Friday, February 17, 2012

Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.

Makaya's Forum: USHINDI…UNAHITAJI KUJIANDAA.: Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiw...

USHINDI UNAHITAJI KUJIANDAA.

Maandalizi ni malengo katika kutekeleza yale yanayotaka kufanyika,ikiwa katika mmoja mmoja hadi pale ikafikia kundi,hii yote hutokana ikiwa kila mmoja aliyepo naye akiwa na timamu ya kutaka kufanya jambo lisiloonekana na likaonekana kama ni jambo limefanyika,ikiwa tu,kwake naye lilikuwa ni lengo.katika kujiandaa kuna mengi ili kufikia mwisho,mwisho ndio timilisho la maandalizi ikiwa hapo ndio tunaweza kujua kama ni maandalizi yalikuwa mazuri au la kuwa vyote hivyo inategemea na mtu kufuatana na (ma)lengo lake,USHINDI ni pale mtu anapotimiza lengo,ikiwa tu alijiandaa,hata mara nyingine ushindi huja kwa watu wasio jiandaa,na hiyo siyo ya kuitegemea ikiwa ni bahati,wala hatuwezi kusema ushindi usio kuwa wa kutegemea ni ule wa kukosa.tuna hitaji ushindi ili kutekeleza mambo yetu,tunahitaji kujiandaa ili tuweze kushinda.

useme ni wangapi wanaojiandaa,na utakuta ni wote maana kila mtu ajiandaaye hujiandaa mwenyewe,yule anayeandaliwa ni lazima ajue kuandaa pia kwani endapo akishinda hataweza kuulinda ushindi ya kuwa hana maandalizi useme wale wanaoamka ndio wa kuweza kujiandaa kwani walikuwa wamelala,na wale walio lala ni kuwaamsha ili waweze kujiandaa ikiwa ushindi mtu anaupata pale hasa alipojiandaa mwenyewe,maana unaweza kuja kidogo ama ukazidi na kufanya karaha,kivingine ikawe ni ile bahati maana haukuwa wa maandalizi yale,ushindi wa bila kuongea unaweza usisikike,na mara nyingine ukiongea sana wanaweza kunyamazisha,maana wao hawamjui mungu na labda nisiseme hivyo zaidi iwe wanamjua mungu wao.pale unapokosa ndio pale majibu yalipo,ni kama pale unapopata ingawa haitaweza kulingana,ni tofauti ya kuwa moja ni ushindi nyingine ni kinyume yake.

Kile kinachoweza kuzuilika ni kile kisichopangika,maana kitakaaje?kama maji hupita kokote,hata yakaleta uharibu hata ikawe sio lengo kubomoa,pale yanapobomoa yenyewe ushinda ikiwa yalipotoka yalikuja na yakabomoa,labda yangeenda pengine ili ungejua kuwa haikuwa lengo,na iweje yangefanikiwa ungeeiita ni bahati yake,kwa yule anayejenga ukuta kwa ajili ya kuzuia maji hayo anajiandaa,kwa yule anayeyasubili yaingie mpaka ndani basi atafanikiwa,maana amesubiri hivyo,muda mwingine huwa inakuwa haiwezekani,ikiwa katika hali ya kawaida hasa mtanzania ikiwa wengi hatufahamu mazingira yetu,ikiwa ni miili pekee tunayoifahamu,tukisahau mazingira mengine tukataka afya bora,hii itakuja kwa kunenepa ikiwa ni bora basi itakuwa bahati,siwezi kusema sana hapa labda tungeulizana nani au na flani wanapenda nini,maana utofauti upo,na matokeo sio maandalizi,ikiwa yenyewe yakawe na kusudio la kuleta ushindi.

Vizuizi ni haki kuviweka pale unapojiandaa.lakini ni pale tu utakapo jua ni unazuia nini,Katika utofauti wa malengo tuseme yawe yanayofaa yote,yakitofautiana kwa mabaya na mazuri kwani tunaweza kuchanganyana kwa muda mbadala,endapo yale yasiyokuwa ni malengo kufanyika kama malengo wakati Fulani,yule anayejiandaa ndiye anayejua lengo hasa,labda na ije tofauti..hapo tunasema anapanga mungu.
mda mwingine lawama hazifai labda ujue nini unachokifanya,maana kama ni unajiandaa na imetoka kipindi maandalizi yakawa magumu unaweza kuyakimbia endapo haujafahamu unajiandaa na nini, 

'tutaishia kunawa maji ikiwa na chakula tumekiona mbele yetu'.
kwani hata meza zenyewe waligeuza kitambo!!

By:          Benson G, Makaya,
Tel:         +255 714 33 66 57.
email.   bensonsmakaya@gmail.com

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...