Wednesday, August 8, 2012

ASILI...


Hii ikiwa ni kama tabia lakini pengine hapa tukajumuisha wengi,
hapa ikawa ni mazoea kwa kuwa wengi huwa wanatumia kufanya hiyvo,sio ya kwamba wamekosa au hawajafuata maelekezo ni namna ya vile ya asili ya waliopo juu wanavyofanya maana hata katika nafasi ndogo ilibidi wafanye wale wa hali ya chini sasa wakubwa wanafanya,hivyo inaleta kulalama kwa kuwa hali ni ngumu,tulipotoka ni mbali wala haina haja ya kuyakumbukia labda tusubiri matokeo maana tulishalalamika kabla ya kufanya.

Tunapopaza sauti kwa kutaka kusikika ni namna ya vile kutumia nguvu kubwa wakati safari ni ndogo,
pale tunapohitaji kutulia na kufanya yale tunayoyaweza yanakuwa magumu yakuwa yalizoeleka ni mengine,
ikiwa asili imepoteza maana yake,na asili sio mtu zaidi ya mtu vile alivyo,maana kila mtu anafanya vile katika wakati na mlengo wake,tunapokuwa tunaheshimu asili zetu tunajua kile tunachokiwaza,
ikiwa ni mafanikio na maono ya kufika pale unapohitaji kwa undani na kukufanya ujiskie vizuri.

Maisha ya mwanadamu hayajaumbwa kwa shida,labda pengine tumechelewa,na hivyo ikiwa tunaishi tofauti na asili zetu,sio kwamba kujiskia vizuri ndiyo kuwa na asili nzuri,pengine asili haina maana kwa kuwa unaishi kwa namna unavyoishi,hapo ukiwa umechagua kufurahia maisha yako.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...