Tuesday, January 16, 2024

ISHI NA YAKO

Watakwambia unabahati kwakile ulichokifanya kilichokufanya uwepo hapo,kujipa ufalme na kuzungumzia maisha ya mwengine kwa kuwa umefika mahala fulani,tambua maisha yana stepu,uliyopo sasa mwengine alipita juzi ukicheka leo mwenzako kulia ni sawa na kulia wakati mwenzako anacheka.

Usibabaike na waliowahi kufikia ukitakacho,tambua muda wako ikiwa unajiandaa jiandae vyema ili ukikosa isiwe lawama kwa wengine,maana imekuwa mmoja akishindwa akatoa sababu za mwengine kumuangusha.

Usifikiri ni raisi kukaza jambo,kuna mengine yanakaza mpaka kufungua inakuwa kama ni kukaza,ujiandae vyema maana kuna vilio,maumivu yasiyo na machozi na hata usumbufu usiohitajika.yatambue magumu yako na jipe muda kuyatatua ikiwa humu duniani wote mpaka muda huu tunatafuta maisha.

Kheri udongo unarudi utokapo maana ingekuwa foleni kubwa barabarani kwa kuwapa heshima wajionao miungu,usifikiri wakati wa magumu peke yake mwishowe ukawapa lawama watu wasio husika na maisha yako,tambua nafasi yako si ile aisemeayo mwengine,watu huwa wanaongezea kwa kile ulichonacho.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...