Saturday, March 17, 2012

NI SAWA..


.......tunapokwenda ni sawa,kwa kuwa kila siku kadri ya zinavyokwenda mwanadamu anaishi katika ile hali ya kutokusema kwamba!!
na sio haieleweki,kwani kwa wasio elewa ni lazima kubisha na kwa yule abishaye asome,aone ili aje ahakikishe ni vigumu kuhakikisha kitu ambacho kipo hapa yaani ni wewe ujuaye usawa wake,na sisemi kibaya kwani sio changu..hapa tunaweza kuleta ugomvi na tuelewe yasiyoeleweka yanatoka wapi?

Tuwakumbuke wenye miwani,tusielewe kwamba hawataona,elewa kwamba watahitaji kuangalia zaidi,
labda kuna muda na akili ivae miwani pia,ile kama unazuia jua usiku.
Haya ya kila siku ni magumu kuyafuatilia,ingawa kila siku tunakaa tukifuatilia mambo ili tufanikiwe kwa kile kitakacho onekana,
tusione nyuma.tujaribu kule kunakoonekana,siwakatazi wale wanaorudi nyuma na kuokota vile walivyovidondosha,au kusahau,wakitumia nguvu nyingi wakiacha mengine ya muda husika yanaendelea
Masikini hafirisiki,maskini ni yule mtafutaji,maana anatafuta nini sasa?na akakae kila siku akitafuta bila kujali ni lisilo na muda au halieleweki,maskini anayetafuta huelewa yote

uelewa kuwa yasiyoeleweka ni yale anayoyafahamu ambaye hajaelewa,
ni ruksa kubwa kuunga mtaji kwa maskini kuliko kwa tajiri maana kwa tajiri pale itakuwa ni kuungwa,labda iwe tajiri naye  ni maskini katika nafsi,na ili tuelewe vingine vipo kwa nini,kuwe na vitu vinavyoeleweka ,tuwashe moto bila mafuta na tuone kama hautachoma nyumba,
hapa tusije singizia ni vyanzo vingine,maana sijui zamani walitumia nini..au ni mayai haya?


ukipanda mti na ule mkavu tegemea,
mapya yapo na isije wengine wakaitwa wao ni wa kila siku,labda wazoefu..maana na mambo yenyewe yanabadilika bila taarifa,ikiwa yanaweza kuwa ya kisasa au ya kizamani anayeyabadilidha ni nani?
maana sisi tumekuwa hatubadiliki,yaani tupo vile vile,hivyo ndivyo wasemavyo waungwana.pengine maskini kuwa tajiri yakuwa imeonekana maskini wengi wanatamani hivyo,tajiri hawezi kutamani kwani ametoka huko.

ingawaje tama inafanya kazi popote,labda tuseme itakuwa sio kila siku,maana hapa tutaepuka ubishi na wale wasio elewa wakati haya ni mambo yao.
Naweza kusema yetu au yangu pia pale yatakapo nishinda yale yangu,hata nisiposema sifai kuchekwa kwani nani anayafahamu haya yangu?ni sawa na kumshangaa yule anayeelewa akiwa anaomba msaada wa kueleweshwa,hata tukasema kwamba Fulani huelewi naye akakataa,
usishangae amekataa ni kwa sababu haelewi

Mengi hatuyafahamu...Tutakufa Maskini...!!
by:Benson G.Makaya
tel:+255714336657
email:bensonsmakaya@gmail.com


No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...