Wednesday, August 8, 2012

VIJANA MSILIE..



Haina haja ya kutoa machozi wakati unayeishi ni wewe mwenyewe,haikuwa na maana ya kutafuta na kufika mahala fulani,serikali ikiwa sio baba wala mama yako,serikali ukiwa ni wewe na unahitaji kusaidia wananchi wasiojiweza,msilie wale wa mbagala mabomu,msilie enyi wataifa kama wafuasi wa kibwetele,utamaliza nguvu zeko bure,maana anayetakiwa kusikia ameongeza sauti ya kutokusikia,ukisema umechoka kwa yale uliyoyalilia,ni baada ya kuwa magumu na ahadi wengi umewapatia.

Unakaukiwa maji mwilini na mabomba yamekatwa,ikiwa maisha ya chini ya mtanzania ni chini ya dora,yanashida sana kwa ajili ya kuongezeka kuwa mengi hapo wengine watalia wakitaka usaidizi bila kujua wamejijazia wenyewe,haitaleta maana.ukiwa mwalimu ni lazima utengeneze pesa kupitia mlango mwengine,swali linakuja ni unawezaje kutengeneza?maana yeye akafundishe kufanya biashara na asifanye,unawezaje kukaa na kuja na majibu mazuri ambayo yasikufanye ukalia,hapo ni swala la mwalimu kukubali kusoma yale ya duniani,kama umegundua kitu hakiendi ni heri kukiacha maana kitakuliza sana.

Duniani kuna lile la ukitaka kuwa na pesa ni lazima ukae katika mchezo wanaotengenezea pesa,hapa labda kimazingira maana kuna mahala pesa zinamwagika kama vile zinatengenezwa,yale ya msingi yakiwa bado hayajafanyiwa kazi,ukiwa nje tu utaskia pale ni pazuri,ni kwa sababu ya kuutambua uzuri,usiende na maisha yako na baadaye kuwapa watu lawama,kama ulishazaliwa na unakuwa jua wewe ni wewe,jitambue.hata ukitokwa machozi hutafutw, wachache sana,na ukisema hafadhari ya kwa heri,maana huko unakoelekea yaweza ukatoa machozi sana,kwa vile ilivyo hata haikutegemeka.

ASILI...


Hii ikiwa ni kama tabia lakini pengine hapa tukajumuisha wengi,
hapa ikawa ni mazoea kwa kuwa wengi huwa wanatumia kufanya hiyvo,sio ya kwamba wamekosa au hawajafuata maelekezo ni namna ya vile ya asili ya waliopo juu wanavyofanya maana hata katika nafasi ndogo ilibidi wafanye wale wa hali ya chini sasa wakubwa wanafanya,hivyo inaleta kulalama kwa kuwa hali ni ngumu,tulipotoka ni mbali wala haina haja ya kuyakumbukia labda tusubiri matokeo maana tulishalalamika kabla ya kufanya.

Tunapopaza sauti kwa kutaka kusikika ni namna ya vile kutumia nguvu kubwa wakati safari ni ndogo,
pale tunapohitaji kutulia na kufanya yale tunayoyaweza yanakuwa magumu yakuwa yalizoeleka ni mengine,
ikiwa asili imepoteza maana yake,na asili sio mtu zaidi ya mtu vile alivyo,maana kila mtu anafanya vile katika wakati na mlengo wake,tunapokuwa tunaheshimu asili zetu tunajua kile tunachokiwaza,
ikiwa ni mafanikio na maono ya kufika pale unapohitaji kwa undani na kukufanya ujiskie vizuri.

Maisha ya mwanadamu hayajaumbwa kwa shida,labda pengine tumechelewa,na hivyo ikiwa tunaishi tofauti na asili zetu,sio kwamba kujiskia vizuri ndiyo kuwa na asili nzuri,pengine asili haina maana kwa kuwa unaishi kwa namna unavyoishi,hapo ukiwa umechagua kufurahia maisha yako.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...