Sunday, August 5, 2012

MIPAKA..


Leo imefika tunagombana kwa yale tuliyoyashindwa jana,pengine haikuleta faida sana,ama hasara ikiwa endapo kama tunaweza kukaa na mali na bila ya kuziendeleza basi ni tumeshindwa kabisa,hii ikiwa mali zenyewe zinaendelezeka,inapofika mwisho wa jambo ni haki kuweka alama ikiwa ni kwako,hii haki..maana ni dhuruma kwa mwengine kuichukua.tusifikiri tumeishi zamani  na ya kutamani tutayaweza,zisije fikra zenyewe kwani wengine wameshasema wakijiandaa mapema.leo ikiwa mwisho kulipia haina maana ya kesho usilipe,ila kama ilichukulika bila ya malipo ya kuelewana kuna uwalakini wa kutokuelewana zaidi,hasa mzazi anapomwambia mwana mpaka wako wa kucheza ni mwisho hapa.

Ni wazi ya kuonekana hayafichiki,tuseme vingine vipo wazi lakini vinahitaji ubishi,maana kama kuna kukubari haraka haraka hata itakuja siku tuwakatae wazazi wetu,kama walivyo wengine tayari kuona mipaka yao kwa wazazi wao,maana  mmoja atasema huyu sio mama yangu na mwengine atasema wala baba.hapo tukivuka mipaka bila  ya kufahamu kama mwisho wa safari ndiyo mwanzo maana yapasa kujipanga upya.

Leo unaweza kugombana sana,pengine watakufa wachache na kwa wengine ikawa maana,
maana unaweza kujiuliza tangia siku zote hizo ulikuwa wapi?
hapa ikiwa  tunataka sababu.kama kwa mungu hakuna mipaka basi hakuna anayejua,
maana hii yetu sijui tumeitoa wapi ikiwa bado tutaendelea kung’ang’ania hata vile visivyo vyetu,mwishoni kueleweka mambumbumbu kwani hata na kuingia shuleni hakuna cha zaidi ya kufanyia tulichojua zaidi ya mipaka ya shule yenyewe,unapoambiwa uingie chumbani kwa baba sio uzungu ni muvi za video tu hizo,waache wakubwa wanaongea watafikia mwisho wa mipaka yao.

No comments:

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...