Thursday, June 7, 2012

UOTO..

Tusitake ubishi kwa yaliyo matapishi,tusipende upishi kwa walio wabishi,tumeamka leo mapema ikaonekana ni wabishi,tumefanya leo jambo jema isije kuwa watishi,watoto chungeni wazazi wenu wanawaona,wakubwa jiangalieni madogo mumeyaona,tumetoka juzi kufanya bila kujua,tulifahamu juzi kwa watoto walitambua,mizigo  midogo vyombo vikubwa visije ungua,uadilifu mdogo tuyaangalie makubwa yatatuumbua..

Samaki mkunje akitaka akikatika amezeeka,samaki mbonye  akiweza kaoza,ona tumekuja leo bila kuzoza,wachache jitayarisheni mje kutuongoza,tumesubiri sana tusije kupuuza,watoto kaeni wazazi kuwatunza,wazazi kaeni chinjo wakubwa wamekuwa,tusiseme kwa sasa ya kuwa tumejipiga msasa,tusiseme ya sasa kwani yametungoja sana


Vichwa vitakuja na kuwa wangu mkia,watoto watakuwa bila ya salamu kuwatamkia,haki iacheni mwenyezi akatubarikia,mabaki yaacheni maana wasije kututapikia,wachache waacheni maana matusi watatutamkia,haki ya nani wa kwanza kashika mkia,haki ya Fulani wa mwisho atapaswa kutuamkia,adhabu hapewi mtu akafa akafia,adhabu hapewi mtu yakaja yakamfikia.

Tunaondoka tukienda tukisema,tunaenda tukiondoka tukihema,mazoezi yamekuwa mazito kwa watoto na kunena,mapenzi yamekuwa mazito kwa Fulani kunisema,haki hawa watoto wa vizito sio tukiwasubiri tutawasoma,haki wa kwa watu wenye vibito kwa foleni hawatagoma.mtoto subiri haya magali yamegoma,ingekuwa kiroboto asingesubiri kwa magodoro kuyachoma.

Ndoto zikamilike kwa watoto,uoto uelimike hata kwa viboko..

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...