA UTAMFATIA,MWANADAMU YAANI.

By:          Benson G. Makaya,

Tel:      +255714 33 66 57.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...