Monday, October 9, 2023

Makaya's Forum: NAONA

Makaya's Forum: NAONA: Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni ...

NAONA

Naona umekalia mguu wako ukijaribu kutupa mkono kulia ili usaidie kusimama na mguu wa kushoto,naona ukiambiwa acha kwa kuwa hujajua kuwa ni moto na unaunguza,Naona vingi ukipata uelewa ntakuelewesha.

Naona wamefunga milango wakijua upo nje,wamefunga njia ikiwa bado haujapita,wanakusema unakonda kwa kukataa kunywa uji,naona ukisoma herufi bila ya kuelewa,umeanza kuita mma ukijua ni uhai,naona chuki juu ya moyo mkunjufu,Subiri ukipata uelewa ntakuelewesha.

Naona hujajua kama sufuria sio kikombe,hujajua mtu anayesubiria hakupata hajapata sifuri,usikimbilie kuendesha vitakavyo kuendesha,subiria kupandishwa basi likisimama utashushwa,Unapokula usijichafue sana meza wapo wabaya watu wanaotafuna vya kumeza.

Naona unaanza kuelewa ya msingi,ukitaka kujisaidia waogope watu na isiwe kwa chuki ,kama umekuwa jua safari unaiweza na unapoelekea naona safari ndo inaanza,Naona unashindwa kufanikiwa kwa fitina nyingi,vita zipo nyingi kaa mbali na maadaui,binadamu yoyote anaweza kuwa adui bila hata wewe kutaka,naona unakuwa msuruhishi mbele ya ndugu zako na sio kuwagandamiza.

Kesho naiona tena,naliyaona ya jana yakanipa majibu ya kuwa mtihani ni ule ule.naona yake akae nayo yako baki nayo mwenyewe ili kutokuchanyikikika,Naona unakanyaga maji na hakuna sehemu yenye moto ,Naona nisikuchoshe Sali sana kaa mbali sana na ndugu msumali.

Thursday, October 5, 2023

NEEMA YA MUNGU

 Neema ya Mungu haipangwi na mwanadamu ,maana siwezi kuomba na kutaka nijibiwe kesho ama muda ule nitakaotaka ikiwa naamini Mungu anapenda maisha yangu na yupo bize kuhakikisha shetani hanichukui moja kwa moja,

Ufahari na mafanikio  unaweza kuwa hitaji la kila mmoja lakini vitu hivyo vinagharama na unaweza kulazimisha kugharamia ukawa navyo lakini ukakosa namna ya kuendesha na kufurahia uliyochonacho,ikawe muomba jiwe akapewa mkate.

Namshukuru Mungu hata nisingekuwa hapa,naishi vile Mungu ametaka na ifike kipindi nisisahau wala kudharau kusali na kumwomba kwa kuwa yeye ananipenda,anabadili kile kitu kinachosumbua nafsi yangu ,anajua ninachohitaji na muda wa kunipa.

Najua maisha yangu hayajabadilika hivi hivi bila neema ya Mungu,pale ninapo muomba ananipa,anabadilisha mazingira.Hata kesho sitasimama peke yangu maana ndiyo umenifikisha hapa nilipo,

Maombi mengine ukatizwa na hofu na kuzuia neema zisikudondokee,namuomba Mungu nifanye tofauti na hofu ilivyo iwe kutaka,kuendea na kukipata kukiwa na maono juu ya kile ninachokihitaji,

Ndoto hata ikifeli moja ntaota tena maana neema yako Mungu haina muda kamili,muda wa kupata kitu zaidi kile mtu usichokidhania.

ELEWA 2

  Mateso ya moyo huudhoofisha undani wa mwili,unaweza kubadili mwelekeo hata ule uliotakiwa kuelekea baadaye na kukataa kuelekea hata kwa ku...